Posts

Showing posts from May, 2025

WAKILI MADELEKA AJITOSA JIMBO LA KIVULE

Image
Wakili Peter Madeleka leo amechukua fomu ya kugombea Ubunge  Jimbo la Kivule kupitia tiketi ya Chama cha Act Wazalendo . Mapema leo amefika katika katika Ofisi za Chama cha Act Wazalendo zilizopo Jimbo la Kivule Kata ya Kitunda, akiwa na wafuasi wa Chama hicho kuchukua fomu hiyo na kuomba ridhaa ya Chama hicho kumpitisha kugombea Jimbo hilo.  Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kuchukua fomu hiyo amesema ameamua kugombea Jimbo hilo ili kuweza kuwasaidia wananchi kutokana na changamoto nyingi za kijamii zinazowakabili Jimbo humo. "Jimbo hili ni jipya lakini hakuna maendeleo yoyote yaliyoletwa, barabara ni mbovu hazipitiki mvua zikinyesha mawasiliano yanakua shida, limesahaulika kwa muda mrefu sasa nimekuja mkombozi wao"amesema Wakili Madeleka Amesema kuwa, miongoni mwa ajenda zake atazokwenda nazo endapo chama kitampaa ridhaa ya kugombea katika Jimbo hilo ni kusimamia haki na kuhakikisha anaweka misingi mizuri ya watu kuishi bila maumivu. ...

TANZANIA NA JAPANI ZATILIANA SAINI YA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO WA MPANGO WA PAMOJA

Image
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Japan zimetia saini Hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika mpango wa pamoja wa uwekezaji katika Biashara ya Kaboni utakaowezesha kampuni za nchi hizo mbili kuwekeza katika Biashara ya Kaboni nchini Tanzania. Utiaji saini wa makubaliano hayo umefanyika Mei 28, 2025  Tokyo, Japan kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni na Serikali ya Japan ikiongozwa na Waziri wa Mazingira, Mhe. Asao Keiichiro (Kei). Akizungumza mara baada ya utiaji saini huo, Waziri Masauni amesema Makubaliano ya Mashirikiano yaliyosainiwa yamekusudiwa kuimarisha uhusiano kati ya Japan na Tanzania kwa maendeleo endelevu na hatua za kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi. Amesema mashirikano haya yataongeza  fursa ya kupanua soko la Biashara ya Kaboni kutoka kwa wawekezaji wa Japan watakaowekeza katika miradi ya biashara ya Kabo...

RC CHALAMILA ATOA WIKI MBILI WAMACHINGA KUFUNGUA NJIA

Image
Na Mwandishi wetu  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ametoa agizo kwa wafanyabiashara wadogo (machinga) waliopo katika eneo la Kariakoo kuhakikisha wanafungua njia ndani ya kipindi cha wiki mbili kuanzia Mei 28, 2025, ili kuruhusu shughuli za kibiashara kufanyika kwa ufanisi kuelekea uzinduzi wa soko la Kariakoo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, RC Chalamila amesema soko hilo limekamilika kwa asilimia 98, hivyo ni muhimu njia za kuingilia kwenye soko ziwe wazi ili kurahisisha uingizaji wa bidhaa. Amesisitiza kuwa, Serikali itawaondoa machinga waliopo kwenye njia na kuwapeleka kwenye maeneo maalum yaliyotengwa, kama ilivyoelekezwa na Wizara ya TAMISEMI. Aidha, RC Chalamila ameeleza kuwa wafanyabiashara waliokuwa wakifanya shughuli zao kwenye soko la awali kabla ya kuungua, watarudishwa kwenye maeneo yao baada ya uhakiki, kwa mujibu wa agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Amesisitiza kuwa watahitajika kujaza mikataba, kujiandaa kulipa kodi, n...

WIZARA YA NISHATI YASHIRIKI WIKI YA NISHATI JADIDIFU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
  Wizara ya Nishati imeshiriki Wiki ya Nishati Jadidifu 2025 inayoendelea jijini Dar es Salaam. Katika picha ni Wadau na Wageni mbalimbali walipotembelea Banda la Wizara na kupata elimu juu ya masuala mbalimbali ikiwemo umeme na Nishati Jadidifu.  Wiki ya Nishati Jadidifu inafanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC). "Picha mbalimbali za matukio" Mkuu wa Sekta ya Nishati kutoka Umoja wa Ulaya (EU),  Maximilliano Pedretti akitembelea mabanda mbalimbali ya maonesho  katika Wiki ya Nishati Jadidifu 2025 inayoendelea jijini Dar es Salaam. Pamoja naye ni Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga,pamoja na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia Bw. Nolasco Mlai kutoka Wizara ya Nishati. 

MAKAMU WA RAIS AFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI MBALIMBALI IVORY COAST

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya  mazungumzo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) anayemaliza muda wake Dkt. Akinumwi Adesina kando ya Mkutano wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) unaofanyika katika Hoteli ya Sofitel Ivoire Jijini Abidjan nchini Ivory Coast.

MAPATO YA KIKODI CHANZO CHA MAENDELEO - DKT MPANGO

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema maendeleo ya Tanzania katika uendelezaji miundombinu ni kutokana na ufanisi katika mapato ya kikodi,  ushiriki wa sekta binafsi pamoja na uimarishaji wa masoko ya mitaji na dhamana inayotumika katika kufadhili miradi hiyo. Makamu wa Rais amesema hayo wakati aliposhiriki majadiliano ya Viongozi wa Juu kuhusu “Umuhimu wa kutumia Rasilimali za Bara la Afrika kwa ufanisi ili kuchochea Maendeleo” yaliyofanyika wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) unaofanyika katika Hoteli ya Sofitel Ivoire Jijini Abidjan nchini Ivory Coast. Amesema kutokana na umuhimu wa miundombinu katika mageuzi ya kiuchumi nchini Tanzania, Serikali ilihitaji kufanya kazi zaidi katika kukusanya fedha ya uendelezaji wa miundombinu ikiwemo Reli ya kisasa (SGR) pamoja na barabara kuu ambazo zitaunganisha mataifa mbalimbali na kuwezesha ufanyaji biashara. Makamu wa Rais ametaja juh...

KAFULILA AELEZA HOJA NZITO KUHUSU PPPC, KONGAMANO LAFANA

Image
Na Mwandishi wetu  Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), David Kafulila amesema deni la dunia limekuwa likiongezeka ila deni la Taifa la Tanzania limebaki kuwa himilivu. Aidha, Kupitia ( Public -Private Partnership ) PPP, Serikali inapunguza mzigo wa kifedha na kiutendaji huku ikihakikisha Miradi ya Maendeleo inakamilika kwa wakati. Hayo ameyabainisha leo jijini Dar es Salaam wakati akiwasilisha mada katika Kongamano la kitaifa kuhusu ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi lenye mada kuu dola, masoko na uhamasishaji mitaji, nafasi ya Ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi kufikia malengo ya dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050. Amesema kuwa,ongezeko la mahitaji ya rasilimali za kugharamia bajeti ya Serikali yamefanya dhana ya Ubia kati Sekta binafsi (PPPC) kugharamia miradi ya maendeleo kuwa na umuhimu wa kipekee nchini Tanzania. Kafulila aliwasilisha mada inayosema nafasi ya PPP katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maend...

WAZIRI MASAUNI ATOA ONYO UZALISHAJI NA MATUMIZI BIDHAA ZA PLASTIKI

Image
  Serikali imetoa onyo kali kwa watu na kampuni zinazoendelea kuzalisha bidhaa za mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku na kuingiza katika matumizi kwa njia za panya. Imesema itaendelea kufanya doria za kushtukiza katika viwanda, viwanda bubu na masoko ili kuwabaini na kuwachukulia hatua wahusika wote wanaojihusisha na biashara hiyo. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema hayo leo Mei 27, 2025 jijini Dodoma wakati akitoa tamko la Serikali kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kilele chake kitakuwa jijini Dodoma na mgeni rasmi anatarajia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hatua hiyo inakuja kutokana na kujitokeza kwa changamoto ya matumizi ya vifungashio vya plastiki aina ya tubings kutumika kama vibebeo na vifungashio ambavyo havina sifa na kutokukidhi matakwa yaliyowekwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Kufuatia hatua, Mhandisi Masauni amelielekeza B...

REDET, PPPC KUFANYA KONGAMANO

Image
  Na Mwandishi wetu Dar  Kituo cha Ubia kati Sekta Binafsi na Sekta ya Umma (PPPC) kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa masuala Demokrasia (REDET) chini ya Chuo Kikuu Cha Dar es salaam  wameandaa kongamano kwa ajili ya kujadili nafasi ya sekta binafsi na sekta ya umma kuelekea dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 . Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo,  Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia (PPPC) David Kafulila, amesema moja ya majukumu ya PPPC ni kuiwezesha jamii kupata uelewa  juu ya masuala ya kisera na kisheria na mipango ya Serikali katika maeneo ya ubia  Aidha, amesema kongamano hilo ambalo litakuwa la wazi linatarajia kufanyika Mei 27,2025 katika ukumbi wa Maktaba katika Chuo Kikuu Cha Dar es salaam ambapo limelenga kuwashirikisha wadau mbalimbali ambapo mada mbalimbali zitajadiliwa. "PPPC iliona ipo  haja ya kushirikiana na Taasisi ya REDET ambayo imebobea katika uendeshaji wa makongamano kwa lengo la  kuushirikisha umma zaidi, T...

MITAA 58 HALMASHAURI YA MJI WA TARIME IMEFIKIWA NA UMEME– MHE. KAPINGA

Image
Ni kati ya mitaa 81 ya Halmashauri  ya Mji wa Tarime Asema kazi ya kupeleka umeme vitongojini ni endelevu Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali imefikisha  umeme kwenye mitaa 58 ya Mji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kati ya mitaa 81 ya Halmashauri hiyo. Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 26, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Tarime Mjini, Mhe. Michael Kembaki aliyeuliza Serikali itapeleka lini umeme katika mitaa 18 ya Halmashauri ya Mji wa Tarime.  "Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Tarime ina mitaa 81, kati ya hiyo mitaa 58 tayari  imefikiwa na umeme, na mitaa 23 bado haijafikiwa na umeme."  Amesema  Kapinga Ameongeza kuwa, mitaa 13 inapelekewa umeme kupitia mradi wa Hamlets Electrification Project - IIA (HEP IIA) unaotekelezwa na Mkandarasi Dyname Construction Engineering,  na mitaa 10 iliyobaki itafikishiwa umeme katika miradi inayofuata. Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Wa...

WAZIRI MCHENGERWA AFURAHISHWA NA UONGOZI WA MKOA WA DAR

Image
Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu( TAMISEMI) Dkt, Mohamed Mchengerwa, ameupongeza uongozi wa mkoa wa Dar es Salaam chini ya mkuu wake Albert Chalamila kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kusimamia miradi ya maendeleo na utekelezaji wake . Pongezi hizo alizitoa jijini Dar es Salaam katika kongamano la wamachinga wa Kariakoo la kumpongeza Rais Dkt Samia na kuliombea Taifa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika hivi karibuni. Amesema njia waliochagua wamachinga ndio sahihi ya kuleta maendeleo na kuisaidia Serikali inawaunga mkono ili waweze kuendelea kwani Taifa la Tanzania linaendelea kuwa salama na amani Rais wa JMT amefanya makubwa ikiwemo kuwashika wafanyabishara.  Sambamba na hayo, ametoa maelekezo Wilaya ya Ilala kuhusu ujenzi wa Jangwani Mpya na majengo ya kisasa ya Wamachinga yaweze kuongezwa katika mji wa kisasa majengo ya wafanyabishara wamachinga yawekwe eneo hilo ujenzi ukikamilika waweze kutumia masoko na wao. Akizungumzia masoko ya mkakati yatakayojengwa mikoa yote pia ...

WAZIRI MCHENGERWA AMPA TANO KUMBILAMOTO

Image
Na Mwandishi wetu WAZIRI wa Nchi Ofisi ya waziri mkuu (TAMISEMI) Dkt Mohamed Mchengerwa, amemtabiriwa mambo makubwa Meya wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto, ambaye ni Diwani wa kata ya Vingunguti kwa utendaji bora wa kazi katika kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan. Aidha, Waziri Dkt Mohamed Mchengerwa  amesema hayo wakati wa kuzindua mradi wa Serikali wa ujenzi wa soko la nyama  choma la lililopewa jina la KUMBILAMOTO mradi huo uliopo machinjio ya Vingunguti wilayani Ilala.  "Nawapongeza Madiwani wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam mmepata Meya bora Omary Kumbilamoto, mchapa kazi na anafanya kazi kwa weledi za Serikali anajua kazi yake isingekuwa katiba ya chama cha Mapinduzi Meya Omary Kumbilamoto  anapita bila kupingwa na Jimbo lingegawanywa angepewa jimbo moja  "amessema Dkt Mchengerwa.  Amesema kuwa, kutokana na utendaji kazi wa Meya Kumbilamoto ni vyema madiwani wa Halmashauri ya jiji la ...

WAZIRI MASAUNI AUNGANA NA UJUMBE WA WAZIRI MKUU MAJALIWA NCHINI JAPAN

Image
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais ( Rais Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Masauni ameungana na ujumbe wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa uliopo nchini Japan Kushiriki maonesho ya Dunia ya EXPO 2025 Osaka Japan ambapo leo Mei 25,2025 ni Siku ya Taifa la Tanzania(Tanzania National Day)

SULUHU MGAWANYO WA MAPATO WA HUDUMA ZA USAFIRI WA ANGA NCHINI YAPATIKANA

Image
  Dar es Salaam Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) pamoja na Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) wafanikisha upatikanaji wa suluhu ya mgawanyo wa mapato yatokanayo na huduma za usafiri wa anga nchini. Suluhu hiyo imepatikana kupitia kusainiwa kwa mkataba wa makubaliano ya pamoja baina ya wakuu wa taasis hizo katika ukumbi wa mikutano wa TAA uliopo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, tarehe 23 Mei 2025. Mkataba huo unafuatia kuundwa kwa mfumo wa kielektroniki (Ankara Jumuishi) utakaosaidia kuimarisha uwazi, ufanisi na tija katika mgawanyo wa mapato yatakayokuwa yamekusanywa kwa kuingizwa moja kwa moja kwenye taasis husika kulingana na asilimia zilizokubalika. Mfumo unatarajiwa kuanza kutumika kuanzia tarehe 1 Julai 2025. Wakizungumza katika zoezi la utiaji saini, Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Abdul Mombokaleo alieleza kuwa mfumo huo wa kielektroniki utarahisisha mgawanyo wa mapato na ku...