Posts

RAIS SAMIA ANAAMINI KATIKA USHIRIKIANO NA VIONGOZI WA DINI - DKT. BITEKO

Image
  📌Atoa pole kwa Familia, KKKT kifo cha Askofu Sendoro 📌Kanisa Lashauriwa Kumuenzi Askofu Sendoro kwa Vitendo 📌 Waumini Waaswa Kuishi Maisha ya Kumpendeza Mungu Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali ipo tayari kushirikiana na viongozi wa dini ili kuwawezesha kutimiza majukumu yao ya kitume kwa maendeleo ya Watanzania. Dkt. Biteko amesema hayo leo Septemba 17,  2024 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya Mwanga, Kanisa Kuu lililopo Mkoani Kilimanjaro wakati akitoa salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya ibada ya mazishi ya aliyekuwa Askofu wa Dayosisi hiyo, Chediel  Sendoro. Askofu Sendoro amefariki  dunia kwa ajali ya gari iliyotokea Septemba 9, 2024  katika eneo la Kisangiro wilayani Mwanga.  “ Rais yupo tayari kushirikiana na kanisa wakati wowote ili kanisa liweze kufanya kazi zote za kitume na sisi tuk

SERIKALI YAJIPANGA KUTOKOMEZA MAGONJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE

Image
  Na Mwandishi wetu Dar  Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria ifikapo 2030 kutokomeza maambukizi ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele kwenye halmashauri zote nchini humo ili kuwakinga wananchi wake na magonjwa hayo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Afya Jenister Mhagama amesema wanatarajia hadi kufikia mwaka 2027 wawe wamevuka asilimia 95 kuelekea kutokomeza magonjwa hayo pamoja na kufanya vizuri licha ya kuwepo changamoto mbalimbali ikiwemo fedha. Amesema kuwa katika kukabiliana na changamoto ya kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele, Serikali ya uingereza imekuwa ikiisaidia wizara ya Afya, ambapo leo wamekutana na mkamwana wa mwana mfalme wa Uingereza ili kujadili magonjwa yasiyopewa kipaumbele ikiwemo mabusha, matende na vikope (Trachoma) "Leo tumekutana na huyu mke wa mtoto wa mfalme ili kuonyesha maeneo ambayo tumefanya vizuri, kwani Shirika la Afya duniani linataka ifikapo mwaka  2030 tuwe tumeshapambana na magonjwa hay

MKURUGENZI WA KAMPUNI YA GREEN HIPPO TRAVEL AZURU MAKUYUNI WILDLIFE PARK

Image
Astaajabishwa na wingi wa vivutio na kuahidi kuwahamasisha wageni mbalimbali kutembelea eneo hilo Mkurugenzi wa Kampuni mashuhuri  ya utalii inayofahamika kama Green Hippo Travels, Astrid Kleinveld akiwa ameambatana na rafiki yake  Naomi Rugenbrink ambao wote ni raia wa Uholanzi,   tarehe 15 septemba 2024, walitembelea eneo la Makuyuni Wildlife Park liliopo wilayani Monduli mkoani Arusha kujionea vivutio mbalimbali vilivyopo na kupata fursa ya kufahamu namna wanavyoweza kufanya biashara ya utalii katika eneo hili hasa  utalii wa Kupanda Mlima na Kutembea kwa miguu. Bi Astrid na mwenzake wakiongozwa na Afisa Utalii wa eneo hilo Chacha Masase walipata fursa ya kupanda Mlima Kipara ambao unapatikana ndani ya eneo hilo wenye urefu wa mita 1900 kutoka usawa wa bahari pamoja na kufanya utalii wa Kutembea kwa miguu hivyo kufanikiwa kuona wanyamapori kwa ukaribu zaidi na kufurahia mandhari iliyopo. "Uzuri wa eneo hili ni wa kustaajabisha mnoo, tumepata uzoefu wa kipekee ambao nina imani s

KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI NLD ASISITIZA WATAFANYA KAMPENI ZA BUSARA ZA

Image
Na Ombe kilonzo Zanzibar Katibu wa Uenezi na Itikadi wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Ahmed Salim Hamad, akizungumza katika kikao cha ndani na viongozi wa chama hicho kutoka Chaani, Zanzibar, alisisitiza kuwa kampeni za chama hicho zitaendeshwa kwa njia ya amani. Mhe. Ahmed aliwataka viongozi wa NLD Zanzibar kuongozwa na busara wanapoeneza sera na itikadi ya chama cha NLD,  Alisisitiza, "Chama cha NLD kitaendesha kampeni za busara, kuepuka uchochezi, udanganyifu, au vurugu, na badala yake tutaweka msisitizo kwenye hoja na sera, kwani NLD Ina sera nzuri kuliko chama chochote nchini." Aliwahimiza viongozi wa NLD kuhakikisha wanajenga mahusiano bora na wananchi wa ngazi za chini, akiwataka viongozi hao kuelewa matatizo ya wananchi na kuonyesha suluhu ya matatizo kupitia sera za chama cha NLD. "NLD haitaki kuwa kama vyama vingine vinavyolalamika bila kutoa njia za kutatua matatizo ya wananchi." Alisema Mhe. Ahmed. Chama cha NLD kipo kwenye Ziara ya

HUU HAPA UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO LEO SEPT 12,2024

Image
 

KIKOSI CHA AFYA JESHI LA POLISI KIMEZINDUA KAMPENI YA KUPIMA AFYA BURE KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA POLISI

Image
  KAMISHNA Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Abdallah Mpallo amesema jamii ijitokeze kupima afya  kwenye kambi zinazokuwa kimeandaliwa ili kuikomboa afya na magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza. Mpallo ambaye pia anatoka kikosi cha afya alisema katika kuelekea kilele cha wiki ya Polisi shughuli mbalimbali zimefanyika ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za Afya kwa kupima magojwa mbalimbali. Mpallo alisema hayo leo Septemba 11, 2024 wakati akimuwakilisha Kamanda wa Kikosi cha Afya Naibu Kamishna wa Polisi, DCP Lucas Mkondya. "sisi kama kikosi cha polisi tumelenga kutoa huduma za vipimo bure kwa watu wote ili kutambua afya zao na endapo mtu atagundulika kuwa anahitaji matibabu makubwa zaidi atapewa rufaa ya kwenda hospitali kubwa ilikuendelea na matibabu zaidi. Pia tunatoa elimu kuhusu magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza hasa namna ya kijikinga na homa ya nyani (Mpox). ACP. Mpallo alisema katika kambi hiyo itatolewa elimu hukusu mguu kifundo kwani watu wengi uamini kuwa ulema

WAZIRI JAFO: WIZI WA KUCHEZEA VIPIMO NI KOSA KISHERIA

Image
 Na WMA, Mwanza Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo amehimiza wananchi jijini Mwanza kuzingatia matumizi sahihi ya vipimo kila mara wanapofanya manunuzi na kuuza bidhaa mbalimbali. Aliyasema hayo Septemba 11, 2024 wakati akifungua rasmi Maonesho ya 19 ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayofanyika katika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza.  "Wizi wa kuchezea vipimo ni kosa kwa mujibu wa Sheria ya Vipimo Sura Na. 340 na hata vitabu vya dini vinakataza wizi wa vipimo," alisisitiza. Katika hatua nyingine, akizungumzia ushiriki wa Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho hayo, Afisa Vipimo Mwandamizi Mkoa wa Mwanza, Lazaro Joram alisema ni mwendelezo wa utoaji elimu kwa umma kuhusu matumizi sahihi ya vipimo kwa wafanyabiashara waliopo ndani ya Mkoa wa Mwanza pamoja na nchi jirani. "WMA tunatumia Maonesho haya ili kuwawezesha wadau wetu kutambua majukumu yetu, kueleza umuhimu wa kuhakiki na kutumia vipimo sahihi na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya matumizi ya vipim