Posts

Showing posts from September, 2025

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

“NCHI YENYE MADINI YA KIPEKEE, KUWA NA WANANCHI MASIKINI NI AIBU” DOYO

Image
  Mwanza, Geita Buseresere  Mgombea urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, akiendelea na kampeni zake Kanda ya Ziwa, amefanya mikutano ya hadhara katika Jimbo la Sengerema, eneo la Stendi ya Zamani, na Kata ya Buseresere, Mkoa wa Geita. Katika hotuba yake, Mhe. Doyo aliwataka wananchi wa Kanda ya Ziwa kutafakari kwa kina juu ya sababu zinazowafanya kuendelea kukosa maendeleo licha ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kushika dola kwa zaidi ya miaka 60. Mhe. Doyo aliwaahidi wananchi kuwa endapo watampa ridhaa ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atahakikisha wakulima wanapata fursa ya kuuza mazao yao katika masoko yenye tija na faida, badala ya kulazimishwa kuuza katika masoko yanayowanyonya na kuendeleza umaskini.  “Wananchi, mkiniamini na kunipa kura Oktoba 29, nitasimamia na kuhakikisha wakulima wanapata bei nzuri na zenye motisha kwenye mazao yenu yote. Haiwezekani mtumie gharama kubwa katika kilimo chenu halafu mpangiwe bei, hizi ni mbinu za kuendelez...

REA YAUZA MAJIKO 1500 KWA BEI YA RUZUKU MAONYESHO YA MADINI GEITA

Image
REA yauza majiko 1,500 kwa bei ya ruzuku kwenye maonesho ya Madini Geita REA yapongezwa kwa kuuza majiko kwa bei ya ruzuku na kutoa elimu ya miradi ya wakala Geita Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita yamehitimishwa rasmi na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambayo yalifunguliwa Septemba 18 na kufikia kilele tarehe 28 Septemba, 2025 Wakala umeshiriki maonesho hayo kwa kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia, kutoa elimu ya miradi inayotekelezwa na wakala wa nishati vijijini pamoja na fursa zinazopatikana kwa wakala kama vile vituo vidogo vya mafuta. Sambamba na hayo Wakala unahamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuuza kwa ruzuku mitungi ya gesi ya kilo 6 ambayo inauzwa kwa bei ya 50% ambayo ni kiasi cha shilingi 17,500 ambapo jumla ya mitungi 5,00 imeuzwa kwa ruzuku kwenye maonesho. Pamoja na hayo, Wakala unafadhili uuzwaji wa majiko banifu yanayotumia mkaa mbadala pamoja na mkaa wa kawaida, majiko hayo yameuzwa kwa be...

WASIRA AWANYOOSHEA KIDOLE WANAOJIPANGA KWA UMEYA, UENYEKITI WA HALMASHAURI BADALA KUSAKA USHINDI WA. CCM

Image
Na Mwandishi Wetu, Mkinga MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amewaonya baadhi ya wagombea udiwani katika maeneo mbalimbali ambao wameanza harakati za kusaka uenyekiti wa halmashauri na umeya, kabla ya uchaguzi. Amesema wanachotakiwa kufanya wana CCM wote kwa sasa ni kuhakikisha wanasaka kura za kishindo kwa Chama hususan za mgombea urais Dk. Samia Suluhu Hassan. Amesema hayo leo Septemba 25, 2025 alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM katika kikao cha ndani kilichofanyika wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga, jana. Kikao hicho ni mfululizo wa vikao anavyoviendesha kwa kukutana na viongozi na wana CCM kumwombea kura Dk. Samia, wagombea ubunge na udiwani waliosimamishwa na Chama kwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu. "Kwa madiwani ninawaomba sana sio hapa Mkinga, hapa sijaambiwa lakini huko nilikotoka madiwani wameanza kutafuta mwenyekiti wa halmashauri na huku wao wenyewe hawajachaguliwa, sasa wewe utajuaje kama utachaguliwa wew...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO, LEO SEPT 24,2025

Image
 

SERIKALI YAONDOA VAT KWA VITUO VYA GESI ASILIA ILIYOSHINDILIWA (CNG)

Image
Lengo ni kuongeza uwanda wa  matumizi ya CNG katika vyombo vya moto nchini Mhandisi Mramba azindua kituo cha Gesi Asilia iliyoshindiliwa ( CNG) cha PUMA Energy Asema vifaa vya kuwekea mifumo  ya gesi  kwenye vyombo vya moto pia imeondolewa Apongeza PUMA Energy kwa kuiunga mkono Serikali katika ujenzi wa vituo vya CNG Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema  Serikali imeondoa kodi ya ongezeko la thamani  (VAT) kwa vituo vyote vya Gesi iliyoshindiliwa (CNG) nchini  ili kuhamasisha matumizi ya gesi asilia  kwenye vyombo vya moto kupitia uwepo wa vituo vingi vya kutoa huduma hiyo kwa wananchi.  Amesema kuwa Serikali pia imeondoa kodi kwenye vifaa vya kuwekea mifumo hiyo ya gesi  kwenye vyombo vya moto kama vile magari na bajaji ikiwa ni hatua pia ya kuhamasisha matumizi ya gesi asilia katika vyombo vya moto. Mhandisi Mramba ameeleza hayo leo Septemba 24, 2025 jijini Dar es Salaam wakati  akizindua kituo cha Gesi Asili...

WASIRA: TUTAENDELEA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA WATANZANIA

Image
  Na Mwandishi Wetu,  Kisarawe CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kitaendelea kulinda amani, umoja na mshikamano kwa kuwa bado hakijakamilisha lengo la kuwatumikia Watanzania na kuwaletea maendeleo makubwa zaidi. CCM imesema jukumu la kulinda amani umoja, mshikamano na kuleta maendeleo makubwa ya Tanzania imelirithi kutoka kwa vyama vya ukombozi Tanu na Afro Shiraz, hivyo itaendelea kulilinda kwa wivu mkubwa. Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,  Stephen Wasira alieleza hayo jana, Kisarawe mkoani Pwani alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM Mkoa wa Pwani akiwa katika ziara ya kumwombea kura mgombea urais wa CCM Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea ubunge na udiwani waliosimamishwa na Chama kwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu. "CCM imekabidhiwa jukumu la kuendeleza umoja, mtu akijaribu kuvunja umoja anavunja msingi tuliokabidhiwa, CCM hatuwezi kuwa miongoni mwa wale wanaounga mkono wanaotaka kuvunja umoja wa nchi, ni kazi tulikabidhiwa, ya his...

DOYO: AHIDI KUSITISHA MIKATABA YA MADINI YENYE HARUFU YA UFISADI

Image
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, akiwa mkoani Mara, wilaya ya Tarime, amewahakikishia wananchi kuwa endapo atachaguliwa kuwa Rais, atasitisha mikataba yote ya madini na kuipitia upya. Mhe. Doyo amesema kuwa iwapo itabainika mikataba hiyo imeingiwa kwa njia ya rushwa au ufisadi, serikali yake itaiondoa na kuanzisha mikataba mipya yenye kuzingatia maslahi ya taifa. Aidha, ameongeza kuwa wananchi wazawa wa Tarime watapewa kipaumbele cha kwanza katika uwekezaji wa madini ili kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha Watanzania wenyewe. Akiwa Nyamongo, mkoa wa mara Mhe. Doyo alisisitiza kuwa haiwezekani eneo lenye mgodi mkubwa kama huo likakosa huduma bora za kijamii huku wageni wakiendelea kumiliki utajiri wa taifa. Alitolea mfano wa Saudi Arabia, akieleza jinsi wananchi wa nchi hiyo wanavyonufaika na huduma bora kutokana na mapato ya mafuta, na akasema wananchi wa Nyamongo hawapaswi kubaki wakitegemea kuendesha bodaboda pe...

NISHATI SAFI INATEKELEZWA KWA VITENDO GEITA

Image
Chereko yatajwa na wananchi Banda la REA Majiko ya gesi na majiko banifu yanauzwa kwa bei ya ruzuku Wananchi wakiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kununua majiko ya gesi na majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini  mkoani Geita.  Maonesho hayo yamefunguliwa  rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.

KATIBU MKUU MRAMBA AKUTANA NA KAMPUNI YA NYUKLIA YA CHINA

Image
Wajadili ushirikiano katika kuzalisha umeme wa nyuklia nchini Watanzania kujengewa uwezo  katika masuala ya nyuklia Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba ameongoza ujumbe wa Serikali ya  Tanzania katika kikao na Shirika la Taifa la Nyuklia la China (China National Nuclear Corporation – CNNC), kujadili fursa za ushirikiano  katika kuanzisha na kuendeleza mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia teknolojia ya nyuklia. Katika kikao kilichofanyika jijini Vienna, Austria pembezoni mwa Mkutano Mkuu wa 69 Wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomi (IAEA), Wawakilishi wa CNNC waliieleza Tanzania kuwa kampuni hiyo ina uzoefu mkubwa katika kujenga na kuendesha mitambo ya kuzalisha umeme wa nyuklia, na wako tayari kushirikiana na Tanzania katika hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya aina hiyo. “Tanzania imeanza maandalizi ya kuzalisha umeme kwa kutumia nyuklia ikiwa ni utekelezaji wa dhamira na nia njema ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya ...

WATUMISHI WIZARA YA NISHATI WAPATIWA ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Image
Ni baada ya Dkt.Biteko kuwakabidhi  majiko yanayotumia umeme kidogo (Induction Cookers). Yaelezwa kuwa majiko hayo yanatumia umeme kidogo kwa gharama ndogo Watumishi wa Wizara ya Nishati leo wamepata  elimu ya matumizi bora na sahihi ya majiko yanayotumia umeme kidogo  ( Induction cookers) baada ya kukabidhiwa majiko hayo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko hivi karibuni. Dkt. Biteko aliwakabidhi majiko hayo Watumishi wa Wizara ya Nishati ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na kwa kutambua kuwa Watumishi hao ni mabalozi katika utoaji wa elimu ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi. Mafunzo hayo ambayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati- Mtumba,  Dodoma yameandaliwa na Kitengo cha Nishati safi ya kupikia kwa kushirikiana na wataalam kutoka Kampuni ya Positive Cooker. Akitoa elimu ya matumizi bora na sahihi ya majiko hayo,  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni  ya Positiv...

CCM TUMEDHAMIRIA KUENDELEA KULETA MABADILIKO KATIKA MAENDELEO YA WATANZANIA

Image
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema Chama kinafanya kazi kubwa ya kuleta mabadiliko ili kuwaletea maendeleo wananchi. Aidha, amesisitiza wananchi wandelee kukiamini na kukipa nafasi Chama kiendelee kudumisha amani kwa kuwa maendeleo hayatapatikana iwapo itatoweka. Wasira alieleza hayo alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM kutoka Jimbo la Mbeya Vijijini, akiwa katika ziara ya kumwombea kura mgombea urais wa CCM Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wa ubunge na udiwani mkoani Mbeya, jana. Alitumia mkutano huo kumwombea kura Dk. Samia, wagombea ubunge na udiwani waliosimamishwa kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu. "Kazi yetu ni kuleta mabadiliko katika maisha ya watu, maendeleo ni mabadiliko katika maisha ya watu, ukitengeneza barabara unamwezesha huyu mtu aweze kufikisha bidhaa zake sokoni kwa hiyo ataongeza kilimo na uchumi wake utaongezeka kwa sababu ana mahali pakuuza. ...

SERIKALI YA AUSTRIA KUFADHILI MIRADI YA UMEME TANZANIA

Image
  Ni inayozalisha umeme kutokana na Jua; Takataka Ufadhili huo ni kupitia Benki ya UniCredit ya Austria Serikali ya Tanzania yaahidi ushirikiano Serikali ya Austria kupitia Benki ya UniCredit  imeahidi kuipatia fedha Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kiasi cha Euro Milioni 20 sawa na takribani Shilingi bilioni 60 kwa ajili ya Utekelezaji wa miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia jua na takataka. Hayo yamesemwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Merl Solar Technologies GmbH, Mha. Hannnes Merl alipofanya mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba Septemba 17, 2025 pembeni ya  Mkutano Mkuu wa 69 wa Shirika la Kimataifa la nguvu za Atomic unaoendela Jijini Vienna, Austria. Ili kuanza utekelezaji wa miradi hiyo, Mhandisi Mramba  ameikaribisha kampuni hiyo nchini Tanzania ili kukutana na wataalam na kuanza  kufanya maandilizi stahiki ya miradi hiyo mipya ya kuzalisha umeme  huku akiahidi kutoa ushirikiano katika kufanikisha Ute...

NITALIPIA UPYA MIKATABA YA MADINI ILI WANANCHI WANUFAIKE - DOYO

Image
Monduli, Arusha Mgombea urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, ameendelea na ziara zake za kampeni zinazofanyika kwa mfumo wa kufikia na kuwafata wapiga kura popote walipo, kwa mtindo wa kampeni za kijiji kwa kijiji na kata kwa kata. Akiwa njiani kuelekea Arusha, Mhe. Doyo alipita Kata ya Makuyuni, lakini pia alizungumza na wananchi wa Kata ya Meserani, Wilaya ya Monduli. Katika hotuba yake, aliwaeleza wananchi kuwa mikataba ya madini iliyosainiwa na serikali ya Chama cha Mapinduzi imekuwa ikifanyika kwa usiri mkubwa, bila Watanzania kuonyeshwa manufaa wanayoyapata kutokana na mikataba hiyo. Mhe. Doyo aliahidi kuwa, endapo atachaguliwa kuwa Rais, hatua yake ya kwanza itakuwa ni kuhakikisha anapitia upya mikataba ya madini ili kubaini kwa uwazi kile ambacho taifa linanufaika nacho. Alisisitiza kuwa suala hilo limekuwa siri kwa muda mrefu, jambo ambalo atalivalia njuga ili kuhakikisha rasilimali za Watanzania zinabaki salama na zenye manufaa kwa wananchi. Aidha, aliwaambia w...

MTAMBO WA GESI ASILIA WASAFIRISHWA KWENDA MTWARA KUONGEZA NGUVU YA UZALISHAJI WA UMEME

Image
  Na Agnes Njaala, Dar es Salaam Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika katika mikoa ya Mtwara na Lindi, ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya matumizi ya umeme kutokana na ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii.  Hayo yanathibitishwa na hatua zilizochukuliwa na Shirika hilo Kusafirisha mtambo  wa Kuzalisha Umeme kwa Gesi Asilia  megawati 20 unaojulikana kitaalamu kwa jina la TM 2500 kutoka kituo cha Ubungo III jijini Dar es Salaam kwenda Mtwara. Akizungumza Septemba 11, 2025 wakati wa zoezi la usafirishaji, Mhandisi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme Mtwara II, Godfrey Matiko, alisema mtambo huo una uwezo wa kuzalisha Megawati 20, na utaunganishwa na mtambo mwingine uliopo ambao tayari unazalisha Megawati 20 na hivyo kuongeza jumla ya uzalishaji kufikia Megawati 40 kwenye Kituo cha Uzalishaji Umeme kwa Gesi Asilia kilichopo eneo la Hiyari mkoani humo.  Amesema, Umeme huo utasamba...

MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAONGEZEKA NCHINI

Image
Mhandisi Mramba asema yamefikia asilimia 20.3  kutoka asilimia 6.9 ya mwaka 2021 Lengo ni kufikia asilimia 80 ifikapo 2034 Apongeza juhudi za Rais Samia katika kuwezesha upatikanaji wa nishati safi, salama na nafuu kwa Watanzania Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha.Felchesmi Mramba ameeleza kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia nchinj yameongezeka kutoka asilimia  6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 20.3 huku lengo likiwa ni kufikia asilimia 80 ndani ya miaka 10, ambapo hadi sasa imebakia miaka 9. Mha. Mramba ameyasema hayo Septemba 12, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizindua Kongamano la  Nishati Safi ya Kupikia lililoandaliwa na kampuni ya Mwananchi kwa ushirikiano  na Wizara ya Nishati pamoja na wadau mbalimbali likibebwa na kaulimbiu ya  ‘Nishati safi ya Kupikia Okoa Maisha, Linda Mazingira. Akizungumza  wakati wa uzinduzi huo, Mha. Mramba amesema  “Nishati Safi ya Kupikia siyo jambo la kinadharia bali ni jambo linalohusu maisha, mazingira na uchu...

MHANDISI MRAMBA, JICA WAJADILI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA NISHATI

Image
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amekutana na Wataalam kutoka Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) ili kujadili hali ya utekelezaji wa miradi ya Nishati inayofadhiliwa na shirika hilo kwa lengo la kuhakikisha kuwa miradi hiyo inatekelezwa kwa wakati na kwa ufanisi. Kikao hicho kimefanyika tarehe 8 Septemba 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati Mtumba Jijini Dodoma ambapo pande hizo mbili pia zilijadiliana kuhusu suala la kujengea uwezo wataalam wa Wizara ya Nishati, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) katika masuala ya kusanifu mitandao ya usambazaji wa Gesi Asilia. Miradi iliyojadiliwa kwa kina katika kikao hicho ni wa kusafirisha umeme kutoka Tanzania hadi Uganda (UTIP) na mradi wa umeme Dodoma Ring Circuit unaolenga kuzidi kuimarisha hali ya upatikanaji umeme Dodoma. Katika kikao hicho, Mramba ameisisitiza JICA kuhusu suala la utekelezaji mradi wa mfano wa usambazaji gesi asilia katik...

DOYO KUONDOA SHERIA KANDAMIZI YA KIKOKOTOO

Image
Handeni, Tanga Mgombea Urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, amehutubia mamia ya wananchi katika viwanja vya Soko la Zamani, Handeni Mjini. Katika hotuba yake, Mhe. Doyo aliwataka wananchi wa Handeni kutafakari kwa kina changamoto mbalimbali zinazowakabili, ikiwemo tatizo la maji ambalo limekuwa sugu kwa muda mrefu. Mhe. Doyo alisema: "Tatizo la maji Handeni limekuwepo tangu nikiwa mdogo hadi leo. Chanzo cha maji kiko umbali wa kilometa 50 kutoka Mswaha, lakini maji hayo yamekuwa yakipita hapa Handeni na kuelekea Pangani, kwa sababu tu Waziri wa Maji anatokea Pangani. Hili si jambo la bahati mbaya. Wanahandeni wanapaswa waamke na kuelewa kuwa baadhi ya viongozi siku zote hubeba maslahi yao binafsi. Ukosefu wa maji Handeni si kwa bahati mbaya, bali ni kwa sababu ya kukosa utashi wa kisiasa. Nawaomba mnichague ili twende tukatatue changamoto hii. Wananchi wa Handeni wanahitaji maji kwa haraka na si ahadi tena." Aidha, Mhe. Doyo aliwahakikishia wananchi kuwa iwapo ...

TMA YATOA UTABIRI WA MVUA ZA VULI OCTOBER HADI DISEMBA

Image
Na Mwandishi wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za Vuli kwa kipindi cha Oktoba hadi Desemba 2025, ikionya kuwa mvua zinatarajiwa kuwa za Wastani hadi Chini ya Wastani katika maeneo mengi ya nchi, huku baadhi ya maeneo machache yakitarajiwa kupata mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa (IPCC), ametoa taarifa hiyo leo Septemba 11, 2025 wakati akitangaza utabiri huo kwa waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam, katika ukumbi wa Ubungo Plaza. "Vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko usioridhisha wa mvua vinatarajiwa kutawala hasa katika pwani ya kaskazini na nyanda za juu kaskazini mashariki," amesema Dkt. Chang’a. Dkt. Chang’a amesema mvua zinatarajiwa kuanza wiki ya kwanza na ya pili ya Oktoba katika mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Mara na kaskazini mwa Kigoma, kabla ya kusambaa kati...

TATHMINI YA MCHANGO WA WANAHABARI YAONESHA KURIDHISHWA NA USAHIHI WA UTABIRI WA HALI YA HEWA

Image
MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekutana na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini ili kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Vuli (Oktoba – Desemba) 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Usafirishaji (NIT). Akizungumza wakati wa mkutano huo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema kupitia warsha hizi uelewa wa wanahabari kuhusu masuala ya hali ya hewa umeendelea kuimarishwa kwa kiasi kikubwa na hivyo kuwezesha taarifa zitolewazo na mamlaka kufikia jamii kwa urahisi na kwa wakati. “Mnamo mwezi Julai mwaka 2025, Mamlaka iliandaa Dodoso maalumu kwa wanahabari ili kufanya tathmini ya utendaji kazi wake kwa Tasnia ya Habari, ambapo kwa taarifa niliyonayo ni kwamba tathmini hiyo imekamilika na matokeo yake yanaonesha asilimia 95 ya wanahabari waliotoa maoni yao wameridhishwa na usahihi wa utabiri wetu na asilimia 96.3 wameonesha kuzielewa taarifa hiz...

MWENYEKITI WA NLD ARUDISHA FOMU YA KUGOMBEA URAIS ZANZNIBAR

Image
MWENYEKITI wa Chama cha NLD na mgombea urais wa Zanzibar, Mhe. Mfaume Khamis Hassan, leo amerejesha fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya urais wa Zanzibar. Hafla ya kurejesha fomu hizo imefanyika mbele ya Tume Huru ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), ambapo viongozi, wanachama na wafuasi wa chama hicho walihudhuria kwa wingi. Katika hotuba yake fupi baada ya kurejesha fomu, Mhe. Khamis Hassan alisisitiza dhamira yake ya kuleta mabadiliko chanya Zanzibar endapo atapata ridhaa ya wananchi. Alibainisha kuwa vipaumbele vyake vikuu vitahusisha kukuza uchumi wa visiwa kwa kuimarisha sekta ya utalii na biashara ndogondogo, kuboresha huduma za afya na elimu, pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa vijana. Aidha, aliahidi kuendeleza mshikamano wa kitaifa kwa kuhakikisha kila raia anashirikishwa katika mchakato wa maamuzi ya kitaifa, bila kujali itikadi za kisiasa. Kwa mujibu wa chama cha NLD, sera zake zinalenga kuijenga Zanzibar yenye mshikamano, amani, na ustawi wa kijamii na kiuchumi. Zanzib...

DOYO, NITAFUNGUA MASOKO UA NJE KWA WAKULIMA WA LUSHOTO

Image
Na Mwandishi Wetu Lushoto, Tanga Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha NLD, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mhe. Hassan Doyo, ameendelea na kampeni zake kwa kunadi sera za chama katika eneo la Lukozi, wilayani Lushoto. Katika mkutano huo uliovuta idadi kubwa ya wafanyabiashara wa mboga mboga, Mhe. Doyo alibainisha changamoto kubwa inayowakabili wafanyabiashara hao kuwa ni ukosefu wa masoko ya uhakika. Alieleza kuwa iwapo biashara hiyo itaandaliwa kwa ubora na ustadi, inaweza kuwanufaisha wananchi na familia zao kiuchumi. “Mazao haya ya mbogamboga yana soko kubwa hata nje ya nchi, lakini tatizo ni kwamba hatujaandaliwa mazingira mazuri ya kibiashara. Kwa sasa mazao yote yanategemea soko moja la Dar es Salaam, na huko nako madalali huwanyonya wakulima. Mkinipa ridhaa, nitahakikisha tunawatafutia masoko ya nje ya nchi. Tutawaleta wanunuzi wakubwa, watasindika mazao yenu na kusafirisha kimataifa. Jiografia ya Lushoto inaruhusu biashara ya mazao haya k...

TMA YAHIMIZWA KUENDELEA KUSHIRIKISHA WADAU ILI KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA HALI YA HEWA

Image
Dodoma Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imehimizwa kuendelea kushirikisha wadau kutoka sekta mbalimbali ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa nchini. Mgeni rasmi na Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Mhe. Jaji Mshibe Ali Bakari alisema hayo wakati akifungua mkutano wa 24 wa wadau katika kujadili Utabiri wa Msimu wa Mvua za Vuli (Oktoba hadi Disemba) 2025, wenye kaulimbiu “matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa katika kupanga na kutekeleza majukumu ya kila siku kwa maendeleo endelevu” uliofanyika kwenye ukumbi wa PSSSF, jijini Dodoma, tarehe 08/09/2025. “Tunapoelekea kutoa Utabiri wa Mvua za Vuli (Oktoba hadi Disemba), 2025 napenda kuipongeza TMA na kuwahimiza kuendeleza utaratibu huu wa kuwashirikisha wadau kutoka sekta mbalimbali katika hatua za maandalizi ya utoaji wa utabiri wa mvua za misimu hapa nchini. Ushirikiano huu ni mfano wa kuigwa na unafaa kuendelezwa hasa katika kipindi hiki ambacho Dunia inakabiliwa na changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa.” Alisem...

MAKUYUNI WILDLIFE PARK YAZIDI KUWAVUTIA WAGENI WA KIMATAIFA

Image
Na Mwandishi wetu, Arusha Hifadhi ya Makuyuni Wildlife Park iliyo chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA inaendelea kujidhihirisha kama lulu mpya ya utalii nchini  hususani katika ukanda wa kaskazini, ikiwavutia wageni wa ndani na nje ya nchi kwa mandhari yake ya kipekee na utajiri wa wingi wa idadi na spishi mbalimbali za wanyamapori. Leo Septemba 8, 2025 hifadhi hiyo imepokea tena kundi la wageni wa kimataifa kutoka mataifa mbalimbali kupitia kampuni maarufu ya utalii, Ranger Safaris & Tours, yenye makao yake jijini Arusha. Zaidi ya wageni 20 kutoka Denmark, Australia na New Zealand wametembelea hifadhi hiyo na kueleza kufurahishwa kwao na mandhari ya kipekee, urithi wa kiasili na vivutio adimu vinavyopatikana hifadhini humo. Aidha,  Wageni hao wameeleza kuridhishwa na ubora wa Makuyuni Wildlife Park na baadhi yao wakaahidi kurejea tena Novemba mwaka huu kwa ziara ya pili. Wakizungumza mara baada ya kutembelea hifadhi na kujionea vivuti...