Posts

Showing posts from August, 2025

DKT.BITEKO AZINDUA MRADI UTAKAOWAKWAMUA VIJANA KIUCHUMI KATIKA MAENEO YANAYOPITIWA NA BOMBA LA MAFUTA GHAFI (EACOP)

Image
Unahusisha kuongezea vijana ujuzi, kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha, na kuondoa vikwazo vya ujasiriamali na ajira binafsi Ataka ujuzi unaotolewa kwa vijana uende sambamba na utoaji wa mitaji Awaasa Vijana kuchangamkia fursa na kuwa waaminifu wanapopata nafasi  Wanawake 6,130, Wanaume 4,905 na Makundi maalum 1,226 kufikiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko leo amezindua  Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE) ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) ikiwa ni jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali katika kuhakikisha kuwa jamii zilizo karibu na miradi zinanufaika na miradi hiyo. Akizindua mradi huo katika  Kijiji cha Bukombe, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita tarehe 18 Agosti 2025, Dkt. Biteko amesema mradi huo wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi ni moja ya miradi iliyopangwa kuwezeshwa na Kampuni ya EACOP kwa kipindi cha ujenzi na baada ya ujenzi ikiwa ni sehemu ya Uwajibikaj...

KANIKI ACHUKUA FOMU

Image
Picha mbalimbali za matukio wakati Mgombea udiwani Kata ya Zingiziwa Selemani kaniki akielekea kuchukua fomu Mgombea udiwani wa Chama cha Mapinduzi CCM Kata ya  Zingiziwa Wilayani Ilala Selemani Kaniki leo Agosti 18/2025 amechukua fomu ya kugombea Udiwani wa kata ya Zingiziwa ambapo Pichani alisindikizwa na viongozi wa chama wa kata hiyo pamoja na viongozi wa kata 

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA, WAPEWA SOMO NA JAJI MUTUNGI

Image
  Na Mwandishi wetu Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, amevitaka vyama vya siasa nchini kujiepusha na lugha za matusi, kashfa, uchochezi au vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga amani na utulivu wa taifa la Tanzania hasa kuelekea uchaguzi Mkuu. Wito huo ameutoa jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi kwa viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa ambapo amesisitiza kuwa vyama vya siasa vina wajibu wa kuendeleza misingi ya amani na mshikamano wa taifa. Amesema kuwa, viongozi wa vyama vya siasa nchini ni vyema kuhakikisha kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 zinafanyika kwa kistaarabu, bila kutumia lugha za matusi, kashfa au vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha tunu ya amani Taifa iliyopo. "Nendeni mkafanye kampeni za kistaarabu mkiwanadi wagombea wenu, kuweni na lugha nzuri za kuzungumza, epukeni matusi, lugha za kashfa, kwani amani ya taifa hili ni muhimu kuliko chochote"mesema Jaji Mutungi. Ameongeza kuwa, amani na mshika...

TUKITUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA TUTAOKOA HEKTA 400,000 ZA MISITU ZINAZOTEKETEA KWA MWAKA-MJIOLOJIA NSAJIGWA

Image
Awanoa Wanawawake na Wajasiriamali Songwe kuhusu Nishati Safi ya Kupikia Atoa wito kwa Wadau kushirikiana na Wizara ya Nishati kutoa elimu ya Nishati Safi ya Kupikia Songwe Imeelezwa  kuwa matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia si tu yanahatarisha afya bali pia yanachochea uharibifu wa mazingira ambapo takribani hekta 400,000 za misitu hupotea kila mwaka nchini kutokana na ukataji wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa, jambo linalochangia kuongezeka kwa ukame na mabadiliko ya tabianchi. Hivyo, Watanzania wameaswa kuhamia katika  matumizi ya nishati safi ya kupikia na kuachana na matumizi ya nishati isiyo safi kama kuni na mkaa kutokana na athari zake kwa binadamu na mazingira. Wito huo umetolewa leo Agosti 16, 2025, na Mjiolojia kutoka Wizara ya Nishati, Nsajigwa Maclean, wakati akitoa elimu ya  Nishati Safi ya Kupikia kwa  Wajasiriamali mkoani Songwe. Amesema kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, ni asilimia 16 tu ya Watanzania ndio wanaotum...

ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA WANAWAKE MKOANI MBEYA

Image
Ni kupitia Kongamano la Wanawake na Fursa za Kiuchumi Wizara ya Nishati yasisitiza matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ili kulinda afya na mazingira Mbeya. Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetoa wito kwa wananchi kuachana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia na kutumia nishati safi ya kupikia kama vile umeme na gesi ikiwa ni njia pia ya kulinda afya, mazingira na kuimarisha uchumi wa kaya. Wito huo umetolewa leo na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka Wizara ya Nishati, Ndg. Deo Alex katika Kongamano la Wanawake na Wajasiriamali kuhusu fursa za kiuchumi lililofanyika mkoani Mbeya. Ndg. Deo Alex amesema kuwa mwaka 2022 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alitoa maelekezo ya kuandaliwa kwa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ikiwa ni mwanzo wa safari ya kuelekea katika matumizi ya nishati iliyosafi ya kupikia. Ameeleza kuwa kufuatia agizo hilo, Wizara ya Nishati iliandaa mkakati huo na kuuzindua ...

WAGOMBEA UDIWANI ILALA WATAKIWA KUVUNJA MAKUNDI

Image
  Na Mwandishi wetu  Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala Chief Sylvester Yaredi amewaomba Wagombea wa Udiwani Kata zote waliyoteuliwa kugombea nafasi hiyo Wilayani humo,wakawe sehemu ya kuvunja makundi kati yao na kamati za siasa za kata,nakuondoa tofauti walizo nazo ili waingie kwenye uchaguzi wakiwa wamoja.  Yared amewaasa Madiwani hao leo August 15,2025 wakati akiwakabidhi barua za uteuzi wa kugombea nafasi hiyo,nakuwasisitiza kuwa wamoja ili kukisaidia Chama Cha Mapinduzi kupata Ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba 29,2025. "Nimewatoa wasiwasi kuwa chama Cha Mapinduzi kimetumia Vigezo Mbalimbali ambapo kimebaini wanastahili na kufaa kugombea nafasi ya udiwani,walikua wagombea wengi lakini nafasi ilikua ni moja kwa maana hiyo waliopata nafasi ya uteuzi nimewaasa wasijione wao ni bora zaidi kuliko wenzao." Ameongeza" Cha pili ambacho nimewaasa wagombea wote wa Chama Cha Mapinduzi nafasi ya udiwani Wilaya ya Ilala,nimewaomba warudi chini wakaj...

NITAWATUMIKIA WANANCHI KIMANGA- JULIUS LYIMO

Image
Na Mwandishi Wetu. Mgombea Udiwani wa Kata ya Kimanga kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM)Julius Pitter Lymo amesema kuwa atashirikiana Vyema na Wananchi wa kata hiyo katika kutatua changamoto zinazowakabila endapo watampa ridhaa ya kuwa diwani wao katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29,Mwaka huu. Amesema hayo leo Agost 15,2025 Jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wanahabari mara baada ya kukabidhiwa barua ya uteuzi wa kugombea nafasi hiyo kutoka kwa katibu wa CCM Ilala Chief Sylivester Yared. "Kusema kweli leo nina furaha sana chama Changu kuniamini nakuona kwamba naweza  kuwaletea wananchi wa Kimanga Maendeleo,na leo tupo hapa kuchukua barua zetu za uteuzi,hivyo wana Kimanga nawaahidi sito waangusha,nitaitekeleza Vyema Ilani ya Chama Chetu". Nakuongeza kuwa" Kimanga ina changamoto kubwa ya Miundombinu na mimi katika vipaumbele vyangu namba moja ni Miundombinu,tutajitahidi Kimanga tupate barabara ambazo zita tuunganisha na Kata zingine,vilevile Kimanga ina changamoto ya st...

LUCY AWATAKA WANANCHI KUIUNGA MKONO CCM

Image
 Na Mwandishi Wetu  MGOMBEA wa udiwani wa Kata ya Kisukuru kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM),  Lucy Lugome, ameahidi kuendesha kampeni za kistaarabu, zenye amani na busara, huku akiwataka wakazi wa Kisukuru kujitokeza kwa wingi kuiunga mkono CCM katika uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Octoba 29 mwaka.huu. Lugome ambaye anagombea kwa kipindi cha pili katika kata hiyo  ameyabainisha hayo leo Agosti 15, 2025 Jijini Dar es salaam mara baada ya kupokea rasmi barua ya uteuzi  kwa ajili ya kupeperusha bendera katika Uchaguzi Mkuu . “Nitaendesha uchaguzi wa amani, hekima na busara kwa lengo la kupata kura za kishindo kwa Rais wetu wa Tanzania, wabunge na madiwani,” amesema Lugome  Ameongeza kuwa, Kata ya Kisukuru iko katika mikono salama chini ya uongozi wake na kuanzia sasa, wananchi wote wamekubaliana kwa pamoja kuacha makundi ya kiushindani na kuungana katika jitihada za kuhakikisha ushindi wa CCM. “Kuanzia leo na kuendelea, sisi watu wa Kisukuru hatuna makun...

KANIKI AAHIDI KUWATUMIKIA WANANCHI ZINGIZIWA

Image
  Na Mwandishi wetu MGOMBEA Udiwani wa Kata ya Zingiziwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Selemani Kaniki, amekishukuru  Chama hicho kwa kumpa ridhaa ya kugombea nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Agosti 15, 2025, mara baada ya kupokea barua rasmi ya uteuzi, katika Ofisi za CCM Wilaya ya Ilala, Kaniki amesema uteuzi huo ni heshima kubwa kwake na kwa wakazi wa Zingiziwa ambao amewahakikishia utumishi uliotukuka. “Nakishukuru Chama cha Mapinduzi kwa kuniamini na kuniteua rasmi kuwa mgombea wa udiwani wa Kata ya Zingiziwa. Hii ni furaha kubwa na ndoto niliyoiombea kwa muda mrefu kwa ajili ya kuwatumikia Wanazingiziwa,” amesema Kaniki.
Image
Mgombea udiwani katika Kata ya Liwiti kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM ), Alice Mwangomo, ameeleza mikakati yake ya kuibadilisha kata hiyo endapo atapata ridhaa katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29 mwaka huu. Akizungumza leo Agosti 15,2025 jijini Dare es Salaam mara baada ya kukabidhiwa barua ya uteuzi na Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala, Sylivester Yaredi, amekishukuru chama hicho kwa kumuamini tena kwa mara ya pili kupeperusha bendera katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba. Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Chama Cha Mapinduzi imefanya mambo makubwa mwaka 2020 - 2025 kwa kutatua changamoto za wananchi wa Kata ya Liwiti ikiwemo ujenzi wa Shule ya Sekondari kwa mtindo wa ghorofa  "Kata ya Liwiti haikuwa na shule ya sekondari lakini kutokana na juhudi za chama chetu na Serikali imeweza kutatua changamoto ya shule ya sekondari, madaraja yanayounganisha Kata ya Kimanga, Kisukuru na Segerea," amesema Mwangomo.

MGOMBEA UDIWANI PUGU STESHENI AAHIDI KUTEKELEZA ILANI

Image
Mgombea wa udiwani kata ya Pugu Stesheni kupitia Chama Cha mapinduzi Salumu Shaibu Omary  amewaahidi wananchi wa kata hiyo kuwafanyia kazi kwa bidii na kuhakikisha ilani ya  chama hicho inatekelezwa ipasavyo. Ameyasema hayo leo  August 25 jijini dare es salaam baada ya kukabidhiwa barua ya uteuzi na katibu wa ccm wilaya ya ilala chief Sylvester Yared, ambapo amesema atafanya kazi kwa bidii ili kutatua kero zilizopo katika kata hiyo ya pugu stesheni. "Nawashukuru wajumbe kwa kuniteua naahidi nitafanya kazi kwa bidii na kutatua kero za wananchi wa kata ya pugu stesheni amesema Omary"

HII HAPA KAULI YA WAHENGA BAADA KUPOKEA BARUA YA UTEUZI

Image
 Na Mwandishi wetu Mgombea Udiwani wa kata ya Kinyerezi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)Jonh Ryoba Mrema maarufu kama "Wahenga" amesema kwamba yupo tayari kuwatumikia wananchi wa Kata ya Kinyerezi endapo watampa ridhaa ya kuwatumikia katika uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba,2025. Ameyasema hayo leo Agost 15,2025 Jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wanahabari mara baada ya kukabidhiwa barua ya uteuzi wa kugombea nafasi hiyo kutoka kwa katibu wa CCM Ilala Chief Sylivester Yared. "Sisi familia yetu ni watu wa kawaida kabisa,lakini nimeaminiwa na wajumbe,Chama kimeniamini,sasa nimepata nafasi yakuenda kuomba ridhaa kwa Wananchi wa kata ya Kinyerezi ili wanichague mimi niwe diwani wao ili tuendeshe gurudumu la Maendeleo"amesema Mrema.  Nakuongeza" Nashukuru sana Mwenyekiti Wetu wa Chama ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka Mazingira sawa ya Ushindani ndani ya Chama,nitoe wito kwa watu wenye ndoto ya kutafuta uo...

JESCA MOTTO AAHIDI MAKUBWA BUYUNI

Image
Mgombea wa Udiwani Kata ya Buyuni Jimbo la Ukonga, Jesca Motto, amesema atahakikisha Kata hiyo inapata maendeleo makubwa chini ya uongozi wake kutokana na kuguswa moja kwa moja na changamoto zilizopo ndani ya Kata hiyo. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es mara baada ya kukabidhiwa barua ya uteuzi kwa nafasi hiyo na Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Chief Sylvester Yaredi katika Ofisi za CCM wilaya ya Ilala amekishukuru Chama chake kwa kumpitisha . "Ulikua mchakato mgumu wagombea walikua wengi lakini nashukuru Chama changu kwa kunipitisha nikawakilishe wananchi naahidi nitatatua changamoto zilizopo katika Kata yetu, tutashirikiana kwa pamoja kuhakikisha maendeleo yanapatikana"amesema Jesca Motto.  Aidha, amesema amemua, kuchukua fomu ya kuomba kugombea udiwani Kata Buyuni ili aweze kumsaidia Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwani amevutiwa sana na uongozi wake wa kuwatumikia wananchi . "Nitajitolea kwa wananchi wangu kuhakikisha wanapata maendeleo katika sek...

BURAH KUIBADILISHA KIWALANI

Image
  Mgombea Udiwani wa Kata Kiwalani Kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Iddi Bura amesema amejipanga kutatua changamoto zilizopo katika Kata hiyo ikiwemo miundombinu ya barabara hasa za ndani ya mitaa. Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam alipokua akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea barua ya uteuzi kutoka Kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala Sylvester Yaredi ambapo amesema Serikali imeleta barabara za lami nyingi. "Barabara za ndani ya mitaa bado ni changamoto mvua ikinyesha hazipitiki nitahakikisha natatua changamoto zote ikiwemo Afya elimu na Maji, nimejipanga kuwahudumia watu wa Kiwalani. Amesema kuwa, Serikali imejitahidi sana kuleta barabara za lami lakini zile za mitaa ni korofi hasa wakati wa mvua, hazipitiki, amewahakikishia wananchi wa Kiwalani anaenda kuzitatua changamoto hizo. "Kama ambayo Chama kimeniamini naomba na wananchi wawe na imani na mimi ili kuhakikisha Kiwalani inazidi kusonga mbele zaidi kwani tuna kwenda kufanya mageuzi makubwa kat...

WALIMBWENDE WA MISS GRAND TANZANIA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HIFADHI YA PANDE

Image
Na Beatus Maganja, Dar es Salaam Walimbwende 24 wanaoshiriki mashindano ya Miss Grand Tanzania 2025 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara, wamefanya ziara ya siku moja katika Hifadhi ya Pande iliyopo jijini Dar es Salaam tarehe 13 Agosti 2025 kwa lengo la kujifunza masuala ya uhifadhi na utalii wa ndani. Ziara hiyo iliandaliwa kwa ushirikiano kati ya waandaaji wa Miss Grand Tanzania na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha walimbwende hao kujifunza masuala ya uhifadhi na utalii na kuwa mabalozi wa vivutio vya utalii wa ndani, hususan Hifadhi ya Pande. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Kamanda wa Hifadhi ya Pande, PC Suleiman Keraryo, alisema hifadhi hiyo ni kivutio cha kipekee kilichopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo wageni hupata fursa ya kutalii na kujionea vivutio mbalimbali  ikiwa ni pamoja na kujifunza kuhusu historia ya hifadhi hiyo, bioanuwai na mchango wake katika uhifadhi wa mazingira na viumbe hai. “Karibun...

MKUTANO WA WAKUU WA TAASISI ZA UMMA KUCHOCHEA MAGEUZI NA USHINDANI

Image
  Na Mwandishi wetu Katika kuendeleza juhudi za Serikali kuhakikisha taasisi za umma zinakuwa sehemu hai ya uchumi wa kisasa, Ofisi ya Msajili wa Hazina imeandaa kikao kazi maalum ‘CEO Forum 2025’ kitakachowaleta pamoja Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa mashirika ya umma nchini wapatao 700. Mkutano huo unaotarajiwa kufanyika Agosti 23-26 jijini Arusha, unalenga kujadili kwa kina jinsi taasisi za umma zinavyoweza kuwa shindani katika soko la kimataifa, kuongeza mapato yasiyo ya kodi, na kushiriki kikamilifu katika kuendesha uchumi wa kisasa unaoongozwa na matokeo. Kupitia mijadala ya kitaasisi, Serikali inalenga kuimarisha ufanisi, uwajibikaji na ubunifu katika taasisi hizi ili ziweze kuwa wabia halisi wa maendeleo ya Taifa.  Aidha, akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Jumatatu, Agosti 11, 2025, Bi. Lightness Mauki, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Utendaji, Ufuatiliaji na Tathmini---Mashirika ya Umma ya kibiashara, alisema kipaumbele kitawekwa katika kufanikish...

RAIS WA TAFF ATUA NCHINI AKITOKEA NCHI ZA AFRIKA, AJA NA MIKAKATI LUKUKI

Image
  Na Mwandishi wetu Rais wa Shirikisho la filamu Tanzania (TAFF) Rajab Amiry leo amerudi nchini Tanzania akitokea nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Botswana, Ethiopia na South Afrika lengo ni kujifunza na kushirikiana na viongozi wa mashirikisho wa Filamu barani Afrika. Akizungumza na waandishi wa habari leo Agost 10, 2025, mashirikisho ya filamu barani Afrika yamelenga kuandaa chombo kimoja maalum kitakachotumika kuonesha kazi za wasanii wa Filam kutoka mataifa yote ya Afrika. Amesema kuwa, mazungumzo yao katika ziara hiyo yalijikita katika kuimarisha ushirikiano wa kisekta, kuongeza nasoko ya kazi za wasanii  na kuanzisha majukwaa ya pamoja ya maonyesho ya filamu za kiafrika. Aidha, amesema Shirikisho la filamu Tanzania limeahidi kutoa Taarifa za kina kuhusu hatua zitakazofuata ikiwa ni pamoja na uzinduzi wa chombo cha pamoja na maonyesho ya filamu za Afrika. Katika hatua nyengine amesema alichukua fomu ya kuomba ridhaa kwa wananchi wa Jimbo la Segerea, aligundua changamoto ...

ROTARY CLUB OYSTERBAY YAWEKA KAMBI YA MATIBABU BURE UKONGA

Image
  Na Mwandishi wetu  Rotary Club  Oysterbay Dar es salaam kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya leo wameweka kambi ya  matibabu bure ikiwemo upimaji wa Saratani ya uzazi, tezi dume, macho, malaria, masikio, VVU pamoja na kutoa ushauri nasaha. Kambi hiyo imewekwa katika  Shule ya Msingi Mzambarauni iliyoko Ukonga Gongolamboto Jijini Dar es salaam huku matarajio ya kuona wagongwa ikiwa ni 3500  kutoka maeneo mbalimbali wakiwemo wazee, wanafunzi na watoto. Akizungumza na waandishi wa habari Agosti 9,2025 Jijini Dar es salaam Muandaji wa Kambi ya Matibabu hiyo, Hilu Bura amesema wamejikita zaidi kutoa huduma kwa Jamii katika maeneo mbalimbali ikiwemo Afya, elimu pamoja na maji. Ameongeza kuwa, zoezi hilo limepokelewa vizuri kwani walijiwekea lengo la kuhudumia watu  Elfu tatu miatano lakini mpaka sasa wanakaribia na kufika lengo hadi kuzidi  "Tumekuja na madaktari bingwa wanawake na wanaume ambao wanatoa huduma za matibabu ya meno, ngozi, masik...

DKT SAMIA KUCHUKUA FOMU LEO

Image
Na Mwandishi wetu Dodoma Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajia kuchukua fomu ya kugombea urais kesho, Agosti 9, 2025, katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), zilizopo Njedengwa, Dodoma. Hayo yamebainishwa mapema leo Agosti 8,2025 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, wakati akizugumza na waandishi wa habari ambapo amesema fomu hiyo atachukua saa 10:50 asubuhi, sambamba na mgombea mwenza, Dkt. Emmanuel Nchimbi. Makalla amesema Tume ya Uchaguzi imetoa ratiba rasmi ya uchaguzi ambayo inaonyesha uchukuaji wa fomu za urais utaanza Agosti 9 hadi 27, wakati ubunge na udiwani ni kuanzia Agosti 14 hadi 27. Uchaguzi Mkuu utafanyika Oktoba 28, 2025. “Kwa upande wa CCM, mchakato wa ndani wa kupata wagombea ulishakamilika mapema Januari mwaka huu. Kwa hiyo Dkt. Samia kama mgombea wa CCM atachukua fomu rasmi kesho,” amesema Makalla. Baada ya kuchukua ...