Posts

WANAOTAKA KUHARIBU UCHAGUZI MKUU WAONYWA, VIJANA WA CCM WACHARUKA

Image
Na Mwandishi wetu Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam wamewaonya wanasiasa na wanaharakati wanaohamasisha wananchi wasishiriki Uchaguzi Mkuu kwani ni dai la kikatiba na sio matakwa ya mtu binafsi. Akizungumza na  Waandishi wa habari Makao Makuu ya UVCCM Jijini Dar es salaam,mmoja wa Vijana hao Isack Sumbali amesema kuwa mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi yamefanyika kwa kiasi kikubwa ikiwemo Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) kubadilishwa nakuwa Tume huru ya Taifa ya  Uchaguzi(INEC). Amesema kuwa, tume miongoni mwa mabadiliko ni pamoja na kua na uhuru wa vyanzo vya mapato, ambapo awali ilikua haiwezi kujiendesha kwa fedha za ndani,na kutegemea ufadhili kutoka UNDP, ambapo uchaguzi mkuu wa mwaka huu utagharamiwa na fedha za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha Sumbali amesema kuwa kwa sasa Uhuru wa Tume hiyo umeongezeka katika sehemu kuu mbili ambazo ni uhuru wa kitaasisi na uhuru wa kiutendaji,pamoja na kutungwa Sheria maalumu inayoongoza kupatikana kwa...

TANESCO YAWAPA SOMO WENYEVITI WA MITAA WILAYA YA KINONDONI NA UBUNGO

Image
Shirika la umeme TANESCO leo limekutana na wenyeviti wa mitaa kutoka Wilaya ya Kinondoni na Ubungo lengo ikiwa ni kutoa elimu kwa watendaji hao kwani shirika hilo asilimia kubwa utendaji unaanzia kwenye mitaa. Akifungua kikao kazi hicho, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Altbert Chalamila  kilichoandaliwa na TANESCO kwa ajili ya Wenyeviti wa Serikali za mitaa kutoka Halmashauri za Manispaa ya Kinondoni na Ubungo amesema wenyeviti wa Serikali za mitaa ni wadau muhimu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Serikali kwa kuwa miradi hutekelezwa katika maeneo yao. "Hata miradi mingi ya TANESCO iko kwenye mitaa hivyo, ni imani yangu kuwa kupitia kikao kazi hiki wenyeviti wote wanakwenda kuwa mabalozi wa kueleza huduma nzuri zinazotolewa na TANESCO pia kulinda miundombinu ya Shirika hilo"amesema RC Chalamila. Aidha ameipongeza TANESCO kwa kuona umuhimu wa kukutana na kundi hilo muhimu ili liweze kufahamu kwa kina majukumu ya shirika hilo lakini pia kutoa mawazo na ushauri wa namna b...

DKT ABAS AHAMASISHA WATANZANIA KUTEMBELEA TABORA ZOO

Image
  Dkt. Hassan Abbasi Ahamasisha Watanzania Kutembelea Tabora ZOO, Aahidi Maboresho Makubwa Zaidi ya Miundombinu. Na Mwandishi wetu, Tabora  Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, Juni 23, 2025 alifanya ziara katika bustani ya wanyamapori ya Tabora, maarufu kama Tabora ZOO, kwa lengo la kukagua na kuona usimamizi wa bustani hiyo ambapo alitumia fursa hiyo kuwahamasisha Watanzania hususani wa ukanda wa magharibi, wakazi wa Mkoa wa Tabora na Mikoa ya jirani kutembelea kivutio hicho cha kipekee ambacho kipo Katikati ya Mkoa wa Tabora. Katika ziara hiyo, Dkt. Abbasi ameonesha kuridhishwa na uwepo wa bustani hiyo ambayo ni hazina ya vivutio vya wanyamapori na mazingira asilia. Ameeleza kuwa Tabora ZOO ni sehemu muhimu ya utalii wa ndani ambayo Serikali imejipanga kuhakikisha inafanya maboresho makubwa ya miundombinu ili kuvutia watalii wengi zaidi. "Hii ni Hifadhi ya kipekee, kuwa na eneo la heka zaidi ya 27 Katikati ya Manispaa ya Tabora au mji ni jambo k...

WAZIRI MKUU MAJALIWA AZINDUA MITAMBO 10 YA UCHORONGAJI KWA WACHIMBAJI WADOGO

Image
Asisitiza dhamira ya Serikali kuwainua wachimbaji wadogo kiuchumi Mitambo Yagharimu shilingi bilioni 12.41 STAMICO yasaini mkataba wa ushirikiano na VETA Dodoma, Katika mwendelezo hatua za Serikali kuendelea ya kuimarisha sekta ya wachimbaji wadogo nchini, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amezindua rasmi mitambo 10 ya uchorongaji kwa ajili ya wachimbaji wadogo yenye thamani ya shilingi bilioni 12.41 iliyonunuliwa na Serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) sambamba na vitendea kazi vya Shirika hilo kwa ajili ya kuimarisha utendaji kazi wa Shirika.  Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo Juni 24, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali, wadau wa madini, wachimbaji pamoja na wananchi. Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kwa dhati kuwawezesha wachimbaji wadogo il...

SEKTA YA NISHATI YACHANGIA ASILIMIA 14.4 YA PATO LA TAIFA

Image
Kapinga ampongeza Rais, Dkt. Samia kwa uwekezaji mkubwa katika Sekta ya Nishati Aeleza mafanikio yaliyofikiwa katika Umeme, Gesi Asilia na Mafuta Asisitiza kuwa Nishati ni moyo wa uchumi Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Sekta ya Nishati ni moja kati ya Sekta tatu nchini ambazo zimechangia ukuaji wa pato la Taifa katika kipindi cha kati ya mwaka 2015 hadi 2025. Kapinga ameyasema hayo wakati akichangia hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mipango na Uwekezaji Bungeni Jijini Dodoma.  "Mheshimiwa Mwenyekiti ukiangalia kwa tathmini kati ya mwaka 2024 hadi 2025 Sekta ya Nishati imefanya vizuri katika kuchangia pato la Taifa, Sekta hii imetoka asilimia 5.8 mwaka 2015 na sasa hivi tunazungumzia asilimia 14.4”. Amesema Mhe. Kapinga Ameongeza kuwa, Sekta ya Nishati imeweza kufanikiwa kutokana na uwekezaji mkubwa unaofanyika katika miradi ambapo  amepongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa uwekezaji huo mkubwa. "Katika Gesi na Mafuta y...

UJENZI KITUO CHA KUPOZA UMEME NKANGAMO-MOMBA KUKAMILIKA MEI 2026

Image
Naibu  Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema ujenzi wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Nkangamo- Momba  unatarajiwa kukamilika Mei mwakani. Kapinga ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Momba, Condester Sichalwe (CCM) ambaye aliuliza ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha kusambaza umeme Nkangamo – Momba.  Kapinga amesema ujenzi wa kituo hicho cha Nkangamo - Momba ulianza mwezi Mei, 2024 ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 30.

DKT MPANGO ATEMBELEA KAMPUNI YA KIMATAIFA YA UZALISHAJI VIFAA TIBA NCHINI ITALIA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametembelea Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji Vifaa Tiba ya Health 3000 iliyopo Roma nchini Italia leo tarehe 23 Juni 2025. Makamu wa Rais amefanya mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Maurizio Flammini pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Bi.Eleonora Flammini. Mazungumzo hayo yamelenga ushirikiano baina ya Tanzania na Kampuni ya Health 3000 hususani katika matibabu kwa njia ya mtandao (Telemedicine). Kampuni hiyo ni moja ya Makampuni yaliyo chini ya mwamvuli wa FG Group ambayo imejikita katika kutoa huduma za afya hususani uzalishaji wa vifaa tiba kwa kutumia teknolojia za kisasa. Makamu wa Rais yupo nchini Italia kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na mikutano mbalimbali ya uwili.