Posts

MRADI WA TAZA KUFUNGUA SOKO JIPYA LA BIASHARA YA UMEME AFRIKA

Image
Wafikia asilimia 83 Dkt. Mataragio akagua mradi na kutoa maelekezo TANESCO TAZA kuunganisha Mkoa wa Rukwa na gridi ya Taifa Kuimarisha upatikanaji umeme Mikoa ya Kusini mwa Tanzania Mbeya Imeelezwa kuwa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Zambia kupitia Tunduma (TAZA) umefikia asilimia 83.45 huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Mei 2026 na hivyo  kufungua soko jipya la biashara ya umeme barani Afrika. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo leo Oktoba 23, 2025 katika eneo la Iganjo, Mbeya, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amesema mradi wa TAZA ni muhimu kwa Taifa kwa kuwa utaiunganisha Tanzania na Nchi za ukanda wa Kusini mwa Afrika (Southern Africa Power Pool) na pia kuimarisha muunganiko wa ukanda wa Mashariki mwa Afrika (East Africa Power Pool). “Nimshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya nishati. K...

DKT. MATARAGIO AAGIZA VIFAA VYOTE VYA UHAKIKI WA JOTOARDHI ZIWA NGOZI KUFIKA KWA WAKATI

Image
Ni baada ya kukagua mradi na kukuta baadhi ya vifaa bado havijafika Asisitiza mradi kukamilika kwa wakati ikiwa ni  utekelezaji wa Sera ya Nishati ya mwaka 2015 Kazi ya uhakiki wa Jotoardhi Ziwa Ngozi yafikia asilimia 60 Mbeya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Kampuni yake Tanzu ya Uendelezaji Jotoardhi (TGDC)  kuhakikisha kuwa vifaa vyote vya uhakiki wa rasilimali Jotoardhi  katika mradi wa Ziwa Ngozi  vinafika kwa wakati ili kazi za uhakiki  ziweze kumalizika kulingana na muda uliopangwa. Dkt. Mataragio ametoa maagizo hayo leo Oktoba 22, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua kazi zinazoendelea kutekelezwa katika mradi huo wilayani Rungwe mkoani Mbeya. “Huu mradi mnapaswa kuukamilisha kwa wakati kutokana na umuhimu wake nchini, tunapotekeleza miradi hii ya Jotoardhi tukumbuke kuwa tunatekeleza pia Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015 ambayo inasema Tanzania inapaswa izalishe umeme kwa ku...

TAMASHA LA NYAMAPORI CHOMA LAVUTA UMATI TABORA ZOO

Image
Zaidi ya watalii 500 wafurika kuonja ladha ya nyama pori na burudani za uhifadhi Na Mwandishi Wetu, TABORA Zaidi ya watalii 500 wamefurika leo, Oktoba 18, 2025, katika Bustani ya Wanyamapori Tabora (Tabora Zoo) kushiriki katika Tamasha la Nyamapori Choma lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Kanda ya Magharibi. Tamasha hilo lililolenga kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na matumizi endelevu na halali ya rasilimali za wanyamapori, limevutia watalii  kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi, likihudhuriwa na viongozi wa Serikali wakiwemo Wakuu wa Wilaya za Tabora na Uyui, wananchi wa Mkoa wa Tabora na mikoa jirani, pamoja na wageni kutoka mataifa mbalimbali duniani. Wananchi waliohudhuria tamasha hilo wameipongeza TAWA kwa ubunifu wa kuandaa tukio hilo, wakieleza kuwa limewapa fursa ya “kuonja ladha ya matunda ya uhifadhi” unaotekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali hizo Kwa nj...

DOYO: AMANI NI NGUZO KUU YA MAENDELEO NA MAPINDUZI YA UCHUMI TANZANIA

Image
  Dar es Salaam  Mgombea urais kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, na Katibu Mkuu wa chama hicho, amewataka Watanzania kudumisha amani kabla, na baada ya uchaguzi mkuu ujao, akisisitiza kuwa amani ndiyo nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote duniani. Akizungumza jijini Dar es Salaam katika muendelezo wa kampeni za chama hicho zinazofanyika kwa mtindo wa “mobile kampeni”, Doyo alisema chama chake kimefanya kampeni za kistaarabu na kisayansi katika mikoa 26 mpaka sasa. Alisema kampeni hizo zimekuwa zikiwalenga wananchi moja kwa moja ili kuwapa sera na kuelewa changamoto zao bila kutweza utu wa mtu. “Niwaombe sana, Watanzania wenzangu, mkapige kura kwa amani. Mkivunja amani, hakuna maendeleo yatakayopatikana. Amani ndiyo tunu ya taifa letu,” alisema Mhe. Doyo. Doyo alifafanua kuwa amani ni sharti muhimu la maendeleo. Alisema pale ambapo amani ipo, ndipo serikali inaweza kutekeleza kwa ufanisi ahadi zake kwa wananchi, ikiwemo kuboresha hud...

TMA YATOA MWELEKEO WA MVUA ZA MSIMU NOV 2025 HADI APRIL 2026

Image
  Na Mwandishi wetu, Dar Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa mwelekeo wa mvua za msimu wa Novemba 2025 hadi Aprili 2026, ikibainisha kuwa maeneo mengi ya nchi yanatarajiwa kupata mvua za chini ya wastani hadi wastani, hali ambayo inaweza kuathiri shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii, hususan katika sekta za kilimo, mifugo, maji, nishati, afya na usalama wa chakula. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus B. Chang’a, amesema mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba katika mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma, na kusambaa kwenye maeneo ya kusini mwa nchi kufikia Novemba 2025, huku zikitarajiwa kuisha kati ya mwisho wa Aprili na mwanzo wa Mei 2026. Dkt. Chang’a amefafanua kuwa msimu wa mwaka huu utatawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha, ingawa nusu ya pili ya msimu (Februari – Aprili 2026) inaweza kuwa na ongezeko la mvua ikilinganishwa na nusu ya...

WAZIRI MKUU MAJALIWA APONGEZA WIZARA YA NISHATI KWA USIMAMIZI THABITI WA MIRADI

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amepongeza Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa utekelezaji na usimamizi miradi mbalimbali ya nishati nchini. Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo leo jijini Tanga wakati akifunga Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Chakula ya Duniani ambayo leo yamefikia kilele chake. Mhe. Majaliwa amesema kuwa usimamizi mzuri wa miradi ya Nishati umepelekea wananchi kuendelea kupata huduma bora. Katika maadhimisho hayo ya Siku ya Chakula Duniani yaliyoanza tarehe 10 Oktoba 2025 yamepelekea wananchi kupata elimu kuhusu mafanikio ya sekta ya nishati na miradi inayoendelea huku wananchi 500 wakinufaika na mitungi ya gesi iliyokuwa ikiuzwa kwa bei ya Ruzuku ya shilingi 17,500/=. Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amekabidhi tuzo kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikiwa ni kupongeza juhudi za taasisi hiyo kupitia maadhimisho hayo ya Siku ya Chakula Duniani.

REA YANG'ARA MAONESHO YA WIKI YA CHAKULA TANGA

Image
Waziri Mkuu aitunuku REA tuzo ya pongezi kwa uhamasishaji wa matumizi nishati safi Majiko ya gesi 500 yauzwa kwa bei ya ruzuku kwenye maonesho Asisitiza kulinda mazingira na kuacha ukataji wa miti hovyo Tanga Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hapa nchini. Mhe. Majaliwa amebainisha hayo leo terehe 16 Oktoba 2025 alipotembelea banda la REA wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Chakula Duniani 2025 yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya Usagara jijini Tanga. Katika hatua nyingine, Mhe. Majaliwa ameipatia tuzo ya pongezi REA ambapo imeibuka kuwa mshindi wa pili wa banda bora katika kuhudumia wananchi katika maadhimisho ya Wiki ya Chakula yaliyofanyika mkoani humo. Naye, Mhandisi kutoka REA, Ramadhan Mganga amesema Rais Samia ni kinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini na kuwataka wananchi kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Sul...