Posts

Showing posts from April, 2025

FURAHIKA YAWAFIKIA WAFANYAKAZI YAJA NA MPANGO HUU

Image
  Na Mwandishi wetu  Wafanyakazi wa Serikali na Sekta binafsi wametakiwa  kuchangamkia fursa ya  kujiunga na Chuo Cha Ufundi  Veta Furahika kwa ajili ya masomo ya jioni kwa kozi mbalimbali   Lengo la masomo hayo ya jioni kwa kundi hilo imeelezwa kuwa yanalenga kuwaongezea maarifa yenye tija yatakayoleta ufanisi katika majukumu yao ya kiofisi. Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Dkt. David Msuya amesema kwamba masomo hayo yatawasaidia waajiriwa kuongeza ufanisi katika utendaji wa majukumu ya kila siku na kuachana na kufanya kazi kwa mazoea na yataendana mahitaji ya sasa. "Masomo haya ya jioni kwa waajiriwa wa Serikali na Sekta binafsi yataanza Machi 5, 2025 kuanzia saa 11 jioni hadi 1:00 usiku hivyo tunawakaribisha wote kwa ajili ya ujenzi wa taifa letu," amesema. Dkt Msuya amezitaja kozi zitakazofundishwa chuoni hapo kwa muda wa jioni kuwa ni Public Administration (Utawala wa Umma), Human Resource Manag...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image

VIJANA WATAKIWA KUJITOKEZA KATIKA ZOEZI LA KUBORESHA DAFTARI LA MPIGA KURA

Image
  Na Mwandishi wetu  Katibu wa Idara ya Chipukizi na Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Jesca Mshana, amewataka vijana wa kitanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la kuboresha daftari la kudumu la mpiga kura awamu ya pili, linalotarajiwa kuanza Mei 1 hadi 7, 2025. Akizungumza na vyombo vya habari, Mshana amesema kuwa ni muhimu kwa vijana kutambua nafasi yao katika mustakabali wa taifa, kwa kuhakikisha wanajiandikisha ili wapate haki ya msingi ya kupiga kura. Ameongeza "Kupiga kura ni haki ya msingi na sauti ya mabadiliko. Vijana msikose kushiriki kwenye hatua hii muhimu ya kidemokrasia," Ameleza kuwa mchakato huo utaanza katika mikoa ya Geita, Mwanza, Ruvuma, Mbeya na Songwe, kabla ya kuhamia kwenye mikoa mingine 16 ikiwemo Dar es Salaam, Arusha na Kilimanjaro. Vilevile, kuanzia Mei 16 hadi 22, uboreshaji utaendelea katika vyuo vya elimu ya juu pamoja na vituo vya magereza. Aidha, Mshana amewataka vijana wajitokeze kugombea naf...

STEVE NYERERE - "NYUMBA ZA IBADA MUSIGEUZE GENGE LA SIASA"

Image
  Na Mwandishi wetu  Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao Steve Mengele (Steve Nyerere) amewataka viongozi wa nyumba za Ibada kurudi katika mstari wa kuhubiri amani na kuliombea taifa kwa maslahi mapana ya nchi . Aidha, amesema nyumba za Ibada kwa sasa zimekua genge la kuhubiri siasa badala ya kumuomba Mungu ili watu wapate kupona kutokana shida zao. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mapema leo katika Ofisi ya Taasisi hiyo amesema kuwa, nyumba  za Ibada zimekua zikitumia muda mwingi kutumia kuhubiri siasa badala ya kuhubiri amani kama ambayo tumezoea. Amesema kuwa, ameamua kuzungumza hayo baada ya kuona viongozi wengi wa kiroho wamekua wakigeuza nyumba za Ibada kama genge la kuhubiri siasa jambo ambalo si jema kwa taifa la Tanzania. Ameongeza kuwa, wanasiasa ni vyema kuhubiri siasa huko kwenye mikutano yao ya hadhara ili viongozi wa kiroho waendelee kutuvusha katika dhambi tulizonazo zipungue na waiombee Serikali na viongozi wetu wawe na maa...

OFISI YA CCM TAWI LA BUTIAMA YAZINDULIWA

Image
Na Mwandishi wetu Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala Chief Sylvester Yeredi amezindua ofisi ya Chama cha Mapinduzi tawi la Butiama iliyopo kata ya Vingunguti ilikarabaitiwa na Mstahiki Meya wa halmashauri ya jiji la Dar es salaam ambaye pia ni Diwani wa kata hiyo Mhe Omary Kumbilamoto. Akizungumza mara baada ya kuzindua ofisi hiyo Chief Yeredi amempongeza Meya Kumbilamoto kwa kuweza kutimiza wajibu wake kama Diwani kwa kusimamia ujenzi hadi kukamilika kwa ofisi hiyo ikiwa ni mwendelezo wake wa kukarabati na kujenga ofisi za Chama ndani ya kata ya Vingunguti. "Nimpongeza Diwani na Meya Kumbilamoto kwa jitihada zake hapa amesimamia ujenzi wa ofisi hii hadi kukamilika na hii sio hapa tu nimeona pia amefanya ukarabati mkubwa katika ofisi yetu ya CCM kata ya Vingunguti na maeneo mengine ya Chama" amesema Chief Yeredi  Nae Meya Kumbilamoto amesema lengo la ujenzi wa ofisi hiyo ni kuweka ustawi nzuri wa chama, na hiyo inatokana na kazi kubwa anayoifanya Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya ...

WASIRA AMTAHADHARISHA MARTHA KARUA WA KENYA KUJIPIMA UBAVU NA CCM

Image
Asema kama anajiona anaweza kutatua migogoro aende nchi nyingine za Afrika Na Mwandishi Wetu,Dodoma MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira amemjia juu Mwanasheria maarufu na mwanasiasa wa nchini Kenya Martha Karua,  ambaye amekuja nchini kumtetea Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu,  anayekabiliwa na tuhuma za uhaini na kuchapisha picha za uongo mtandaoni. Wasira amemtaka mwanasheria huyo kuacha kujipima uzito na Chama Cha Mapinduzi huku akimwambia pia kuwa Chama kinaheshimu mamlaka ya Mahakama na Tume Huru ya Uchaguzi (INEC). Amesisitiza kama Karua anajiona anaweza kushughulika na migoro basi atatue matatizo yaliyoko nchini kwake au mgogoro unaoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya  Congo (DRC).  Akizungumza mbele ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma Leo Aprili 25, 2025 , akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuelezea faida za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Wasira ali...

BODI YA ITHIBATI YAWAONYWA WANAOJINYEZA KWENYE UANDISHI WA HABARI

Image
  Na Mwandishi Wetu, JAB Mwenyekiti wa Bodi hiyo Tido Mhando amewaonya watu ambao wanaia ya kutumia vyeti visivyo halali wakati wa kujaza taarifa zao katika usajili wa waandishi habari ili kupatiwa kitambulisho Cha uandishi wa habari (Press Card) . Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) Leo imefungua rasmi mfumo wa usajili wa Waandishi wa Habari wa https://taihabari.go.tz ili kuomba kuthibitishwa na kupatiwa Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Cards)  Mhando alitoa tahadhali hiyo tarehe 19 Mei, 2025 wakati akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vya Habari katika ofisi za Bodi hiyo zilizopo Mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam. “Ndugu zangu Waandishi wa Habari, Bodi hii itaanza kutoa ithibati kwa waandishi wa habari wote kupitia mtandao na kutoa vitambulisho vya kidijiitali (digital Press Card). Maombi ya ithibati Press Cards yatafanyika kupitia Mfumo unaoitwa TAI-Habari”, alisema. Mhando alisema mahitaji muhimu wakati wa kujaza taarif...

WASIRA:CCM TUNAHUBIRI AMANI KWA SABABU NDANI YAKE KUNA HAKI

Image
Asisitiza Chama hakiwezi kukubali mtu au kikundi cha watu kuvuruga amani iliyopo Na Mwandishi Wetu, Tabora MAKAMU Menyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Stephen Wasira, amesema ni vema wananchi wakafahamu kwamba katika amani ndani yake kuna haki, hivyo Chama kitaendelea kuihubiri kuhakikisha inapatikana haki. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mjini Dodoma alipokuwa akihitimisha ziara yake katika Mkoa wa Tabora, jana, Wasira amesema kuna watu wanahoji CCM inazungumzia sana amani lakini haizungumzii haki, huku akibainisha kuwa wanaotoa madai hayo  ni watu wazito. “Sasa nikasema ngoja niende (Tabora) kwenye kitovu ambapo Mwalimu Julius Nyerere alitoa machozi kwa ajili ya amani, tuwasaidie kuelewa kwamba ukizungumza amani ndani ya amani kuna haki kwa sababu amani ikikosekana wenye uwezo mdogo wanaumia. “Amani ikikosekana wanawake na watoto wao katika nchi jirani wanakilimbilia Tabora...ukilinda amani unalinda haki tena unalinda haki ya wanyonge, unalinda h...

SERIKALI INAENDELEA NA UKARABATI WA MIUNDOMBINU YA UMEME – KAPINGA

Image
Lengo ni kuondokana na changamoto ya kukatika kwa umeme Ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kilindi, Tanga waffikia asilimia 35. Bilioni 2.63 kulipa fidia wanaopisha njia ya kusafirisha umeme Mkata- Handeni-Kilindi Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya kusambaza umeme ili kuondokana na changamoto ya kukatika kwa umeme nchini. Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Aprili 10, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Handeni Mjini, Mhe. Reuben Kwagilwa aliyeuliza ni lini Serikali itaondoa changamoto ya kukatika kwa umeme wilayani Handeni. "Changamoto ya kukatika umeme Wilayani Handeni inatokana na uchakavu na urefu wa miundombinu ya kusambaza umeme. Katika kukabiliana na changamoto hii Serikali kupitia TANESCO inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya umeme ikiwa ni pamoja na kubadilisha nguzo za miti na kuweka za zege". Amesema Kapinga Ameele...

MAKALLA AANZA ZIARA MKOA WA LINDI

Image
  Akagua barabara na madaraja  SOMANGA Atoa pole na kumshukuru Rais Samia kutoa fedha zaidi Bilioni 100 kujenga madaraja Ampongeza Waziri Abdallah Ulega na Tanroad kwa kuwahi na kusimamia matengenezo KATIBU wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi and Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla amewasili mkoani Lindi leo Aprili 10,2025 kwa ajili ya ziara yake katika mikoa miwili ya Lindi na Mtwara. Awali baada ya kuwasili mkuani humo alipita katika Kata ya Somanga Mtama iliyopo katika Jimbo la Kilwa Kaskazini mkoani Lindi kwa ajili ya kusalimia wananchi wa eneo hilo. Aidha, Makalla kabla ya kusalimia wananchi hao alitembelea katika daraja la Somanga Mtama ambalo lilikatika na kupelekea kupotea kwa mawasiliano katika barabara ya Dar es salaam-Lindi na kuangalia hali inavyoendelea katika daraja hilo. Akizungumza katika eneo baada ya Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega kutoa ufafanuzi mfupi Makalla alimpongeza kwa weledi mkubwa aliouonyesha kwa kuweza kurudisha mawasilia...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

RC CHALAMILA AFANYA ZIARA KIBAMBA, ATOA MAAGIZO HAYA

Image
Na Mwandishi wetu Dar  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert  Chalamila ameahidi kutoa shilling mill 100 kwa ajili ujenzi wa Zahanati ya Saranga kupitia ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo. Kauli hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati alipokua katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Kibamba sambamba na kuskiliza kero za wananchi ikiwemo afya, maji, barabara pamoja na Tasaf. Amesema kuwa, licha ya Rais Dkt Samia kutoa fedha nyingi kwa ajili ya sekta ya Afya kwa kujenga hospital kubwa, kuongeza madaktari bingwa na kuongeza vifaa tiba lakini hajawaacha wananchi wa Kata ya Saranga. Aidha, amemtaka fundi ujenzi aliyejenga kituo cha Afya cha mama na mtoto Mpiji Magoe kufanya marekebisho ya dosari alizozigundua mara moja kabla ya kumchukulia hatua za kumpeleka gerezani akajenge milango ya magereza. "Ukiondoa taaluma yangu, pia ninauwelewa wa masuala ya ufundi, hivyo kwa kuangalia tu, yapo baadhi ya makosa ambayo tayari nimeelekeza uy...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

VITONGOJI 9000 KUSAMBAZIWA UMEME MWAKA 2025/2026- KAPINGA

Image
Majimbo yaendelea kufaidika na mradi wa  umeme wa Vitongoji 15. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha kazi ya kupeleka  umeme kwenye Vijiji vyote Tanzania Bara na  nguvu sasa inaelekezwa kwenye vitongoji. Mhe. Kapinga  ameeleza kuwa, pamoja na kazi ya kupeleka umeme vitongojini inayoendelea sasa,  Serikali ina mkakati wa kupeleka umeme kwenye Vitongoji 9,000 katika mwaka ujao wa fedha wa 2025/26. Ameeleza hayo leo Aprili 09, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Nkansi Kusini, Mhe. Vicent Mbogo aliyeuliza ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vitongoji vilivyopo Jimbo la Nkansi Kusini.  "Kitongoji cha Lupata kilichopo Kata ya Kizumbi kitapata umeme kupitia mradi wa Vitongoji 15 vya kila Mbunge, na kitongoji cha Lwela Kata ya Mpembe kitapata umeme kupitia miradi itakayokuja". Amesema  Kapinga Akijibu swali Mbunge wa Momba, Mhe. Condester Sichwale ali...

STEVE NYERERE KUNOGESHA TAMASHA LA MTOKO WA PASAKA

Image
Na Mwandishi wetu, Dar  Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao Steve Mengele maarufu kama (Steve Nyerere) ni miongoni mwa watu mashuhuri watakaohudhuria katika tamasha la mtoko wa Pasaka litakalofanyika jijini Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Steve Nyerere amesema kuwa siku ya sikuu ya Pasaka kutafanyika tamasha kubwa la mtoko wa Pasaka ambapo litawakutanisha wasanii nguli wa mziki wa injili. "Maombi yana nguvu kuliko mtutu wa bunduki,maombi yana nguvu kuliko matusi,maombi yana  nguvu kuliko kitu kingine chochote,hivyo siku hiyo tutaliombea Taifa na Rais Wetu Mpendwa Dkt Samia Suluhu Hassan "amesema Ameongeza "sisi tumeona ndani ya mwezi huu(April)kulikua na mambo mengi ikiwemo ramadhani, kwaresma,na sasa tunelekea kwenye sikukuu ya Pasaka,hivyo kuelekea kilele cha sikukuu ya pasaka tutatoa pakeji ya vifaa vya kumsaidia mama mjamzito kujifungua katika Hospitali zote za Wilaya Mkoani Dar es salaam"  Aidha, Steve amempongez...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

MSHINDI WA KWANZA KUJINYAKULIA MILL 10, NGAO NA CHETI TUZO YA MWALIMU NYERERE

Image
  Na Mwandishi wetu Tuzo ya kitaifa ya Mwalimu Nyerere ya uandishi wa bunifu itatolewa April 13 jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa super Dome Masaki ambapo itahusisha mkusanyiko wa mashairi, tamthilia, hadithi za watoto na Riwaya . Aidha, mshindi wa kwanza wa tuzo hiyo atajinyakulia kitita cha shill mill 10, ngao pamoja na cheti na muswada wake utachapishwa na kusambazwa shuleni na kwenye maktaba za taifa, Mshindi wa Pili: Tuzo ya Shilingi Milioni 7 pamoja na Cheti, Mshindi wa Tatu: Shilingi milioni 5 na Cheti.  Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo hiyo, Prof. Penina Oniviel Mlama, amesema Kamati imetoa taarifa hiyo leo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya hafla ya kilele cha utoaji wa tuzo hizo. Aidha, Prof Mlama ameishukuru jamii ya wanahabari kwa mchango wao mkubwa katika kuitangaza Tuzo hiyo tangu ilipoanzishwa katika mwaka wa fedha 2022/23. "Kamati ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu leo imetangaza zawadi ...

PROF LIPUMBA ATOA RAI HII KWA SERIKALI

Image
  Na wandishi wetu  Chama cha Wananchi (CUF) kimeitaka Serikali kupitia hotuba za bajeti ya mwaka huu kuchambua sababu za nini haifikii malengo ya Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama hicho Prof. Ibrahim Lipumba Wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya mtazamo wa CUF kuhusu Bajeti ya Mwisho ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo 2021/22 hadi 2025/26. Amesema kuwa kikao cha Bunge la Bajeti kinatarajiwa kuanza Aprili 8, 2025 na kwamba hii itakuwa Bajeti ya mwisho ya utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa Maendeleo 2021/22 – 2025/26 na mwaka wa mwisho wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, bajeti za Serikali zilizopita hazijajikita katika utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo.  Prof. Lipumba amebainisha kuwa utaratibu wa zamani wa hotuba za Bunge la Bajeti ulianza na hotuba za Waziri wa Mipango na Waziri wa Fedha kueleza hali ya uchumi na utekelezaji wa mipango ya maendeleo na mapendekezo ya mapato na matumizi.  "Hiv...

MRADI WA KUFUA UMEME WA JNHPP WAKAMILIKA RASMI: DKT BITEKO

Image
Asema ni ndoto ya watanzania,awataka wategemee umeme wa uhakika Asisitiza kazi iliyobaki ni kuimarisha miundombinu ya kuwafikishia wananchi umeme Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Misri kuuzindua rasmi Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kutegemea kupata umeme wa uhakika baada ya Mradi wa kufua umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere uliokuwa ukisubiriwa kwa shauku kubwa na Watanzania  kukamilika  rasmi. Waziri Biteko ameyasema hayo leo April 5, 2025 baada ya kutembelea Mradi huo akiwa ameambatana na Mawaziri ambao ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mha. Hamadi Masauni. Amesema hivi sasa mitambo yote tisa inafanya kazi ambapo amefafanua kuwa  kukamilika kwa Mradi huo kumechangiwa na maono ya Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Dokta Samia Suluhu Hassan ambaye aliupokea Mradi ukiwa katika asilimia 33 ya utekelezaji wake na ndani y...

TIMU YA YANGA YAKOSHWA NA "MAAJABU" YA TABORA ZOO

Image
Pacome, Diarra wavutiwa na mnyama Simba Na Beatus Maganja, TABORA   Viongozi na wachezaji wa Timu ya Young Africans (Yanga) leo hii wamefanya ziara katika Bustani ya Wanyamapori Hai Tabora, maarufu kama Tabora Zoo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukuza utalii wa ndani na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini. Ziara hii iliongozwa na Rais wa Klabu ya Yanga, Injinia Hersi Said ikijumuisha wachezaji maarufu wa klabu hiyo. Katika mazungumzo yake baada ya ziara, Injinia Hersi Said alisema kuwa lengo kuu la ziara hiyo ni kuonyesha mchango wa klabu ya Yanga katika kukuza utalii wa ndani na vilevile kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kutangaza vivutio vya utalii vya nchi yetu.   “Ziara yetu hapa ni sehemu ya kuonyesha michango yetu katika kukuza utalii wa ndani, ikiwa ni njia mojawapo ya kuhamasisha Watanzania kutembelea vivutio vyetu vya utalii, lakini pia kuchang...