UJENZI KITUO CHA KUPOZA UMEME NKANGAMO-MOMBA KUKAMILIKA MEI 2026
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema ujenzi wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Nkangamo- Momba unatarajiwa kukamilika Mei mwakani.
Kapinga ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Momba, Condester Sichalwe (CCM) ambaye aliuliza ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha kusambaza umeme Nkangamo – Momba.
Kapinga amesema ujenzi wa kituo hicho cha Nkangamo - Momba ulianza mwezi Mei, 2024 ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 30.
Comments
Post a Comment