Posts

Showing posts from October, 2025

MRADI WA TAZA KUFUNGUA SOKO JIPYA LA BIASHARA YA UMEME AFRIKA

Image
Wafikia asilimia 83 Dkt. Mataragio akagua mradi na kutoa maelekezo TANESCO TAZA kuunganisha Mkoa wa Rukwa na gridi ya Taifa Kuimarisha upatikanaji umeme Mikoa ya Kusini mwa Tanzania Mbeya Imeelezwa kuwa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Zambia kupitia Tunduma (TAZA) umefikia asilimia 83.45 huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Mei 2026 na hivyo  kufungua soko jipya la biashara ya umeme barani Afrika. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo leo Oktoba 23, 2025 katika eneo la Iganjo, Mbeya, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amesema mradi wa TAZA ni muhimu kwa Taifa kwa kuwa utaiunganisha Tanzania na Nchi za ukanda wa Kusini mwa Afrika (Southern Africa Power Pool) na pia kuimarisha muunganiko wa ukanda wa Mashariki mwa Afrika (East Africa Power Pool). “Nimshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya nishati. K...

DKT. MATARAGIO AAGIZA VIFAA VYOTE VYA UHAKIKI WA JOTOARDHI ZIWA NGOZI KUFIKA KWA WAKATI

Image
Ni baada ya kukagua mradi na kukuta baadhi ya vifaa bado havijafika Asisitiza mradi kukamilika kwa wakati ikiwa ni  utekelezaji wa Sera ya Nishati ya mwaka 2015 Kazi ya uhakiki wa Jotoardhi Ziwa Ngozi yafikia asilimia 60 Mbeya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Kampuni yake Tanzu ya Uendelezaji Jotoardhi (TGDC)  kuhakikisha kuwa vifaa vyote vya uhakiki wa rasilimali Jotoardhi  katika mradi wa Ziwa Ngozi  vinafika kwa wakati ili kazi za uhakiki  ziweze kumalizika kulingana na muda uliopangwa. Dkt. Mataragio ametoa maagizo hayo leo Oktoba 22, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua kazi zinazoendelea kutekelezwa katika mradi huo wilayani Rungwe mkoani Mbeya. “Huu mradi mnapaswa kuukamilisha kwa wakati kutokana na umuhimu wake nchini, tunapotekeleza miradi hii ya Jotoardhi tukumbuke kuwa tunatekeleza pia Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015 ambayo inasema Tanzania inapaswa izalishe umeme kwa ku...

TAMASHA LA NYAMAPORI CHOMA LAVUTA UMATI TABORA ZOO

Image
Zaidi ya watalii 500 wafurika kuonja ladha ya nyama pori na burudani za uhifadhi Na Mwandishi Wetu, TABORA Zaidi ya watalii 500 wamefurika leo, Oktoba 18, 2025, katika Bustani ya Wanyamapori Tabora (Tabora Zoo) kushiriki katika Tamasha la Nyamapori Choma lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Kanda ya Magharibi. Tamasha hilo lililolenga kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na matumizi endelevu na halali ya rasilimali za wanyamapori, limevutia watalii  kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi, likihudhuriwa na viongozi wa Serikali wakiwemo Wakuu wa Wilaya za Tabora na Uyui, wananchi wa Mkoa wa Tabora na mikoa jirani, pamoja na wageni kutoka mataifa mbalimbali duniani. Wananchi waliohudhuria tamasha hilo wameipongeza TAWA kwa ubunifu wa kuandaa tukio hilo, wakieleza kuwa limewapa fursa ya “kuonja ladha ya matunda ya uhifadhi” unaotekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali hizo Kwa nj...

DOYO: AMANI NI NGUZO KUU YA MAENDELEO NA MAPINDUZI YA UCHUMI TANZANIA

Image
  Dar es Salaam  Mgombea urais kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, na Katibu Mkuu wa chama hicho, amewataka Watanzania kudumisha amani kabla, na baada ya uchaguzi mkuu ujao, akisisitiza kuwa amani ndiyo nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote duniani. Akizungumza jijini Dar es Salaam katika muendelezo wa kampeni za chama hicho zinazofanyika kwa mtindo wa “mobile kampeni”, Doyo alisema chama chake kimefanya kampeni za kistaarabu na kisayansi katika mikoa 26 mpaka sasa. Alisema kampeni hizo zimekuwa zikiwalenga wananchi moja kwa moja ili kuwapa sera na kuelewa changamoto zao bila kutweza utu wa mtu. “Niwaombe sana, Watanzania wenzangu, mkapige kura kwa amani. Mkivunja amani, hakuna maendeleo yatakayopatikana. Amani ndiyo tunu ya taifa letu,” alisema Mhe. Doyo. Doyo alifafanua kuwa amani ni sharti muhimu la maendeleo. Alisema pale ambapo amani ipo, ndipo serikali inaweza kutekeleza kwa ufanisi ahadi zake kwa wananchi, ikiwemo kuboresha hud...

TMA YATOA MWELEKEO WA MVUA ZA MSIMU NOV 2025 HADI APRIL 2026

Image
  Na Mwandishi wetu, Dar Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa mwelekeo wa mvua za msimu wa Novemba 2025 hadi Aprili 2026, ikibainisha kuwa maeneo mengi ya nchi yanatarajiwa kupata mvua za chini ya wastani hadi wastani, hali ambayo inaweza kuathiri shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii, hususan katika sekta za kilimo, mifugo, maji, nishati, afya na usalama wa chakula. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus B. Chang’a, amesema mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba katika mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma, na kusambaa kwenye maeneo ya kusini mwa nchi kufikia Novemba 2025, huku zikitarajiwa kuisha kati ya mwisho wa Aprili na mwanzo wa Mei 2026. Dkt. Chang’a amefafanua kuwa msimu wa mwaka huu utatawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha, ingawa nusu ya pili ya msimu (Februari – Aprili 2026) inaweza kuwa na ongezeko la mvua ikilinganishwa na nusu ya...

WAZIRI MKUU MAJALIWA APONGEZA WIZARA YA NISHATI KWA USIMAMIZI THABITI WA MIRADI

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amepongeza Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa utekelezaji na usimamizi miradi mbalimbali ya nishati nchini. Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo leo jijini Tanga wakati akifunga Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Chakula ya Duniani ambayo leo yamefikia kilele chake. Mhe. Majaliwa amesema kuwa usimamizi mzuri wa miradi ya Nishati umepelekea wananchi kuendelea kupata huduma bora. Katika maadhimisho hayo ya Siku ya Chakula Duniani yaliyoanza tarehe 10 Oktoba 2025 yamepelekea wananchi kupata elimu kuhusu mafanikio ya sekta ya nishati na miradi inayoendelea huku wananchi 500 wakinufaika na mitungi ya gesi iliyokuwa ikiuzwa kwa bei ya Ruzuku ya shilingi 17,500/=. Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amekabidhi tuzo kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikiwa ni kupongeza juhudi za taasisi hiyo kupitia maadhimisho hayo ya Siku ya Chakula Duniani.

REA YANG'ARA MAONESHO YA WIKI YA CHAKULA TANGA

Image
Waziri Mkuu aitunuku REA tuzo ya pongezi kwa uhamasishaji wa matumizi nishati safi Majiko ya gesi 500 yauzwa kwa bei ya ruzuku kwenye maonesho Asisitiza kulinda mazingira na kuacha ukataji wa miti hovyo Tanga Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hapa nchini. Mhe. Majaliwa amebainisha hayo leo terehe 16 Oktoba 2025 alipotembelea banda la REA wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Chakula Duniani 2025 yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya Usagara jijini Tanga. Katika hatua nyingine, Mhe. Majaliwa ameipatia tuzo ya pongezi REA ambapo imeibuka kuwa mshindi wa pili wa banda bora katika kuhudumia wananchi katika maadhimisho ya Wiki ya Chakula yaliyofanyika mkoani humo. Naye, Mhandisi kutoka REA, Ramadhan Mganga amesema Rais Samia ni kinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini na kuwataka wananchi kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Sul...

DALILI ZA UWEPO WA GESI ASILIA KATIKA KITALU CHA LINDI-MTWARA

Image
Utafiti wa kina unaendelea katika Kitalu cha Lindi–Mtwara Dkt. Mataragio akagua maendeleo ya mradi, aagiza ukamilike kwa wakati Akagua pia mradi wa kuongeza uzalishaji wa gesi katika kitalu cha Mnazi Bay RC Mtwara asema Gesi Asilia ni kichocheo cha wawekezaji mkoani Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwanamawa asisitiza faida kwa jamii kupitia ajira na miundombinu Utafiti unaoendelea kufanyika katika Kitalu cha Lindi–Mtwara, kinachojumuisha jumla ya vijiji 48 katika eneo la takriban kilomita za mraba 736 – vijiji 40 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara (Mtwara DC) na vijiji 8 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mtama (Mtama DC) – umeonesha dalili za uwepo wa Gesi Asilia, hususani katika vijiji vya Mnyundo na Mpapura, mkoani Mtwara, ambapo visima vya maji vilibainika kuvujisha gesi asilia. Katika ziara yake ya kukagua miradi ya gesi na mafuta mkoani Mtwara, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio, amesema kuwa utafiti wa awali unaonesha uwezekano mkubwa wa kupatikana kwa gesi a...

KATIBU MKUU NISHATI AHIMIZA UZALENDO NA UADILIFU KWA WANACHAMA WA EWURA CCC

Image
  Azindua Baraza la Tatu la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba, ametoa wito kwa wajumbe wa Baraza jipya la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA Consumer Consultative Council – EWURA CCC) kuwa na nidhamu, uzalendo na uwajibikaji  katika majukumu yao, ili kuongeza ufanisi wa kazii na kuleta manufaa kwa wananchi. Akizungumza jijini Mwanza wakati wa uzinduzi wa Baraza jipya la tatu la EWURA CCC pamoja na mafunzo kwa wajumbe wapya, Mha. Mramba amewahimiza wajumbe hao kufanya kazi kwa ushirikiano na kuweka mbele maslahi ya taifa. “Ni muhimu kila mjumbe kuwa mfano wa uwajibikaji na uadilifu. Baraza hili lina jukumu kubwa la kusikiliza na kuwasemea watumiaji wa huduma za nishati na maji, hivyo nidhamu na uzalendo ni nguzo kuu za mafanikio." Amesema Mhandisi Mramba Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa EWURA CCC, Bi. Stella Lupimo, alisema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wajumbe wapya ili w...

DOYO: AAHIDI RUZUKU MAALUM KWA WATU WENYE ULEMA­VU

Image
  Asema: Serikali Ya NLD Itapunguza Kodi Kwa Wawekezaji Ili Kutoa Mitungi Ya Gesi Bure Kwa Watanzania, Ni Hatua Ya Kuokoa Mazingira. Moshi, Kilimanjaro Akiwa katika ziara yake ya kampeni mkoani Kilimanjaro, Mgombea Urais wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, amewahakikishia Watanzania kwamba serikali atakayoiongoza itakuwa ya usawa, matumaini na maendeleo kwa kila Mtanzania bila ubaguzi, huku lengo lake kuu likiwa ni kuimarisha usawa wa kijamii na kiuchumi. Mhe. Doyo amesema wazi kwamba serikali ya NLD itahakikisha makundi maalum nchini yanapewa nafasi na msaada unaostahili. Watu wenye ulemavu, wasioona, wenye ulemavu wa ngozi, na wale wenye changamoto mbalimbali za kimaumbile hawatasahaulika tena iwapo wananchi watamchagua Oktoba 29. “Serikali yangu itatenga ruzuku maalum kwa watu wenye uhitaji maalum. Tutaanzisha mfumo mahsusi wa kuwasaidia moja kwa moja, bila urasimu, bila foleni, na bila kulazimika kupita kwenye milango ya wizara zisizo na maj...

WIZARA YA NISHATI YATUMIA SIKU YA MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KUTOA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Image
Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zake imeendelea kutumia njia mbalimbali kufikisha elimu ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi ambapo safari hii elimu hiyo inatolewa katika Maadhimisho ya Siku ya Chakula duniani yanayofanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga. Akizindua Maadhimisho hayo leo jijini Tanga, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian ameipongeza Wizara ya Nishati na taasisi zake kwa kushiriki maadhimisho hayo yanayotarajiwa kumalizika Octoba 16 mwaka huu. Dkt. Burian ameeleza kuwa Nishati Safi ya Kupikia ina mchango wa moja kwa moja katika suala la chakula kwani Serikali kwa sasa inahimiza matumizi ya nishati safi katika kupikia chakula.  Aidha, akiwa katika Banda la Wizara ya Nishati, Dkt. Burian alielezwa na Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati, Omari Khalifa kuwa, Wizara ikishirikiana na taasisi zake, inatekeleza ajenda ya Taifa ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo kinara wake ni. Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Khalifa amesema katika maadhimisho hay...

DC WANGING'OMBE AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA GHASIA KWA ASKARI WA TAWA

Image
Aridhishwa na umahiri wa Askari hao Na. Beatus Maganja, Njombe. Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe, Mhe. Zacharia Mwansasu, Oktoba 8, 2025 amefunga  rasmi mafunzo siku 10 ya kukabiliana na ghasia (Anti-Riot) kwa kikosi maalum cha Askari 60 wa mwitikio wa haraka wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA (RRT) katika Kituo cha Mafunzo cha Welela Mkoani Njombe, akisisitiza umuhimu wa nidhamu, weledi na uzingatiaji wa sheria katika utekelezaji wa majukumu ya uhifadhi. Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mhe. Mwansasu alisema "Serikali inatambua changamoto zinazowakabili Askari wa Uhifadhi, ikiwemo hatari wanazokutana nazo katika kulinda rasilimali za taifa, ambapo baadhi wamejeruhiwa na wengine kupoteza maisha." Na kuongeza kuwa mafunzo hayo yaliyotolewa na TAWA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi yatasaidia kuongeza ufanisi na uwezo wa askari kukabiliana na ghasia kwa kutumia nguvu ya kadiri bila kuathiri haki za binadamu. Mhe. Mwansasu alieleza kuridhishwa na u...

TANESCO KUWAUNGANISHIA WATEJA UMEME NDANI YA SIKU MOJA.

Image
  Ni katika maadhimisho ya wiki ya huduma kwa Wateja yanayofanyika katika viwanja vya Mwembe yanga. RC Chalamila kuzindua utekelezaji mpango wa kuwakopesha majiko ya umeme wateja wapya watakaounganishiwa umeme na kulipa kupitia manunuzi ya umeme Na Josephine Maxime, Dar es saaam Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja, TANESCO imekuja na program maalumu ya kuwahudumia wateja wao Kwa kuwaunganishia wateja wapya huduma ya umeme ndani ya siku moja, ikiwa ni sehemu ya kusogeza huduma karibu na wateja wao. Akizungumza katika maadhimisho hayo yanayofanyika katika viwanja vya mwembe yanga jijini Dar es salaam Bi. Gowelle ameeleza kuwa TANESCO imekuja na program hiyo ya TANESCO Mtaani kwako kwa lengo la kuwahudumia wananchi wa mkoa wa Dar es salaam ambapo wafanyakazi muhimu wa vitengo mbalimbali vya shirika wameweka kambi kwenye viwaja hivyo kwa siku tatu kuanzia leo Oktoba 08 ili  kutoa huduma kwa wananchi. Vilevile amesema kwa siku ya alhamisi wanatarajia kuwa na hafla ya uzind...

WAMAMA 137 WANUFAIKA NA ELIMU YA POLIO HOSPITALI YA RUFAA MWANYAMALA

Image
  Na Mwandishi. Wetu --Dar es salaam Ikiwa zimesalia siku kadhaa Tanzania kuungana na nchi zingine duniani kuadhimisha siku ya Polio duniani Oktoba 24, 2025, klabu ya Rotary Mikocheni imetoa hamasa kwa wakina mama 137 kuhakikisha wanapojifungua watoto wao wanapata chanjo zote ikiwemo ya Polio wanapofikisha miezi 6 ili wawe salama. Ameyasema hayo Oktoba 2025, Rais wa Klabu ya Rotary Mikocheni Nasibu Mahinya katika Hospitali ya Rufaa Mwananyamala jijini Dar es salaam wakati wakihamasisha wakina mama kuhudhuria kliniki mara baada ya kujifungua ili watoto wao wapatiwe chanjo zote kuwaepusha na magonjwa yanayoweza epukika ikiwemo polio. "Hii ni wiki ya nane ya kampeni ya ‘Mama, Mkinge Mwanao!’ ambayo klabu ya Rotary tumeanzisha kwa kujitolea kuhamasisha wakina mama juu ya umuhimu wa chanjo ya Polio kwa wamama waliojifungua ili wahakikishe mara baada ya kuzaliwa watoto wao wanapata chanjo zote nne za Polio." Amesema rais Nasibu Sambamba na hayo amebainisha kuwa Polio ni ugonjwa hat...

NISHATI YAWASILISHA MIPANGO YA KIMKAKATI KUTEKELEZA DIRA YA TAIFA 2050

Image
Ni katika kikao kazi na Tume ya Taifa ya Mipango. Mradi wa usafirishaji umeme Chalinze–Dodoma ni miongoni mwa miradi ya kipaumbele kufanikisha Dira 2050, Wizara ya Nishati na Tume ya Mipango kushirikiana kwa karibu kusimamia miradi ya Nishati kufanikisha malengo ya Dira 2050. Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, amekutana na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Mipango wakiongozwa na Naibu Katibu Mtendaji – Menejimenti ya Utendaji na Tathmini, Dkt. Linda  Ezekiel kwa lengo la kujadili namna ambavyo Wizara na Taasisi zake zimejipanga kutekeleza miradi ya kimkakati ya nishati inayochangia katika kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Msingi wa kikao hicho umetokana na  Sekta ya Nishati kuainishwa katika Dira 2050 kuwa ni moja ya  vichocheo vitano vitakavyoongeza kasi ya kufikia malengo ya Dira hiyo, ikielezwa kuwa Nishati ya uhakika ni nyenzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya viwanda na shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kuboresha viwan...

DOYO AAHIDI KUFUNGUA KIWANDA CHA KOROSHO TUNDURU NDANI YA SIKU 10

Image
Ruvuma, Tunduru  Msafara wa mgombea urais kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, umewasili katika wilaya ya Tunduru, mkoa wa Ruvuma, ambapo umefanya mkutano mkubwa wa kampeni. Akihutubia wananchi wa Tunduru mjini katika viwanja vya Amazon na wananchi wa kijiji cha Nyakapanya, Mhe. Doyo aliwaahidi wananchi hao kuwa endapo watampa dhamana na ridhaa ya kuwa urais, atahakikisha anarejesha kiwanda cha kubagua korosho cha Wilaya ya Tunduru. Amesema kuwa kiwanda hicho kitakuwa nguzo muhimu ya kuinua uchumi wa wananchi wa Tunduru na kuchochea maendeleo ya mkoa wa Ruvuma kwa ujumla. Mhe. Doyo amesema kuwa utekelezaji wa mpango huo wa kufufua kiwanda ambacho thamani yake haizidi shilingi bilioni mbili, umekuwa ukikwamishwa na uzembe na dharau za viongozi wa chama tawala (CCM) kwa wananchi wa Tunduru. “Kama ukiangalia idadi ya mabango ya CCM, na kila bango moja lina thamani ya takribani shilingi elfu ishirini, utagundua kuwa tatizo si ukosefu wa fedha ba...

BRELA, MORUWASA Waipongeza TANESCO Mageuzi ya TEHAMA

Image
Ni kutokana na mabadiliko ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa Wateja Waahidi kuongeza ufanisi katika Taasisi zao kupitia mafunzo waliyoyapata Na Josephine Maxime, Dar es Salaam Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limepongezwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) pamoja na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA) kwa uwekezaji wake mkubwa katika teknolojia ya mawasiliano ambao umeimarisha kwa kiwango kikubwa huduma kwa wateja. Pongezi hizo zimetolewa na viongozi wa Taasisi hizo baada ya kufanya ziara ya mafunzo katika Kituo cha Huduma kwa Wateja cha TANESCO (Call Center), aambapo walishuhudia jinsi mifumo ya TEHAMA na huduma kwa wateja zinavyoshirikiana kutatua changamoto kwa haraka na kuongeza ufanisi. Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja TANESCO, Bi. Irene Gowelle, amesema TANESCO imekuwa ikifanya jitihada kubwa kuboresha huduma kwa wateja hatua ambayo imechangiwa pia na uwekezaji uliofanyika  katika teknolojia. “Tunaona ma...

WALIMU NI NGUZO YA MAENDELEO - WAZIRI MKUU MAJALIWA

Image
Asema Walimu ni fahari ya nchi na chimbuko la uvumbuzi na ubunifu Dkt. Biteko asema ualimu ndio taaluma inayomtengeneza mtu awe bora kuliko hata ualimu wenyewe Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa walimu ni nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote hapa duniani kwani ndio wanaotoa rasilimali watu yenye elimu ambayo ni muhimu zaidi kwa Taifa. Amesema kuwa mafanikio ya kielimu, kijamii na kiuchumi yanatokana na juhudi za walimu kwani walimu ni fahari ya familia, jamii na nchi na kupitia mikono yao vijana wa kitanzania wanajengewa maarifa, stadi na maadili ya uzalendo. Amesema hayo Oktoba 03, 2025 wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani ambayo kiwilaya imeadhimishwa Bukombe mkoani Geita katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Ushirombo. "Kila hatua ya ustawi wa kijamii na kiuchumi inaanzia darasani kupitia juhudi na maarifa ya walimu. bila walimu, hakuna taaluma, hakuna viongozi wa kesho na hakuna Taifa linaloweza kusimama imara, walimu ndio chimbuko la uvumbuzi na ubunifu w...