Na Mwandishi wetu Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, amevitaka vyama vya siasa nchini kujiepusha na lugha za matusi, kashfa, uchochezi au vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga amani na utulivu wa taifa la Tanzania hasa kuelekea uchaguzi Mkuu. Wito huo ameutoa jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi kwa viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa ambapo amesisitiza kuwa vyama vya siasa vina wajibu wa kuendeleza misingi ya amani na mshikamano wa taifa. Amesema kuwa, viongozi wa vyama vya siasa nchini ni vyema kuhakikisha kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 zinafanyika kwa kistaarabu, bila kutumia lugha za matusi, kashfa au vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha tunu ya amani Taifa iliyopo. "Nendeni mkafanye kampeni za kistaarabu mkiwanadi wagombea wenu, kuweni na lugha nzuri za kuzungumza, epukeni matusi, lugha za kashfa, kwani amani ya taifa hili ni muhimu kuliko chochote"mesema Jaji Mutungi. Ameongeza kuwa, amani na mshika...