Na Mwandishi wetu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameipongeza Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa mageuzi makubwa iliyofanya katika mashirika ya umma. Mhe. Kikwete alitoa pongezi hizo Ijumaa, Julai 4, 2025, alipotembelea banda namba 39 (Ukumbi wa Kilimanjaro) katika maonesho ya 49 ya biashara maarufu kama Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam. “Tunaishukuru Ofisi ya Msajili wa Hazina chini ya uongozi imara wa Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, kwa kuwezesha taasisi za umma kuongeza ufanisi wao,” alisema Mhe. Kikwete. Aliongeza: “Wote ni mashahidi, katika uongozi wa awamu ya sita chini ya Mhe. Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan, tumeshuhudia mabadiliko makubwa ya kiutendaji katika taasisi za umma.” Ofisi ya Msajili wa Hazina imewezesha kuimarika kifedha kwa mashirika ya umma yaliyokuwa na mitaji hasi na yaliyokuwa yanapata hasara mfululizo, ambapo sasa yameweza kuondokana na utegemezi wa ruzuku ya Ser...