Posts

Showing posts from July, 2025

HII HAPA RATIBA YA UCHUKUAJI WA FOMU , ZOEZI LA KUWAPATA WADHAMINI NLD

Image
Chama Cha National League For Democracy (NLD) kimetangaza ratiba ya uchukuaji wa fomu,pamoja na zoezi la kupata wadhamini katika Makao Makuu ya Ofisi za Tume Huru ya Uchaguzi (INEC). Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa leo Julai 31,2025 Jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu wa Chama hicho Doyo Hassan Doyo,imebainisha kuwa zoezi hilo litaanza August,9,Mwaka huu.

MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU MAALUM UVCCM YAMEKAMILIKA

Image
Pichani ni Viongozi wa sekretariet ya Umoja wa Vijana CCM Wakikabidhi vifaa mbali mbali wezeshi Kwa ajili ushiriki wa mkutano mkuu wa maalum wa UVCCM  Mkutano mkuu maalum wa Uvccm unatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 1/08/2025 katika Ukumbi wa Jiji,Mtumba Jijini Dodoma  #MkutanoMkuuMaalumUVCCM #KazinaUtuTunasongaMbele #OktobaTunatiki✅

OFISI YA MSAJILI WA HAZINA 2025/26 KUKUSASANYA SHILL TRILL 2

Image
Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imejiwekea lengo la kukusanya kiasi cha Sh2 trilioni kama mapato yasiyo yakikodi katika mwaka wa fedha 2025/26, imebainishwa.     Hayo yalisemwa Jumatatu, Julai 28, 2025, na Msajili wa Hazina Bw. Nehemiah Mchechu wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi ya siku nne kwa wakuu wa taasisi za umma yaliyoandaliwa na OMH kwa kushirikiana na Taasisi ya Uongozi. Kiasi kinachotarajiwa kukusanywa ni zaidi ya lengo la Sh1.6 trilioni ambalo serikali iliiwekea Ofisi ya Msajili wa Hazina kukusanya mwaka huu wa fedha. “Ili tuweze kufikia lengo letu la kukusanya Sh2 trilioni itatubidi tuongeze bidii kwa asilimia 100 ya tulivyokuwa tunafanya mwaka wa fedha uliopita,” alisema Bw. Mchechu. Katika mwaka wa fedha uliopita (2024/25) Ofisi ya Msajili wa Hazina ilikusanya kiasi cha Sh1.028 trilioni kama mapato yasiyo yakikodi. Miongoni mwa vyanzo vikuu vya mapato yasiyo yakikodi ni Gawio---Mapato haya yanatokana na Mashirika na Taasisi zinazofanya biashara na yanaku...

KIGOGO MWENGINE CHADEMA ATIMKIA CHAUMMA

Image
  Na Mwandishi wetu Aliyekua Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA)Taifa, Sigrada Mligo, ametangaza kujiondoa rasmi ndani ya Chama hicho na kujiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kwa madai kuwa amechoshwa na kauli mbaya zinazotolewa dhidi yake. Uamuzi huo ameutoa  ikiwa ni miezi kadhaa baada ya kuripotiwa kujeruhiwa na mmoja wa walinzi wa Chadema wakati wa kikao cha ndani kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho John Heche March 25, 2025, mjini Njombe. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es Salaam katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama cha Chaumma Kinondoni amesema baadhi ya wanachama na viongozi wa Chama cha Chadema wamekuwa wakimtolea maneno na kumdhihaki kwa kumuita msaliti wa Chama licha ya kujitoa maisha yake yote. Mligo amesema kuwa ameumizwa na namna anavyotajwa kuwa chanzo cha migogoro, licha ya kuwa mmoja wa waliokibeba chama wakati wa kipindi kigumu, hivyo ametumia busara ya kuhama Chama cha Cha...

KATIBU MKUU NILD AHUDHURIA UZINDUZI WA RATIBA YA UCHAGUZI MKUU OCTOBER

Image
Katibu Mkuu wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, ameungana na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa nchini kushiriki hafla ya uzinduzi wa Ratiba ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Madiwani kwa upande wa Tanzania Bara, kwa mwaka 2025. Uzinduzi huo umefanyika leo, Julai 26, 2025, katika ofisi za Makao Makuu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), jijini Dodoma, na umeongozwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Jacobs Mwambegele. Tukio hili limeelezwa na viongozi mbalimbali kuwa ni hatua muhimu katika kuelekea uchaguzi mkuu ujao, na linaakisi dhamira ya Tume ya Uchaguzi kuhakikisha maandalizi ya uchaguzi yanatekelezwa kwa uwazi, ushirikishwaji na kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi. Akizungumza baada ya hafla hiyo, Katibu Mkuu wa NLD, Mhe. Doyo, alieleza kuwa chama chake kipo tayari kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Oktober mwaka huu. Alisema kuwa chama kimejipanga kusimamisha...

RAIS SAMIA KUZINDUA BANDARI KAVU YA KWALA NA UANZAJI RASMI WA TRENI YA MIZIGO YA SGR

Image
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (Mb), amesema kuwa hafla ya uzinduzi wa Bandari Kavu ya Kwala na kuanza rasmi kwa safari za treni ya mizigo ya reli ya kisasa (SGR) kati ya Dar es Salaam na Dodoma itafanyika Julai 31, 2025, Kwala, mkoani Pwani, ikihusisha pia upokeaji wa mabehewa mapya na yaliyokarabatiwa ya reli ya zamani (MGR) ambapo Mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Akizungumza na Wanahabari kwenye ukumbi wa TPA Jijini Dar es salaam leo tarehe 25 Julai,2025 Waziri Mbarawa amesema Bandari Kavu ya Kwala, iliyojengwa Vigwaza, kilomita 90 kutoka Dar es Salaam, ina uwezo wa kuhudumia makasha 823 kwa siku (takribani 339,500 kwa mwaka), sawa na asilimia 30 ya makasha yote ya Bandari ya Dar es salaam na kueleza kuwa eneo hilo lilichaguliwa kutokana na jiografia nzuri na ardhi ya serikali isiyo na migogoro. Ameongeza kuwa, treni ya mizigo ya SGR imeanza rasmi kutoa huduma kuanzia tarehe 27 Juni, 2025 baada ya majaribio kufanyika, a...

BODI YA TMA YAFANYA ZIARA YA KIKAZI RADA YA HALI YA HEWA BANGULO,PUGU NA KITUO CHA HALI YA HEWA JNIA

Image
Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imefanya ziara ya kikazi ya kukagua utendaji kazi wa Mamlaka katika kituo cha Rada ya Hali ya Hewa, Bangulo, Pugu na Ofisi za TMA zilizopo katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 23 Julai 2025.Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi Mhe. Jaji Mshibe Ali Bakari na Makamu Mwenyekiti, Dkt. Emmanuel Mpeta. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Jaji Mshibe alisema lengo la ziara ni kukagua  na kutathmini usimamzi na utendaji kazi wa miundombinu ya TMA  na kutathmini  utekelezaji wa Maagizo na Maelekezo ya Bodi katika kuboresha huduma na pia kutambua changamoto zilizopo,  na kuona Taasisi ilipo na inapoelekea. “Bodi imekuwa ikitoa maelekezo hivyo leo ilikuwa ni siku maalum kuangalia utekelezaji wake”.Alisema Jaji Mshibe. Alisisitiza kuwa TMA ya sasa imepiga hatua kubwa katika uboreshaji wa miundombinu ya utoaji huduma. Aidha, aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuiwezesh...

KATIBU MKUU CHAUMMA APOKEA MAPENDEKEZO YA SIFA, VIGEZO VYA WANAWAKE WATAKAOTEULIWA UCHAGUZI MKUU

Image
  Dar es Salaam  Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu amewataka wanawake kujitokeza kuzigombea nafasi mbalimbali za uongozi katika Uchaguzi mkuu kwani moja ya kigezo kitakachotumika kumpata kiongozi wa kiti maalum ni mchango wake wa kura kwa chama kwenye Uchaguzi mkuu. Rai hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati alipokua akipokea mwongozo rasmi wenye mapendekezo ya sifa na vigezo vya wanawake wa chama hicho wanaotarajiwa kuteuliwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi kupitia udiwani, ubunge na uwakilishi wa viti maalum katika uchaguzi  wa mwaka huu. Amesema kuwa, hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa chama kuhakikisha wanawake wanashirikishwa kikamilifu katika uongozi, sambamba na kuzingatia uwiano wa kijinsia kama ilivyoainishwa kwenye katiba ya chama na miongozo ya kitaifa. Awali, Katibu wa Kamati Maalum ya Viti Maalum, Moza Ally amesema kuwa katika utengenezaji wa mwongozo huo wamezingatia sheria za uhaguzi,  chama na Katiba ya Nchi ili...

RC CHALAMILA ASIKITISHWA NA HUDUMA MBOVU YA MABASI YAENDAYO HARAKA-DART

Image
Asema Serikali sikivu ya Rais Dkt Samia Suluhu imesikia kilio hicho mwarobaini tayari umepatikana. Mku wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amefanya ziara katika Kituo cha mabasi yaendayo haraka DART kilichopo Kimara mwisho Wilaya ya Ubungo na kuitaka mamlaka inayosimamia mabasi yaendayo haraka UDART kuboresha huduma zao ili kumaliza adha wanayopitia wananchi wanaotumia usafiri huo. Akizungumza wakati wa ziara hiyo RC Chalamila amesema hajaridhishwa na huduma ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka kutokana na uchache wa mabasi jambo ambalo limekua likichangia huduma mbovu na kuwasababishia watumiaji wa usafiri huo adha kubwa  kinyume na dhamira ya Rais Dkt Samia ya kutaka kuboresha huduma yq usafiri katika Jiji hilo,hivyo ameitaka UDART kuboreha huduma. Aidha RC Chalamila ametembelea upanuzi wa barabara ya Ubungo Kimara unaosimamiwa na TANROAD ambapo ameitaka mamlaka hiyo kumsimamia mkandarasi amalize ujenzi huo kwa wakati pia ameshauri uwepo wa huduma za vyoo kwenye maeneo ya v...

Huu hapa utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24, zijazo, leo Julai 24,2025

Image
 Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo 

BENKI YA EQUITY NA SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA MIFUGO NA NGOZI NCHINI

Image
  Dodoma – 24 Julai 2025 Benki ya Equity kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanzisha mpango mahsusi wa kuimarisha sekta ya Mifugo na Ngozi nchini, kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao ya Mifugo, kupanua masoko na kuinua maisha ya wafugaji. Akizungumza katika kikao cha wadau wa sekta ya mifugo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Edwin Mhede, alisema serikali imeitaka Benki ya Equity na Bodi yake kushirikiana na serikali kuunda timu maalum ya kitaalamu itakayosimamia uwekezaji katika sekta ya Mifugo. “Hatua hii inalenga kuboresha ufugaji na mifumo ya uzalishaji wa ngozi, kuongeza ubora na kuifanya sekta hii kuwa chanzo kikuu cha mapato kwa wafugaji,” alisema Dk. Mhede. Aliongeza pia ili kuboresha Sekta ya Mifugo nchini, hasa kupambana na Magonjwa, Serikali tayari inaendesha kampeni ya kuchanja mifugo yote nchini, ambapo mpaka sasa imechanja zaidi ya mifugo milioni 16, na zoezi hili linatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba mwaka huu, ili kuhakikisha mazao...

MIKANDA NANE YA KIMATAIFA KUWANIWA JULAI 26, KNOCKOUT YA MAMA

Image
  Na Mwandishi wetu, Dar  Pambano kubwa la Knockout ya mama msimu wa tano inatarajia kuwakutanisha mabondia wenye viwango vikubwa nchini Tanzania, Julai 26, 2025 katika  Viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Pambano hilo kubwa litaweka historia kwa kuwa na mapambano nane ya kuwania mikanda mikubwa ya kimataifa ikiwemo ya WBO na WBC. Akizungumza na waandishi wa habari  Julai 24, 2025 jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Matangazo na Uzalishaji kutoka Kampuni ya Mafia Promotion Omari Clayton, amesema pambano hilo litakuwa na jumla ya mapambano 10 yakihusisha mabondia wa kimataifa. "Mapambano nane yatakuwa ya mikanda na lengo ni kufanya "boxing" ya Tanzania iende mbali kimataifa, bondia atakayeshinda atapata fedha, mkanda na nyota, hivyo kutambulika kimataifa," amesema Clayton. Ameongeza siku hiyo ya pambano itakuwa ni siku ya mtoko kwamba wanataka kila Mtanzania aweze kuifanya Julai 26, 2025 kuwa siku ya Mtoko kwa kwenda kushuhudia pambano hilo. Naye, Mkur...

BENKI YA DUNIA KUJENGA MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA KV 400 KUTOKA UGANDA HADI TANZANIA

Image
Yakutana na Mhandisi Mramba kueleza uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hauna athari kimazingira Yaialika Wizara ya Nishati kushiriki Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa jijini New York Mramba aahidi kuendelea kushirikiana na Benki ya Dunia utekelezaji miradi ya Nishati Benki ya Dunia (WB) imeeleza kuwa itatoa fedha za utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha  umeme wa msongo mkubwa wa kilovolti 400 kutoka nchini Uganda hadi Tanzania. Hayo, yameelezwa na Mtaalam wa Nishati kutoka Ofisi ya Benki ya Dunia nchini Tanzania, Dkt. Rhonda Jordan wakati alipofanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mha. Felchesmi Mramba katika Ofisi za Wizara ya Nishati Mji wa Serikali Mtumba Julai, 23 Jijini Dodoma. Dkt. Rhonda amesema kuwa kwa sasa benki hiyo imeridhia kutekeleza mradi huo baada ya kujiridhisha kuwa hauna athari za kimazingira kama ilivyokuwa ikielezwa hapo awali. “Bodi ya Wakurugenzi sasa itapitisha fedha kwa ajili ya kuanza kutekeleza mradi huo, ambao ulikuwa uk...

DKT. BITEKO AHANI MSIBA WA MZEE MGANGA NGELEJA

Image
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ahani msiba wa Baba Mzazi wa William Ngeleja, Mzee Mganga Ngeleja aliyefariki Julai, 16, 2025 na kuzikwa jana (Julai 21, 2025) Kijijini kwake Bitoto, Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza

RAIS SAMIA ATOA BILIONI NNE UJENZI KIWANDA CHA KUZALISHA NISHATI MBADALA

Image
Kiwanda kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati safi nchini REA kugharamia ununuzi wa mtambo wa STAMICO Stamico yapania kusambaza Nishati Safi ya Rafiki Briquettes kila kona Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na Shirika la Taifa la Madini (STAMICO) leo tarehe 22 Julai, 2025 wamesaini mkataba wenye lengo la kujenga kiwanda kipya cha kuzalisha nishati mbadala (Mkaa mbadala wa Rafiki Briquettes) mkoani Geita ambapo mkataba huo una thamani ya shilingi bilioni 4.5. Katika hafla iliyofanyika katika Ofisi ndogo ya REA, Jijini, Dar es Salaam, REA itatoa jumla ya shilingi bilioni tatu na STAMICO itatoa shilingi bilioni 1.5; kwa mchanganuo huo, REA itagharamia ununuzi wa mtambo wakati STAMICO italipia upatikanaji wa kiwanja, ujenzi wa jengo la kiwanda na gharama za ufungaji wa mitambo.  Mkataba huo umesainiwa na Mhandisi, Hassan Saidy, Mkurugenzi Mkuu wa REA pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dkt. Venance Mwasse. Mkataba huo utaifanya STAMICO kuwa na viwand...