Posts

Showing posts from November, 2024

MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA YATANGAZA MVUA KUBWA MIKOA 11 KUANZIA NOV 30, 2024,YATOA TAHADHARI

Image
  Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetabiri mvua kubwa kwa siku mbili kuanzia leo Novemba 30 na Desemba mosi, mikoa 11 kwenye kanda tatu tofauti. Utabiri huo, mbali na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini (Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe na Rukwa), umegusa ukanda wa Pwani ya Kusini mwa Bahari ya Hindi (Lindi na Mtwara), Kanda ya Kati (Dodoma na Singida) na Kanda ya Kusini mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Morogoro. “Angalizo la mvua kubwa kwa maeneo machache ya Nyanda za juu Kusini Magharibi mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe, Rukwa na Songwe, Ukanda wa Pwani ya Kusini mwa bahari ya Hindi mikoa ya Lindi na Mtwara, Kanda ya Kati mikoa ya Dodoma na Singida na Kanda ya Kusini (mkoa wa Ruvuma) na mkoa wa Morogoro,” imesema taarifa ya TMA.

DKT NDUGULILE AFARIKI DUNIA

Image
      Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Kigamboni, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile kilichotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 27 Novemba, 2024 chini India alipokuwa akipatiwa matibabu.  "Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulle. Kwa niaba ya Wabunge natoa pole kwa familia, wakazi wa Kigamboni na Watanzania wote. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi", amesema Spika.  Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia inaendelea kuratibu shughuli za mazishi na taarifa zaidi zitaendelela kutolewa.  BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, APUMZIKE KWA AMANI.

KAPINGA ATUMIA FAINALI YA MPIRA WA MIGUU KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Image
Mbunge wa Vijana Mkoa wa Ruvuma (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga ameendelea na kazi ya kuhamasisha Wananchi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Ruvuma ili waweze kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.  Akiwa mgeni rasmi katika Fainali ya Mpira wa Miguu Mashindano ya Mkuu Super Cup katika Kata ya Matiri wilayani Mbinga, Kapinga amehamasisha makundi mbalimbali ya wananchi kushiriki katika uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa utakaofanyika nchi nzima. " Ndugu zangu, wote tunafahamu kazi kubwa iliyopo mbele yetu ya kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi makini watakaokuwa wasimamizi wa shughuli za maendeleo katika maeneo yetu, kama ambavyo mmejitokeza kwa wingi katika fainali hii,  nguvu hii pia tuielekeze tarehe 27 Novemba 2024, siku ya kupiga kura." Amesisitiza Kapinga Kapinga ameendelea kuwakumbusha  wananchi  kuchagua Viongozi imara, makini na wenye uchungu na maendeleo katika m...

MAKUYUNI WILDLIFE PARK KUFUNGUA NJIA YA MAFANIKIO YA WATALII

Image
Bodi ya TAWA yaridhishwa na uboreshaji wa miundombinu ya utalii Na Beatus Maganja, Arusha.  MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imeanza rasmi utekelezaji wa mikakati ya kuiendeleza na kuiandaa  Hifadhi ya Makuyuni Wildlife Park iliyopo Mkoani Arusha Kwa ajili ya kupokea wageni wengi zaidi kwa kuongeza mindombinu ya utalii hususani barabara, ujenzi wa mabwawa ya maji Kwa ajili ya wanyamapori na kuondoa mimea vamizi ndani ya eneo hilo. Hayo yamesemwa na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA Dkt. Simon Mduma katika ziara ya wajumbe wa Bodi hiyo ya kukagua ujenzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na TAWA ndani ya Hifadhi ya Makuyuni Wildlife Park. "Hifadhi hii ni mpya ilikabidhiwa takribani mwaka mmoja uliopita na katika mchakato wakuiendeleza na kuiandaa Kwa ajili ya kupokea wageni kulikuwa na umuhimu wa kuongeza barabara kwenye maeneo haya ili wageni watakaokuwa wanatembelea eneo hili wawe na wigo mpana wa kuiona mandhari nzuri sana ya eneo hili lak...

NLD KUTIKISA UBUNGO LEO, KAMPENI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Image
Leo tarehe 25 Novemba, saa 10 jioni, viwanja vya Kwakomba, Mtaa wa King'ongo, Ubungo, Jijini Dar es Salaam, Chama cha NLD kitakuwa na mkutano mkubwa wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mtaa. Viongozi wa NLD wilaya ya Ubungo wanachukua fursa hiyo kuwakaribisha wananchi wote wa wilaya ya Ubungo kwenye mkutano huo wa kumnadi mgombea wa Chama cha NLD Mtaa wa King'ongo, Mhe. Patriki Hilaly Ngayungwa. Pia mkutano huo utaudhuriwa na viongozi wa NLD kutoka makao makuu, kwa lengo la kuunga mkono na kutoa sapoti kwa mgombea wa Chama hicho. Chama cha NLD kinaendelea na mikutano mbalimbali ya kampeni nchi nzima, huku viongozi wake wakisisitiza kusimamisha wagombea wenye ushawishi katika kila mtaa, kijiji, na kitongoji. Uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji, na vitongoji unatarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024, nchi nzima.

NAIBU SPIKA MGENI ASISITIZA UJENZI WA UJENZI WA VIWANDA VYA UONGEZAJI THAMANI MADINI NCHINI

Image
Aishukuru GST kwa kufanya utafiti wa madini na kuandaa Ramani ya Jiolojia Zanzibar Awakaribisha Wawekezaji Kuwekeza Katika Sekta ya Madini Zanzibar Waziri Mavunde asema Wizara itaandaa eneo maalum la kudumu la kufanyia Mikutano ya Madini Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mgeni Hassan Juma, amesema kuwa kama ili kufikia azma ya kuwa kitovu cha madini barani Afrika ni lazima kujenga viwanda vitakavyoongeza thamani ya malighafi na kuzalisha bidhaa za mwisho tayari kwa soko la ndani na nje ikiwemo masoko makubwa duniani.  Amesema hayo, leo Novemba 21, 2024, wakati akifunga Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini 2024 uliofanyika kwa siku tatu (Novemba 19-21, 2024) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam,  Mhe. Mgeni ameeleza kuwa mijadala iliyofanyika kupitia Mkutano huo imejikita katika kutafuta suluhisho la changamoto zinazoikabili Sekta ya Madini, hususan katika nyanja za mitaji na teknolojia ya ...

WAZIRI MAVUNDE AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI WA MADINI KUTOKA FINLAND KUWEKEZA NCHINI TANZANIA

Image
▪️Ampongeza Rais Samia kwa kuboresha mazingira ya Biashara nchini ▪️Wavutiwa na uwepo wa Rasilimali madini za kutosha ▪️Finland yaiahidi Tanzania ushirikiano kwenye utafiti wa madini Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde amewakaribisha jumuiya ya wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Finland kuwekeza kwenye sekta ya madini kwa kuwa nchi ya Tanzania imejaaliwa kuwa na rasilimali ya kutosha ya madini,mazingira ya uwekezaji rafiki na sera zinazotabirika. Waziri Mavunde ameyasema hayo jana  Masaki Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa kifungua kinywa ulioandaliwa na Ubalozi wa Finland nchini kwa lengo la kuwakutanisha wafanyabiashara wa Madini kutoka Finland na Wizara ya Madini ili kubaini maeneo ya ushirikiano na fursa za kiuchumi zilizopo sekta ya madini nchini Tanzania. Akizungumza katika hafla hiyo Balozi wa Finland nchini Tanzania Mh. Theresa Zitting amesema Tanzania na Finland ni nchi zenye ushirikiano mkubwa kwenye masuala ya kiuchumi na hivyo ni wakatinmuafaka sasa kuimarisha mah...

KUANZIA JANUARI 2025, VIVUKO VITAKUWA VINASUBIRIA ABIRIA, SEA TAX KUONGEZWA DAR: BASHUNGWA

Image
Na Mwandishi wetu, Dar  Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) kwa kushirikiana Kampuni ya Azam Marine zinaendelea kuboresha utoaji wa huduma za usafiri wa vivuko katika eneo la Magogoni – Kigamboni jijini Dar es Salaam ambapo kufikia mwezi Januari 2025 vitaongezwa vivuko vidogo (sea tax) kufikia sita (6) ambapo ushirikiano huo utaondoa changamoto kwa wananchi kusubiri vivuko kwa muda mrefu.  Bashungwa ameeleza hayo leo Novemba 19, 2024 Dar es salaam wakati akikagua huduma za usafiri wa vivuko ambapo ameeleza kutokana na changamoto iliyopo sasa, kuanzia kesho (Novemba 20,2024) Azam Marine kwa kutumia sea tax itaongeza muda wa kutoa huduma kulingana na ilivyokuwa awali ili kupunguza msongamano wakati wa asubuhi na jioni.  “Nimeelekeza  kufika Disemba 31, 2024 majengo ya kisasa ya abiria yawe yamekamilika na tuingie mwaka mpya wa 2025 tukiwa na Sea tax za Azam sita, hilo lina maanisha kuanzia Januari 01, 2...

WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA MKUTANO WA KIMATAIFA WA MADINI NA UWEKEZAJI 2024.

Image
  Picha mbalimbali za matukio katika Mkutano wa kimataifa wa madini na uwekezaji Tanzania Na Mwandishi wetu  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Novemba 19, 2024 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa Kimataifa wa Madini na Uwekezaji Tanzania, kwenye kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo unawakutanisha wadau wa madini wanaojishughulisha na utafutaji, uchimbaji, uchenjuaji, uongezaji thamani madini, wasimamizi wa Sekta kutoka Serikalini, watoa huduma migodini na wafanyabiashara. Pamoja na malengo mengine, mkutano huo umelenga kuweka mipango ya kuvutia uwekezaji  wa nje ya nchi, kukuza usimamizi bora wa rasilimali za Madini pamoja na kubadilishana uzoefu na washiriki kutoka maeneo mbalimbali duniani. Kaulimbiu ya mkutano huo ni _Uongezaji wa Thamani ya Madini kwa Maendeleo ya Kiuchumi_

SERIKALI YAONGEZEKA MASAA 24 YA UOKAJI WALIOANGUKIWA NA GHOROFA KARIAKOO

Image
  Na Mwandishi wetu  Mkurugenzi wa Idara ya Habari-Maelezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Thobias Makoba, amesema zoezi la uokoaji wa watu walionasa kwenye jengo lililoporomoka Jumamosi ya Novemba 16, 2024 Kariakoo kwenye Mtaa wa Congo na Mchikichi Jijini Dasr es Salaam, litaendelea tena kwa saa 24 za ziada baada ya saa 72 za kawaida za kiwango cha kimataifa kumalizika. Bw. Makoba ameyasema hayo leo novemba 19, 2024, wakati akizungumza na waandishi wa habari Kariakoo kwenye eneo la tukio, ambapo amesema kuongezeka kwa saa hizo 24 za ziada, ni agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, alilolitoa kupitia kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa, katika kikao cha tathmini kuhusu zoezi hilo la uokoaji ambapo amelitaka jeshi la zimamoto na uokoaji, kuendelea na shughuli hiyo ili kunusuru uhai wa watu ambao bado wamekwama kwenye jengo hilo. “Tukiwa kwenye kikao cha tathmini cha kazi inayoendelea, moja ya ajenda iliyozungumzwa ni k...

WAZIRI SILAA AWEKA BAYANA MAKAKATI YA KUWEZESHA IDARA YAKE YA HABARI , MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA KUPITIA USHIRIKIANO NA WANAHABARI

Image
  Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa, ameweka wazi mikakati yake ya kuboresha sekta ya habari kupitia ushirikiano wa karibu na wanahabari.  Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika mkutano wa wadau wa sekta ya habari kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2025, Waziri Silaa amesema amejipanga kuhakikisha sekta ya habari inaimarika kwa kufanya marekebisho ya sera na sheria ili kuendana na mahitaji ya kisasa. Waziri ameeleza kuwa sekta ya habari ni mhimili muhimu katika maendeleo ya kiuchumi, kijamii, na kiusalama, huku pia ikiwa nguzo ya utawala bora. Amesema serikali inatambua mchango wa vyombo vya habari katika kusimamia uwazi na uwajibikaji, na kwa sasa kuna vyombo 1,023 vya habari ambavyo vinatoa mchango mkubwa kwa taifa. Akiwa na dhamira ya kuboresha sekta hiyo, Waziri Silaa amesema atatembelea wadau wote wa habari, akianza na makundi, na hatimaye vyombo vya habari binafsi, ili kujadiliana na kubadilishana mawazo. Pia ...

KASI YA MAENDELEO DAR ES SALAAM INACHANGIA ONGEZEKO LA MAHITAJI YA UMEME- MHE. KAPINGA

Image
Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga  amesema ukuaji wa kasi wa maendeleo na uchumi katika Mkoa wa Dar es Salaam unachangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa ongezeko la mahitaji ya umeme. Ameyasema hayo leo 18 Novemba, 2024  wakati wa ziara yake kwenye Kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi jijini Dar es Salaam iliyolenga  kukagua maendeleo ya maboresho ya miundombinu ya umeme katika kituo hicho ili  kukiongezea uwezo.  Kituo  hicho kinachohudumia wakazi wa Gongo la Mboto, Mbagala, Kigamboni na Dege kinafungwa Transfoma yenye uwezo wa jumla ya 400 MVA  huku Transfoma za ukubwa wa 175 MVA zikiwa zimeshafungwa. ‘’Nipende kuwatoa hofu wakazi wa Dar es Salaam na Pwani hususani Gongo la Mboto, Dege na Mkuranga kuwa TANESCO imekamilisha maboresho iliyokuwa ikifanya siku tatu zilizopita  na tayari transfoma zimefungwa na hivyo kupunguza mzigo kwenye vituo vya Mbagala Ubungo na Dege na Gongo la Mboto‘’. Amesema Mhe. Kapinga Ameeleza kuwa, kwa sasa kas...