MSHINDI WA KWANZA KUJINYAKULIA MILL 10, NGAO NA CHETI TUZO YA MWALIMU NYERERE

Na Mwandishi wetu Tuzo ya kitaifa ya Mwalimu Nyerere ya uandishi wa bunifu itatolewa April 13 jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa super Dome Masaki ambapo itahusisha mkusanyiko wa mashairi, tamthilia, hadithi za watoto na Riwaya . Aidha, mshindi wa kwanza wa tuzo hiyo atajinyakulia kitita cha shill mill 10, ngao pamoja na cheti na muswada wake utachapishwa na kusambazwa shuleni na kwenye maktaba za taifa, Mshindi wa Pili: Tuzo ya Shilingi Milioni 7 pamoja na Cheti, Mshindi wa Tatu: Shilingi milioni 5 na Cheti. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo hiyo, Prof. Penina Oniviel Mlama, amesema Kamati imetoa taarifa hiyo leo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya hafla ya kilele cha utoaji wa tuzo hizo. Aidha, Prof Mlama ameishukuru jamii ya wanahabari kwa mchango wao mkubwa katika kuitangaza Tuzo hiyo tangu ilipoanzishwa katika mwaka wa fedha 2022/23. "Kamati ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu leo imetangaza zawadi ...