Posts

DKT. KIJAJI AIPA TANO BODI YA TAWA

Image
Na, Sixmund Begashe, Arusha Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), imepongezwa  kwa ubunifu wake katika utekelezaji wa majukumu yake  yaliyosababisha mafanikio katika uhifadhi na Utalii nchini.  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, ametoa pongezi hizo leo Januari 08, 2026 Jijini Arusha wakati akipokea taarifa ya  utekelezaji kazi wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA inayomaliza muda wake.  Dkt. Kijaji amesema ubunifu katika utekelezaji wa majukumu ya Bodi hiyo, umeendana sambamba na maono ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya uhifadhi endelevu wa urithi wa  rasilimali kwa maslahi ya vizazi vijavyo na Taifa kwa ujumla.  Ameongeza kuwa pamoja na mambo mengine, Bodi hiyo  imewezesha  kuongezeka kwa  wawekezaji na mapato kusababisha kuimarika kwa uhifadhi, kupungua kwa uvamizi katika maeneo ya hifadhi na mapori tengefu pamoja na kuimarisha matumizi y...

MAAFISA 84 NA ASKARI 48 WA TAWA WATUNUKIWA VYEO VYA UHIFADHI

Image
  Na Beatus Maganja, Morogoro Kaimu Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Mlage Yussuf Kabange, Januari 07, 2026 aliwatunuku na kuwavisha vyeo vya uhifadhi Maafisa 84 na Askari 48 wa taasisi hiyo, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya TAWA mkoani Morogoro. Akitoa nasaha zake kwa Maafisa na Askari hao, Kamishna Kabange aliwapongeza kwa kufikia hatua hiyo muhimu katika utumishi wa umma, huku akiwaagiza kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, nidhamu na kwa kuzingatia maadili pamoja na taratibu za kijeshi. Aidha, Kamishna Kabange alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kutoa kipaumbele kwa Maafisa na Askari wa uhifadhi kupandishwa vyeo sambamba na utoaji wa ajira mpya. Alisema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025 na 2025/2026, TAWA imepewa kibali cha kuajiri jumla ya Maafisa na Askari 550, hatua inayoongeza morali kwa wahifadhi, kupunguza changamoto za rasilimali watu,...

TUNA DENI LA KUSIMAMIA MIRADI NA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI ILI KULETA MAENDELEO YA KWELI–MHE. SALOME

Image
  Aanza ziara ya kikazi mkoani Shinyanga kukagua miradi ya nishati Ataka changamoto za wananchi zitatuliwe kwa wakati Siku 100 za Rais Samia Umeme kuwashwa kwenye vitongoji mkoani Shinyanga SHINYANGA Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa la kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo sambamba na kusikiliza pamoja  na kutatua kero za wananchi ili kufanikisha maendeleo ya kweli. Mheshimiwa Salome ameyasema hayo leo tarehe 8 Januari, 2026, mkoani Shinyanga wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali ya nishati inayotekelezwa mkoani humo.  Amesema wananchi wana imani kubwa na Serikali yao, hivyo ni wajibu wa viongozi kuhakikisha changamoto zinazojitokeza zinatatuliwa kwa wakati. Ameongeza kuwa katika siku 100 za Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan Wizara ya Nishati imejipanga kuhakikisha umeme unawashwa kwenye miradi ya vitongoji mkoani Shinyanga ili kuwawezesha wananchi kunufaika na huduma hiyo muhimu kwa ...

MRADI WA TAZA KUFUNGUA SOKO JIPYA LA BIASHARA YA UMEME AFRIKA

Image
Wafikia asilimia 83 Dkt. Mataragio akagua mradi na kutoa maelekezo TANESCO TAZA kuunganisha Mkoa wa Rukwa na gridi ya Taifa Kuimarisha upatikanaji umeme Mikoa ya Kusini mwa Tanzania Mbeya Imeelezwa kuwa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Zambia kupitia Tunduma (TAZA) umefikia asilimia 83.45 huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Mei 2026 na hivyo  kufungua soko jipya la biashara ya umeme barani Afrika. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo leo Oktoba 23, 2025 katika eneo la Iganjo, Mbeya, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amesema mradi wa TAZA ni muhimu kwa Taifa kwa kuwa utaiunganisha Tanzania na Nchi za ukanda wa Kusini mwa Afrika (Southern Africa Power Pool) na pia kuimarisha muunganiko wa ukanda wa Mashariki mwa Afrika (East Africa Power Pool). “Nimshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya nishati. K...

DKT. MATARAGIO AAGIZA VIFAA VYOTE VYA UHAKIKI WA JOTOARDHI ZIWA NGOZI KUFIKA KWA WAKATI

Image
Ni baada ya kukagua mradi na kukuta baadhi ya vifaa bado havijafika Asisitiza mradi kukamilika kwa wakati ikiwa ni  utekelezaji wa Sera ya Nishati ya mwaka 2015 Kazi ya uhakiki wa Jotoardhi Ziwa Ngozi yafikia asilimia 60 Mbeya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Kampuni yake Tanzu ya Uendelezaji Jotoardhi (TGDC)  kuhakikisha kuwa vifaa vyote vya uhakiki wa rasilimali Jotoardhi  katika mradi wa Ziwa Ngozi  vinafika kwa wakati ili kazi za uhakiki  ziweze kumalizika kulingana na muda uliopangwa. Dkt. Mataragio ametoa maagizo hayo leo Oktoba 22, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua kazi zinazoendelea kutekelezwa katika mradi huo wilayani Rungwe mkoani Mbeya. “Huu mradi mnapaswa kuukamilisha kwa wakati kutokana na umuhimu wake nchini, tunapotekeleza miradi hii ya Jotoardhi tukumbuke kuwa tunatekeleza pia Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015 ambayo inasema Tanzania inapaswa izalishe umeme kwa ku...

TAMASHA LA NYAMAPORI CHOMA LAVUTA UMATI TABORA ZOO

Image
Zaidi ya watalii 500 wafurika kuonja ladha ya nyama pori na burudani za uhifadhi Na Mwandishi Wetu, TABORA Zaidi ya watalii 500 wamefurika leo, Oktoba 18, 2025, katika Bustani ya Wanyamapori Tabora (Tabora Zoo) kushiriki katika Tamasha la Nyamapori Choma lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Kanda ya Magharibi. Tamasha hilo lililolenga kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na matumizi endelevu na halali ya rasilimali za wanyamapori, limevutia watalii  kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi, likihudhuriwa na viongozi wa Serikali wakiwemo Wakuu wa Wilaya za Tabora na Uyui, wananchi wa Mkoa wa Tabora na mikoa jirani, pamoja na wageni kutoka mataifa mbalimbali duniani. Wananchi waliohudhuria tamasha hilo wameipongeza TAWA kwa ubunifu wa kuandaa tukio hilo, wakieleza kuwa limewapa fursa ya “kuonja ladha ya matunda ya uhifadhi” unaotekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali hizo Kwa nj...

DOYO: AMANI NI NGUZO KUU YA MAENDELEO NA MAPINDUZI YA UCHUMI TANZANIA

Image
  Dar es Salaam  Mgombea urais kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, na Katibu Mkuu wa chama hicho, amewataka Watanzania kudumisha amani kabla, na baada ya uchaguzi mkuu ujao, akisisitiza kuwa amani ndiyo nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote duniani. Akizungumza jijini Dar es Salaam katika muendelezo wa kampeni za chama hicho zinazofanyika kwa mtindo wa “mobile kampeni”, Doyo alisema chama chake kimefanya kampeni za kistaarabu na kisayansi katika mikoa 26 mpaka sasa. Alisema kampeni hizo zimekuwa zikiwalenga wananchi moja kwa moja ili kuwapa sera na kuelewa changamoto zao bila kutweza utu wa mtu. “Niwaombe sana, Watanzania wenzangu, mkapige kura kwa amani. Mkivunja amani, hakuna maendeleo yatakayopatikana. Amani ndiyo tunu ya taifa letu,” alisema Mhe. Doyo. Doyo alifafanua kuwa amani ni sharti muhimu la maendeleo. Alisema pale ambapo amani ipo, ndipo serikali inaweza kutekeleza kwa ufanisi ahadi zake kwa wananchi, ikiwemo kuboresha hud...