Posts

VETA MTWARA YAJA NA UBUNIFU HUU SABASABA

Image
Chuo Cha Elimu ya Ufundi Stadi (VETA) Mtwara kimeshiriki katika maonyesho ya sabasaba ambapo kinawaomba wazazi na walezi kuwapeleka watoto wai kushiriki katika maonyesho hayo ili waweze kufaidika. Hayo yamebainishwa Julai 4,2025 Jijini Dar es salaam  na Msanii mahili kutoka Chuo hicho Saidi Chilumba wakati akizungumza na Waandishi wa Habari waliotembelea bandi la VETA  katika maonyesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba   "Wewe kama ni mtengenezaji wa kitanda chonga na kinyago,ukiwa unasubiri mteja wa kitanda sasa unao uwezo mwingine wa mimsubiri mteja wa kinyago."amesema Chilumba  Hata hivyo, amesema kuwa Lakini pia wameongeza thamani kwenye vitu mbalimbali Kwa mfano tunatengeneza henga za nguo(Hooks) mafundi wa kuchomelea wanatupa baadi ya vipande vya  chuma  ambavyo wanaona wao  havina thamani, kwahiyo sisi tunavigeuze tunatengeza structure kama ya kipepeo kama unavyoona,tumechora tingatinga." Anasema fikiria kutoka shilingi 5...

VETA SONGEA YAWAFIKIA WATOTO SABASABA

Image
Na Fatma Ally  Chuo Cha Ufundi Stadi Songea (VETA) katika kuwa wabunifu kwenye maonesho ya 49 ya kimataifa imekuja na Kona ya watoto ambapo wataweza kujifunza vitu mbalimbali kupitia maonesho hayo. Akizungumza na Matukio Daima Media Mwalimu Faulata Mutalemwa kutoka Songea alipokua katika maonyesho ya 49 ya kimataifa ya biashara amesema miongoni mwa mambo ambayo watoto wanaweza kujifunza ni pamoja stadi za mikono. Aidha, amesema lengo la kuibua vipaji na kuwafundisha misingi ya maishakupitia kona hiyo ya watoto wanajifunza vitu mbalimbali ikiwemo stadi za mikono mbalimbali na kuondoka nazo. Aidha ametaja stadi hizo amesema ni pamoja na ushonaji, urembo pamoja na masuala ya umeme. "Kupitia kona ya watoto mtoto anaweza kujifunza vitu mbalimbali vya namna ya kuchana nywele, kutunza ngozi yake, namna ya kushona nguo zake pamoja na kudhiifadhi"amesema Mutalemwa. Aidha ametoa wito kwa wazazi, walezi kutembelea katika Banda la Veta ili watoto wao waweze kujifunza vitu mbalimbali vina...

FCC YAISHUKURU SERIKALI KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI KWA WAWEKEZAJI

Image
  Na Fatma Ally Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Nchini (FCC) Hadija Juma Ngasongwa amesema tume hiyo, inajivunia na kuishukuru  Serikali kuweza kutengeneza mazingira rafiki  ya wawekezaji kuhakikisha mwekezaji wa ndani anaweza kupata fursa zinazopatikana na ufanyaji wa biashara na mazingira mazuri yaliyowekwa na Serikali. Hayo ameyasema wakati alipotembelea banda la Viwanda na Biashara katika maonyesho ya 49 ya biashara kimataifa (Sabasaba) ambapo amesema FCC itaendelea kutimiza maagizo ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuimarisha hali ya biashara nchini. Aidha amesema, wawekezaji wa ndani ya nchi wanasimamiwa na sheria madhubuti zinazosimamia uwekezaji ili kusaidia kulinda na kuimarisha biashara zao. "Lengo la kuanzishwa kwa Tume ya Ushindani(FCC) ni kusimamia na kuhimarisha ufanyaji wa biashara nchini, kulinda walaji dhidi ya mienendo potofu ya hali ya ufanyaji biashara kati ya kampuni na kampuni,pamoja na kudhibiti bidhaa bandia."amesema Ngasongwa Hata hivyo, ...

VETA MKOMBOZI WA VIJANA, MCHORA RAMANI KWA MIGUU ANAELEZA

Image
  Na Mwandishi wetu  Katika kuhakikisha vijana wanapata ajira Chuo Cha Ufundi stadi (VETA) kimekua kikitoa fursa mbalimbali kwa vijana wa rika tofauti ili waweze kujikomboa kiuchumi na kujipatia kipato. Ukosefu wa ajira imekua ni changamoto kubwa inayowakabili vijana wengi, Joseph Joachim Mtei anaeleza namna alivyoingia Veta na kupata ujuzi wa kuchora ramani za majengo kwa kutumia miguu . "Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Chuo Cha Ufundi stadi VETA Dodoma, ni mlemavu ambae sina mikono lakini natumia miguu yangu kufanya shughuli zangu za uchoraji wa majengo".amesema Aidha, ameishauri jamii kuacha kuwaficha watu wenye ulemavu nabadala yake wawapeleke VETA wapate ujuzi utakao wasaidia kujikwamua kiuchumi. Rai hiyo, ameitoa wakati akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima Media alipotembelewa katika banda la Veta lilikopo katika maonyesho ya 49 ya kimataifa ya biashara (Sabasaba). Aidha amesema amekwenda katika maonesho ya Kimataifa ya kibiashara maarufu kama Sabasaba kuwaone...

WAZIRI KIKWETE AIPA TANO OFISI YA MSAJILI WA HAZINA

Image
  Na Mwandishi wetu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameipongeza Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa mageuzi makubwa iliyofanya katika mashirika ya umma.  Mhe. Kikwete alitoa pongezi hizo Ijumaa, Julai 4, 2025, alipotembelea banda namba 39 (Ukumbi wa Kilimanjaro) katika maonesho ya 49 ya biashara maarufu kama Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam. “Tunaishukuru Ofisi ya Msajili wa Hazina chini ya uongozi imara wa Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, kwa kuwezesha taasisi za umma kuongeza ufanisi wao,” alisema Mhe. Kikwete. Aliongeza: “Wote ni mashahidi, katika uongozi wa awamu ya sita chini ya Mhe. Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan, tumeshuhudia mabadiliko makubwa ya kiutendaji katika taasisi za umma.” Ofisi ya Msajili wa Hazina imewezesha kuimarika kifedha kwa mashirika ya umma yaliyokuwa na mitaji hasi na yaliyokuwa yanapata hasara mfululizo, ambapo sasa yameweza kuondokana na utegemezi wa ruzuku ya Ser...

WAZIRI RIDHIWANI ATOA WITO KWA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZILIZOPO

Image
Na Mwandishi wetu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete ametoa wito kwa vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo ikiwemo mikopo na mifuko mbalimbali ya uwezeshaji wananchi kiuchumi. Mhe. Kikwete ametoa wito huo wakati alipotembelea Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuuu lililopo katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa SABASABA, leo tarehe 04 Julai, 2025 Jijini Dar es Salaam.  “Serikali imeendelea kutenga fedha kuhakikisha makundi mbalimbali yananufaika, kwa mfano kupitia maelekezo ya kisera kwenye Sheria ya PPRA imeelekezwa asilimia 30  ya manunuzi yote ya umma ipelekwe katika kusaidia makundi ya Vijana, akinamama na Wenye Ulemavu," ameeleza Mhe. Ridhiwani. Aidha, ameongeza kuwa upo mfuko maalumu wa kusaidia watu wenye ulemavu,  lakini pia upo mfuko wa vijana na mfuko wa uwezeshaji wananchi kiuchumi, hivyo mifuko yote hiyo kama vijana na  wananchi  wakiikimbilia hakika vilio vya uwezeshaji havitawe...