Posts

SHIMIWI NI MAHALA PA KAZI – Bi ZIANA MLAWA

Image
Asema Wizara ya Nishati ipambane irudi na ushindi Asema Wizara ya Nishati iwe mfano kwa Wizara zingine Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Nishati, Bi. Ziana Mlawa leo amesema kushiriki michezo mbali mbali inasaidia katika kujenga afya ya mwili na akili hivyo mtumishi anapopata nafasi ya kushiriki michezo yeyote aitumie ipasavyo pia husaidia hali itakayowajengea uwezo kujiamini zaidi ikiwemo katika maeneo ya kazi. Bi. Mlawa ameyasema hayo alipokuwa akiwaaga watumishi wa Wizara ya Nishati watakao shiriki michezo ya SHIMIWI itakayofanyika jijini Mwanza kwanzia tarehe 1 Septemba 2025 " Pamoja na kushiriki michezo ambapo ni mbali na eneo la kazi mkumbuke mkiwa huko ni eneo la kazi nidhamu na uadilifu uwe kipau mbele mdaa wote muwapo kwenye michezo  hiyo." Amesisitiza Bi. Mlawa Ameongeza kuwa watumishi hao wajitahidi wapate ushindi ambapo kwa ushindi huo Wizara itapata heshima njee na ndani ya Wizara

WAZIRI MKUU: RAIS SAMIA AMEIHESHIMISHA TANZANIA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Image
Aipongeza REA Kwa Kusimamia vyema utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi na Usambazaji umeme Vijijini Awasisitiza Watanzania kushiriki Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia Ataja faida za kutumia Nishati Safi ya Kupikia Asema Serikali itaendelea kuwezesha wadau wa Nishati Safi ya Kupikia Atoa wito kwa Sekta Binafsi kushiriki kikamilifu kwenye Kampeni ya Nishati Safi Kilimanjaro Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ameeleza kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameipa heshima nchi kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia inayopewa kipaumbele katika mataifa mengi duniani. Amebainisha hayo Mkoani Kilimanjaro leo Agosti 30, 2025 alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya Uzinduzi wa Mpango wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa Jeshi la Magereza iliyofanyika katika Gereza la Karanga na kuhusisha taasisi na wadau mbalimbali wa Nishati Safi ya Kupikia. Amesema Rai...

HIFADHI YA MPANGA-KIPENGERE YAKONGA NYOYO ZA WALIMBWENDE MISS UNIVERSE 2025

Image
Rais Samia Apongezwa uboreshaji Miundombinu Na Beatus Maganja, Mbeya Walimbwende wa Miss Universe Tanzania 2025 wametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutokana na maono yake ya kukuza sekta ya utalii nchini kupitia maboresho ya miundombinu ya Hifadhi ya Mpanga Kipengere jambo linaloifanya Hifadhi hiyo kuwa kivutio kikubwa cha watalii nyanda za juu kusini. Kauli hiyo imetolewa Agosti 29, 2025 na walimbwende hao mara baada ya  kufanya ziara maalum katika hifadhi hiyo iliyopo Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya ambayo inasimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA ambapo walibaini fursa kubwa ya kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia urithi wa asili wa eneo hilo. "Tumeona historia ya Chifu Mkwawa, maji ya baraka na maajabu ya asili ya kipekee. Mpanga-Kipengere ni hazina ya Taifa letu. Sasa ni jukumu letu kama mabalozi kuutangaza urithi huu Kwa dunia nzima " alisema Nais Sayona ambaye ni mshindi wa Miss Universe Tanz...

DKT.BITEKO AZINDUA MRADI UTAKAOWAKWAMUA VIJANA KIUCHUMI KATIKA MAENEO YANAYOPITIWA NA BOMBA LA MAFUTA GHAFI (EACOP)

Image
Unahusisha kuongezea vijana ujuzi, kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha, na kuondoa vikwazo vya ujasiriamali na ajira binafsi Ataka ujuzi unaotolewa kwa vijana uende sambamba na utoaji wa mitaji Awaasa Vijana kuchangamkia fursa na kuwa waaminifu wanapopata nafasi  Wanawake 6,130, Wanaume 4,905 na Makundi maalum 1,226 kufikiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko leo amezindua  Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE) ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) ikiwa ni jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali katika kuhakikisha kuwa jamii zilizo karibu na miradi zinanufaika na miradi hiyo. Akizindua mradi huo katika  Kijiji cha Bukombe, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita tarehe 18 Agosti 2025, Dkt. Biteko amesema mradi huo wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi ni moja ya miradi iliyopangwa kuwezeshwa na Kampuni ya EACOP kwa kipindi cha ujenzi na baada ya ujenzi ikiwa ni sehemu ya Uwajibikaj...

KANIKI ACHUKUA FOMU

Image
Picha mbalimbali za matukio wakati Mgombea udiwani Kata ya Zingiziwa Selemani kaniki akielekea kuchukua fomu Mgombea udiwani wa Chama cha Mapinduzi CCM Kata ya  Zingiziwa Wilayani Ilala Selemani Kaniki leo Agosti 18/2025 amechukua fomu ya kugombea Udiwani wa kata ya Zingiziwa ambapo Pichani alisindikizwa na viongozi wa chama wa kata hiyo pamoja na viongozi wa kata 

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA, WAPEWA SOMO NA JAJI MUTUNGI

Image
  Na Mwandishi wetu Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, amevitaka vyama vya siasa nchini kujiepusha na lugha za matusi, kashfa, uchochezi au vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga amani na utulivu wa taifa la Tanzania hasa kuelekea uchaguzi Mkuu. Wito huo ameutoa jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi kwa viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa ambapo amesisitiza kuwa vyama vya siasa vina wajibu wa kuendeleza misingi ya amani na mshikamano wa taifa. Amesema kuwa, viongozi wa vyama vya siasa nchini ni vyema kuhakikisha kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 zinafanyika kwa kistaarabu, bila kutumia lugha za matusi, kashfa au vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha tunu ya amani Taifa iliyopo. "Nendeni mkafanye kampeni za kistaarabu mkiwanadi wagombea wenu, kuweni na lugha nzuri za kuzungumza, epukeni matusi, lugha za kashfa, kwani amani ya taifa hili ni muhimu kuliko chochote"mesema Jaji Mutungi. Ameongeza kuwa, amani na mshika...