Posts

Showing posts from February, 2025

HIKI NDICHO ALICHOKISEMA DIWANI SHABANI KUHUSU MNADA WA PUGU,WADAU KUCHANGIA UJENZI WA OFISI

Image
LICHA ya kufanya harambee kwa ajili ya kujenga ofisi ya wafanyabiashara wa Pugu Mnadani imeelezwa kuwa kuna Changamoto ya wafanyabiashara kupeleka ngo'mbe zao moja moja kwa moja kwenye machinjio bila kuzitisha kwenye Mnada hali inayochangia kurudisha nyuma maendeleo ya Mnada mkuu wa Pugu. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya harambee hiyo, jijini Dar es Salaam, Diwani wa Kata ya Pugu Stesheni Shaban Mussa amesema kwa sasa mzunguko wa fedha umeshuka katika Mnada huo kutoka shill Bill 1.2 kwa siku hadi kufikia shill mill 800. Amesema kuwa, kuna wafanyabiashara ambao sio waamini wanabeba mifugo kutoka mikoa mbalimbali hawaifikishi Mnadani na kupeka machinjioni moja kwa moja ambapo kisheria mifugo yote inatakiwa kufika mnadani hapo washushe ili wanunuzi wanunue na kwenda kuchinjwa machinjioni.  "Wanapopeleka ngo'mbe moja kwa moja machinjioni sisi hapa hatuwezi kupata fedha kwani sheria za machinjio haziruhusu kukusanya ushuru ngo'mbe zikiwa nzima, bali ...

RC CHALAMILA KUWAONGOZA WATANZANIA PAMBANO LA KNOCK OUT YA MAMA

Image
IKIWA yamebaki masaa chache kushuhudiwa kwa mapambano kali la ngumi ambalo lilikuwa linasubirowa kwa hamu kubwa, imeelezwa kuwa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert  Chalamila anatarajiwa kuwaongoza Watanzania kushuhudia  mapambano hayo ya ngumi yasiyokuwa ya kuwania mkanda yanayopigwa leo, Feb 28 katika Ukumbi wa Magomeni Sokoni jijini humo. Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimepatikana wakati mchakato wa kutambulisha mabondia watakaotwangana leo katika ukumbi huo, kwamba Mkuu wa Mkoa huo, Chalamila atakuwa miongoni mwa viongozi watakaokuwemo ukumbini humo kushuhudia mapambano hayo. "Wakati tukiendelea 'Face Off' kwa mabondia watakaopigana (kesho), leo nimepata taarifa kuwa Mkuu wetu wa Mkoa anatufuatilia kupitia mitandao ya Kijamii ambayo ipo mubashara kwa sasa na ameahidi kuwepo kushuhudia," alisikika mmoja wa washehereshaji akisema. Mchakato wa kutambulisha mabondia hao lililokwenda sanjari na tambo kutoka kwa mabondia ilisababisha bondia Abdallah Pazzy 'Dullah Mbabe...

HUU HAPA UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

CHUO CHA BAHARI DAR ES SALAAM (DMI) KUTOA MAFUNZO YA MANUFAA YA UCHUMI WA BULUU KWA VIJANA

Image
Na Mwandishi wetu  Mkuu wa chuo cha Bahari Dar es Salaam Prof. Tumaini Gurumo amesema kuwa chuo cha bahari Dar es Salaam (DMI) kimeona kunafursa nyingi katika uchumi wa buluu hivyo kinatazamiwa kuanzisha mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa vijan kusiana na manufaa katika uchumi wa  buluu. Prof. Gurumo ameyasema hayo kwenye kongamano la uchumi wa buluu lilifanyika jiji Banjul nchini Gambia. “Kweli  katika kongamano hili tumakubaliana nchi zote za Afrika kutumia vyanzo vyetu vya maji kama vila bahari, mito mabwa, maziwa na vyanzo vingine kuhakiisha vinasaidia jamii za kiafrika hivyo sisi DMI tutaanzisha masomo kwa vijana kuonyesha fursa za Uchumi wa Buluu” Asema Gurumo Kwa upande wake Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Uchukuzi Bi Stella Katondo amesema kuwa kongamo hilo limewakutanisha wataalam  kutoka nchi zaidi ya kumi na Sita za Afrika ni muhimu sana kwa maendeleo na manufaa ya uchumi wa buluu. Hivyo kwa chuo cha DMI imepata nguvu ya kuendelea kutoa...

SERIKALI IMEIMARISHA USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA UONGOZI NA SHUGHULI ZA KIUCHUMI-KAPINGA

Image
Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani atoa wito wa kushikamana Naibu Waziri Nishati,  Mhe. Judith Kapinga amesema kuwa Serikali imeboresha mazingira ya wanawake nchini ili waweze kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kiuchumi, maendeleo ya Tanzania na kushika nafasi za uongozi. Mhe. Kapinga ameyasema hayo alipokuwa akielezea nafasi ya mwanamke katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya  Wanawake Duniani ambayo nchini yatafanyika mkoani Arusha. "Kipekee namshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani amekuwa dira ya kutuongoza na kuhakikisha wanawake wengi zaidi tunashiriki katika shughuli za maendeleo na hata katika nafasi za uongozi." Amesema Mhe. Kapinga Amesema Rais Samia amekuwa kinara katika kuibua wanawake katika sekta mbalimbali za kiuchumi nchini.  Ameitaka jamii kuondokana na dhana kwamba mwanamke anapopewa nafasi ya uongozi anaweza kusahau majukumu yake mengine ya kijamii.  Aidha, Mhe. Kapinga ametoa wito kwa wanawake kupendana, kushikamana, kus...

BONDIA AMIRI MATUMLA KUZICHAPA NA AMAVILA FEB 28

Image
  Na Mwandishi wetu  Mkurugenzi wa Mafia Boxing Promotion Ally Zayumba amesema kuwa pambano la knock out ya mama msimu wa tatu litanogesha na mapambano 12. Aidha katika pambano la knock out ya mama msimu wa tatu bondia Amiri Matumla atazichapa dhidi ya mpinzani wake Paul Amavila kutoka Nchini Namibia.  Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam Zayumba amesema kuwa mapambano hayo yanatarajiwa kufanyika Februari 18 Mwaka huu jijini Dar es Salaam. Zayumba amebainisha kuwa katika usiku huo pambano kuu lolitakuwa ni la Bondia Amiri Matumla ambaye atapanda ulingoni katika Ukumbi wa Magomeni Sokoni kuzichapa dhidi ya mpinzani wake kutoka Namibia, Paul Amavila. Amebainisha kuwa Bondia Matumla katika pambano hilo atazichapa  na mpinzani wake huyo kwa mizunguko nane. "Hili ni pambano lake la kwanza tangu ajiunge kwenye mapambano ya ngumi za kulipwa na ameahidi kufanya vizuri kwa lengo la kuanza kutengeneza rekodi nzuri katika karia yake kupitia masumbwi," a...

UJENZI KITUO CHA KUPOZA UMEME HANDENI KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME- RAIS SAMIA

Image
Kituo  kugharimu  shilingi bilioni 50 Zaidi ya Shillingi billioni 98 kutekeleza mradi wa gridi imara Kilindi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema utekelezaji wa ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Handeni mkoani Tanga  utakapokamilika utaboreha upatikanaji wa umeme katika Wilaya za Handeni  na Kilindi pamoja na maeneo jirani. Rais Samia ameyasema hayo leo Februari 25, 2025 katika ziara yake mkoani Tanga wakati akizungumza na wananchi wa Handeni mara baada ya kuzindua Shule ya Wasichana ya Kilindi na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.  "Tatizo la umeme hapa Handeni Serikali inalifahamu, imeanza kuchukua hatua kwa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme   kitakachogharimu takribani  shilingi  bilioni 50 za kitanzania ambacho kitaboresha upatikanaji wa umeme." Amesema Rais Samia Ameeleza kuwa,  upatikanaji wa umeme wa uhakika Handeni utasaidia ukuaji wa uchumi pamoja na kuyainua madini ...

AFARIKI AKIWA SAFARINI AKITOKEA MWANZA KWENDA DAR

Image
  Na Lilian Kasenene, Morogoro KIJANA aliyefahamika Godfrey Mbaga anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka (25-30)mkazi wa Mwanza amefariki Dunia wakati  akisafiri akitokea mkoa wa Mwanza kuelekea Dar es Salaam kwa basi la Dragon mali ya kampuni ya Ally's. Kamanda  wa polisi mkoa wa Morogoro Alex Mkama alisema tukio hilo limetokea Februari 23, 2025 majira ya asubuhi eneo la Mikese Wilaya ya Morogoro na kwamba alipanda basii lenye namba za usajili T 433 EBG. Mkama alisema marehemu wakati wakiwa safarini walipofika eneo la Mikese abiria huyo alianza kujisikia vibaya na kufikishwa hospitali kwa matibabu lakini hakupata nafuu na hatimaye alifariki dunia. Alisema mwili wa marehemu Godfrey umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hospital ya rufaa mkoa wa Morogoro kusubiri ndugu wa marehemu kwa ajili ya utambuzi na uchunguzi. Wakati huo huo  Februari 24, 2025 majira ya asubuhi katika eneo la Cape town mtaa wa Kambi tano kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro ulipatikana mwi...

KOROGWE WAIPONGEZA SERIKALI UTEKELEZAJI MIRADI YA UMEME

Image
Ni katika ziara ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Tanga Vijiji vyote 118 vyafikishiwa umeme Naibu Waziri Kapinga ashiriki ziara. Wananchi wa Wilaya ya Korogwe wameipongeza Serikali kwa utekelezaji wa miradi  ya umeme Vijijini ambapo katika wilaya hiyo  vijiji vyote vimefikishiwa umeme. Pongezi hizo zimetolewa kupitia Mbunge wa Korogwe Vijijini  Mhe. Timotheo Mzava leo Februari 24, 2024 wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Wilayani Korogwe kukagua miradi ya maendeleo.  "Tarehe 15 mwezi wa tatu 2021 ulikuwa kwenye viwanja hivi na sisi wabunge tulipata nafasi ya kusema.Tuliyoyaomba ikiwemo ya umeme vijijini umeyatekeleza tunakushukuru sana." Amesema Mhe. Mzava Amesema wakati huo wa ziara ya Rais Samia walieleza kuhusu changamoto ya upatikanaji umeme ambapo  Vijiji 54 kati ya 118 vilikuwa havina umeme. Mhe. Mzava ameongeza kuwa hivi sasa vijiji vyote 118 vya Korogwe Vijijini vimefikiwa na nishati  ya u...

TMA YATOA TAHADHARI UPEPO MKALI DAR, TANGA, PWANI

Image

KAMATI YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA UANDAAJI WA MPANGO KAZI WA KITAIFA WAKUTANA DAR

Image
Na Mwandishi wetu  Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi wa Uandaaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu na Biashara imefanya kikao maalum kuhakikisha kuwa rasimu ya mpango kazi huo inakidhi viwango vya kitaifa na kimataifa katika kulinda na kuheshimu haki za binadamu ndani ya mazingira ya biashara  Aidha, pamoja na mambo mengine timu hiyo ya wataalam imekabidhi rasimu ya awali ya mpango kazi huo kwa kamati lengo ikiwa ni kufanya mapitio na kuidhinishwa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mohamed Khamis Hamad amesema kuwa, mpango kazi huo utakuwa na mikakati ambayo inahusiana na masuala ya haki za binadamu katika shuguhuli za kibiashara, Serikali baada ya kuridhia itaikabidhi wizara ya katiba na sheria ya Tanzania bara na Zanzibar kwa ajili ya kuratibu mchakato mzima. Aidha, kikao hicho kimejumuisha wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali, sekta binafsi, asasi za kiraia, na wataalam wa ma...

ETDCO YAIBUKA KIDEDEA TUZO ZA ZICA

Image
Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme nchini (ETDCO) imebuka mshindi katika kipengele cha Mkandarasi Bora wa Ujenzi wa Miundombinu ya Umeme, katika Tuzo za Zanzibar International Construction Awards (ZICA) zilizofanyika Februari 22, 2025, Zanzibar. Akizungumza wakati akikabidhi Tuzo kwa Washindi, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Mhe. Dkt. Khalid Salum Mohamed, amesema kuwa  sekta ya ujenzi ni msingi mkuu wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku  akiwataka washiriki wote kutumia tuzo hizo kama chachu ya kuendelea kufanya kazi kwa  bidii ili kufikia viwango vinavyohitajika na kuleta tija kwa Taifa. Kaimu Meneja Mkuu wa  ETDCO CPA. Sadock Mugendi, ameishukuru ZICA kwa kutambua mchango wao  katika sekta ya ujenzi wa miundombinu ya umeme nchini, na kuahidi kuendelea kutoa huduma zenye viwango ili kukuza uchumi wa nchi. "ETDCO tumejipanga kuhakiksha tunaboresha matumizi ya teknolojia kwa kununua mashine...

HUU HAPA MSIMAMO WA NLD KUELEKEA UCHGUZI MKUU

Image
  Chama Cha National League for Democracy (NLD) kimesisitiza kuwa hakina mpango wa kushirikiana na chama kingine chochote cha siasa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu 2025. Akizungumza mapema leo februari 23, 2025 wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kamati kuu jijini Dar es salaam katibu mkuu wa chama hicho, Doyo Hassan Doyo amesema historia mbaya walioipata  katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 mara baada ya kushiriki na kuungana na vyama vingine kupitia umoja wa UKAWA chama hakipo tayali kushirikiana na chama chochote kwa sasa. "Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 chama chetu kilikuwa moja ya vyama vilivyoshiriki kuunda umoja wa UKAWA na kuzunguka kufanya kampeni nchi nzima kwa kutoa mda, asilimali zetu lakini baada ya kutangazwa kwa matokeo chama akikuweza kupata faida yoyote zaidi ya kuwanifaisha wengine kwa kupata wabunge na madiwani nchi nzima". Alisema Doyo Alisema kufatia madhira hayo na siku za hivi karibuni kumekuwepo na tamko la CHADEMA lililotolewa kupitia M...

WAKANDARASI WASIMAMIWE KUTEKELEZA MIRADI YA NISHATI KWA WAKATI - KAPINGA

Image
Aagiza  wasimamiwe kwa karibu kumaliza miradi Awataka Watendaji TANESCO kuwa na mahusiano mazuri na wananchi Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amewataka watendaji wa Sekta ya Nishati kuwajengea uwezo watoa huduma wanaotekeleza miradi mbalimbali ya sekta ya nishati nchini.  Hayo ameyasema leo Februari 23, 2025 na Kapinga wakati akizungumza na wafanyakazi wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO, na wakuu wa taasisi za wizara kabla ya kushiriki ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan inayotarajiwa kuanza leo mkoani Tanga. "Tunataka hii miradi ikamilike kwa wakati na kwa ubora mkubwa, wakandarasi wajengewe uwezo wa utendaji kazi ili kazi ionekane inafanyika, " Ameongeza Mhe. Kapinga.  Aidha, ameipongeza REA kwa kumaliza kufikisha umeme kwenye vijiji vyote nchini na kusisitiza miradi inayoendelea na ile inatakayoanza mwaka huu wa fedha itekelezwe kwa wakati.  "Ni muhimu sana kuwasimamia wakandarasi kwa nguvu kuanzia mwanzo tuwe na...

SHIGONGO AFUNGUKA MAZITO KUHUSU BUCHOSA, AMPA MAUWA YAKE DKT SAMIA

Image
Mbunge wa Jimbo la Buchosa, wilayani Sengerema Erick Shigongo amesema ana kila sababu ya kumpongeza na kumshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa maendeleo makubwa aliyoyafanya jimboni kwake. Akizungumza na waandishi wa habri leo jijini Dar es Salaam Mbunge huyo amesema Rais Dkt Samia amefanyia mambo makubwa ikiwemo kugusa sekta zote muhimu ikiwemo afya, elimu, maji ambapo huduma zote hizo hapo awali ilikua ngumu kupatikana kwake. Amesema kuwa, yeye amekua ni shuhuda namba moja kwa maendeleo hayo kwani alikua akitembea umbali wa kilomita tisa kwenda na kurudi shule ambapo kwa sasa kadhia hiyo imebaki historia. "Ndani ya miaka minne ya uongozi wa Serikali ya awamu ya sita, mimi kama mbunge wa Jimbo la Buchosa nimepokea zaidi ya bilioni 62.3 ambapo tumejenga barabara, Sekondari mpya 8, Zahanati 21 vituo vya Afya 5, hilo linatosha kusema kwamba Serikali ya Dkt Samia anawapenda wanabuchosa"amesema Shigongo. Amesema pamoja na kuyumba kwa uchumi...

BALOZI WA ASANTE MAMA, WAFUNGUKA YUMO SHAMSA FORD, MAFUFU, JB, KINGWENDU

Image
  Msanii wa filamu, Jimmy Mafufu akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari juu ya uamuzi wake wa kuhamia chama cha mapinduzi (CCM) mkutano uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam Shamsa Ford aliyekuwa kada wa chadema akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa habari juu ya uamuzi wake wa kuhamia chama cha mapinduzi (CCM) mkutano uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam. Msanii wa maigizo Single mtambile maarufu kama Richie akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari juu uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam. Msanii wa muziki wa kizazi kipya Boniventure Kabongo maarufu kama ‘Stamina" akielezea sababu za kujiunga na CCM katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam. Dar es salaam - Wasanii wa filamu, Jimmy Mafufu na Shamsa Ford wametangaza rasmi kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na sasa wakiwa chini ya Taasisi ya Mabalozi wa Mama na wataanza ziara nchi nzima kutangaza ...

DIWANI LUCY LUGOME KUWAWEZESHA WANAWAKE KWA KUGAWA KUKU BURE

Image
DIWANI wa Kata ya Kisukuru Lucy Lugome, amesema miongoni mwa mikakati yake ndani ya kata ya Kisukuru wilayani Ilala ni kuwawezesha kiuchumi Wanawake kupitia vikundi vyao kwa kugawa kuku bure 50 ili waweze kukuza mitaji yao kupitia vikundi  . Diwani Lucy Lugome, alisema hayo Dar es Salaam jana, katika mkutano wake wa wananchi ambapo mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo, na mgeni Maalum Meya wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto.  Wanawake wezangu wa Kusukuru kuna fursa inakuja kwa ajili ya kukuza uchumi kwa kushirikiana na wadau wangu wa Maendeleo hivyo kuna utaratibu maalum utawekwa, utaratibu kupitia vikundi vyenu muweze kupata kuku bure kupitia vikundi vyenu tuwawezeshe kiuchumi "alisema Lugome.  Diwani Lucy Lugome  aliwataka wanawake wa Kisukuru kufuata utaratibu ili waweze kupata fursa hiyo kila mmoja kwani Kisukuru ya kisasa ya maendeleo inakuja . Aliwataka wananchi, na wanawake wa Kisukuru kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri...

NLD YAJIWEKA MGUU SAWA NA UCHAGUZI MKUU

Image
Chama cha National league for Democracy kimesema kimeanza kujiweka mguu sawa katika maandalizi ya uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika hapo badae. Akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari Makao Makuu ya chama hicho, Tandika jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, alielezea hatua zinazochukuliwa na chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. .Doyo alisema kuwa chama hicho kimeanza kufanya vikao mbalimbali vya tathmini ya Uchaguzi uliopita, hususan Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, vijiji, na vitongoji, huku lengo kuu likiwa ni kujiandaa kikamilifu kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu. Aliongeza kuwa tathmini hiyo inalenga kubaini namna chama hicho kitakavyoshiriki katika uchaguzi huo mkubwa na kuhakikisha kuwa hakikosi nafasi yake katika ulingo wa siasa. Pamoja na kukutana na changamoto katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, vijiji, na vitongoji, Katibu Mkuu wa NLD alisisitiza kuwa hilo halitakuwa kikwazo kwa c...

OPARESHENI YA KUWADHIBITI FISI SIMIYU YAONESHA MAFANIKIO MAKUBWA

Image
📍 Zaidi ya Fisi 16 wavunwa. Na Mwandishi wetu, Simiyu. Oparesheni maalumu ya kuwadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu aina ya fisi waliokuwa wanaleta taharuki na madhara Kwa jamii inayoendelea Mkoani Simiyu imeonesha mafanikio makubwa baada ya fisi 16 kuvunwa ikiwa ni hatua muhimu iliyochukuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii ya kuhakikisha usalama na utulivu Kwa wananchi vinarejea. Hayo yamesemwa leo Februari 19, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenani Kihongosi alipokuwa akiongea na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari. Mhe. Kihongosi amesema kufuatia changamoto hiyo,  Serikali ilichukua jukumu kubwa la kuhakikisha inalinda wananchi wake ikiwemo kuanzisha oparesheni maalumu inayohusisha Jeshi la Uhifadhi Kwa Taasisi za TAWA, TANAPA na TFS Kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi pamoja na wananchi, oparesheni inayotajwa kuanza  Januari 25, 2025. "Tarehe 20/12/2024 baada ya fisi kuvamia wananchi Serikali ilichukua hatua kubwa ya kushirikisha vyombo ...

MAMA SAMIA LEGAL AID YAFIKIA WANANCHI ZAIDI YA MILIONI 1-MAJALIWA

Image
_Asema kampeni hiyo ni ubunifu wa Rais Dkt. Samia ya kuwasaidia Watanzania wasio na uwezo kupata huduma za kisheria bure._ WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ni ubunifu wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan uliolenga kuongeza wigo wa upatikanaji haki kwa wananchi wasio na uwezo wa kumudu gharama za huduma za kisheria. Amesema kuwa kupitia kampeni hiyo ambayo inatolewa bure mpaka sasa imefanikiwa kuwafikia zaidi ya wananchi milioni moja wakiwemo wanawake 681,326 na wanaume 691,773 katika mikoa 19 nchini. Amesema hayo leo Jumatano (Februari 19, 2025) wakati alipozindua kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika mkoa wa Lindi, kwenye viwanja vya Madini, Ruangwa Mkoani Lindi. “Mheshimiwa Dkt. Samia alijifunza shida, kero na changamoto wanazopata watanzania na hasa wale ambao hawana uwezo wa kulipia gharama za huduma za kisheria, aliguswa na akaamua kuanzisha kampeni hii na kuikabidhi Wizara ya Katiba na Sheria isim...

MHE. BITEKO AMPONGEZA MWANAFUNZI ALIYEELEZEA MIRADI YA UMEME

Image
   Amuahidi kutembelea mradi wa Julius Nyerere         Na Josephine Maxime- Dar es Salaam            Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko ameagiza Mwanafunzi Mirabelle Msukari na Wenzake wa Shule ya Msingi Sun Rise iliyopo Wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam kupelekwa katika Mradi wa kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) ili kujifunza zaidi kwa Vitendo namna mradi huo unavyozalisha Umeme. Mheshimiwa Biteko amesema  hayo leo Februari 18 kwa njia ya simu baada ya Naibu Waziri wa Nishati Mheshimiwa Judith Kapinga  kutembelea shule hiyo kwa lengo la kumpongeza mwanafunzi huyo ambaye video yake ilijizolea umaarufu kupitia mitandao ya kijamii ambapo  Mirabelle alielezea kwa ufanisi juu ya miradi mbalimbali ya umeme inayotekelezwa nchini ukiwemo mradi wa Julius Nyerere. ‘’Sisi tukupongeze na tumefurahi kwa umri wako unafuatilia masuala ya Nishati, sasa tutakupeleka kuliona Bwawa la...