RAIS DKT SAMIA KESHO KUTUA KOREA, MIKATABA SABA KUSAINIWA

 

Na Mwandishi wetu, HabariPlus

Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kesho anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku sita nchini korea yenye lengo la kukuza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. anaenda kufanya  Ziara ya kikazi. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje January Makamba amesema kuwa pamoja na mambo mengine pia atasaini mikataba saba na Rais wa nchi ya korea yenye lengo la ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

"Miongoni mwa mikataba  hiyo ni pamoja na mikataba  hati ya makubaliano kati ya Taasisi ya madini Tanzania na Taasisi ya miamba nchini korea, huu ni ushirikiano unahusu utafiti, uchoraji ramani, rasilimali na uchoraji  wa maabara"amesema Waziri Makamba.

Ameongeza"mkataba wa pili ambao unaenda kusainiwa ni ushirikiano wa uchumi wa bluu, huku mkataba wa tatu ukihusu kwenda kutambua vyeti vya mabaharia  na tutaweza kusaini tamko la pamoja kuhusu siasa  na makubaliano ya hati ya madini, viwanda na biashara  "amesema Waziri makamba

Hata hivyo, mkataba mwingine ni msaada wa fedha kutoka benki ya Exim nchini korea  na Serikali ya  Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambao unaenda kupelekea Tanzania  kupata msaada na mikopo nafuu, pia wanakwenda kushirikiana na chuo kikuu kutoka nchini korea katika kuendeleza huduma za usafiri wa anga nchini.

Aidha, amesema ziara hiyo imedhamiria  kuendeleza  ushirikiano  baina ya Serikali ya Tanzania na Korea kwenye mambo muhimu ikiwemo elimu, afya, na miundombinu hivyo ziara hiyo inaenda kuleta mafanikio mbalimbali nchini Tanzania.

Aidha  Waziri  Makamba ameongeza kuwa kuhusu madini kwenye mkakati watasaini  mkataba katika kuwezesha  kuchambua, na kufanya mkakati na shirika la madini Tanzania  STAMICO na shirika la ukarabati  wa madini nchini Korea.

Comments

Popular posts from this blog

TMA YATOA TAHADHARI KUHUSU UWEPO WA KIMBUNGA "HIDAYA"

HUU HAPA MWENENDO WA KIMBUNGA "HIDAYA" , UPEPO KUVUMA KWA KASI YA KILOMITA 130 KWA SAA

NHIF YAFANYA MABORESHO YA KITITA CHA HUDUMA ZA MATIBABU, YAENDELEA KUPOKEA MAONI