Posts

Showing posts from August, 2023

USIKOSE KUFUATILIA UTABIRI WA HALI YA HEWA KUANZIA SAA 3:00 USIKU, AGOSTI 28,2023

Image
 

MAWAZIRI, WANASHERIA WAJIFUNGIA DAR KUJADILI MCHAKATO WA KATIBA MPYA

Image
  Na fatma Ally, HPMedia, Dar  Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Damas Ndumbaro amesema kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watanzania hawaifahamu katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo wengine hawajaiona kabisa hivyo ni wajibu wao kuhakikisha watanzania wanaifahamu ili kupuuza maneno wanayoambiwa.  Kauli hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akifungua kikao cha Mawaziri wa sheria na wanasheria wakuu wa Serikali wastafu na waliopo madarakani kuhusu majadiliano ya mchakato wa katiba mpya pamoja na mkakati wa Taifa wa elimu ya umma (MTEKU 2023/2026). Amesema kuwa,ipo haja ya watanzania kueleweshwa kuhusu katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuijua ili kuuza maneno wanayoambiwa ambayo hayahusu katiba ikiwemo kupanda kwa bei bidhaa ikiwemo vyakula pamoja ugumu wa maisha. "Wapo watanzania ambao hawaijui kabisa katiba na wengine hawajaiona kabisa hivyo ni muhimu kuifahamu ili yanapozungumzwa mambo yanayohusu katiba iwe ni rahisi kuweza kuyafahamu kwa upana

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO, KUANZIA SAA 3 USIKU, LEO AGOSTI 22,2023

Image
 

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO, KUANZIA LEO AGOSTI 21,2023

Image
 

ZUNGU ATOA MAJIKO YA GESI 200 KWA MAMA LISHE ILALA

Image
  Na fatma Ally, Matukio DaimaApp, Dar  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu amegawa majiko 200 ya gesi kwa mama lishe wa soko la Machinga Complex lililopo Ilala Ili watumie nishati mbadala waache kutumia kuni katika kupika chakula . Akizungumza mbele ya mama lishe hao na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema Rais wa Dkt Samia Suluhu Hassan anajali afya za wafanyabiashara  wa mama lishe ndio maana amewagawia majiko Ili kurahisisha mapishi waache kutumia mapishi ya kutumia moshi ni hatari katika afya . "Tumegawa majiko ya gesi kwa mama lishe wa Ilala soko la Machinga Complex, Ilala Boma, Mchikichini na Gerezani, hii itawasaidia mama lishe kupika chakula na kupasha moto kila wakati kwa wateja wao itawavutia biashara zao "amesema Zungu . Aidha, amewataka waondokane na kasumba kwamba chakula ukipika na gesi sio kizuri badala yake watumie gesi katika mapishi yao mapishi ya gesi hayana  moshi na chakula kinakuwa ki

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KILIMO

Image
  Na Mwandishiwetu, HPMedia, Dar  Mkurugenzi Mtendaji wa TANTRED Latifa Khamis amezindua kongamano la kimataifa la biashara ya mazao ya kilimo (World agrifam) ilikua lengo kuu ni kufungua fursa kwa wakulima wa mazao ya jamii ya mikunde korosho mafuta pamoja na pamba kwa kwani  walaji wakubwa wa mazao hayo ni bara la Asia. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kuzindua kongamano hilo wakati akimuwakilisha Waziri wa Viwanda Dk Ashatu Kijaji amesema kuwa, ni jambo la kupongezwa kwa ubalozi wa India kwa kuamua kuleta kongamano hilo Nchini Tanzania kwani wakulima wadogo watapata fursa ya kuonana na wahusika wenyewe wanaojihusisha na mazao ya kilimo. Aidha, amewataka watanzania kushiriki kwa wingi katika kongamano la kimataifa la biashara ya mazao ya kilimo World agrifam ili kuweza kupata fursa ya kuuza mazao mbali mbali nje ya nchi. Amesema kuwa, kwa mazao ya kilimo yamekuwa yakifanya vizuri katika soko la nje hususani zao la parachichi kutoka mkoa wa  mbeya

IGP WAMBURA ATOA ONYO KWA WANAOTISHIA KUIANGUSHA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

Image
  Na Mwandishiwetu, HPMedia, Dar Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Camilius Wambura ametoa onyo kali kwa  kundi la watu waliosambaza taarifa kuwa  wanaandaa maandamano nchi nzima juu ya kuiangusha Serikali ya awamu ya sita kabla ya mwaka 2025, kwani Jeshi la Polisi halitakaa kimya na kuwavumilia kitendo wanachotaka kukifanya cha kuvunja amani iliyopo.  Onyo hilo amelitoa leo Jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema kuna watu ambao wanasambaza taarifa za ajabu huku zikihusisha maaandano nchi nzima, huku wakiwashawishi watanzania wawaunge mkono katika hoja zao. Amesema kuwa, maandamano hayo wanayoyapanga kushawishi jumuiya ya watanzania na kuwataka waunge mkono mjadala wa Bandari unaoendelea. "Sisi tuliamini suala la bandari linajibiwa kwa hoja na na vilevile tukaamini kwa sababu hawa watu walikwenda mahakamani wangeheshimu maamuzi ya mahakama lakini badala yake wametoka Sasa na kuanza kutafuta ushawishi na kuwataka watanzania waingie kwenye maandaman

PODIUM INC KUWANOA WAANDISHINWA HABARI

Image
Na Mwandishi wetu HPMedia, Dar  Katika kukuza sekta ya habari hapa nchini Kampuni ya Podium inayojihusisha na masuala ya Habari, Mawasiliano na Utafiti imeandaa mijadala ya kila mwezi ambayo inatarajiwa kuanza mwisho wa mwezi wa nane na itahusisha wanahabari hususani vijana wanaochipukia ili kuhakikisha kuwa jamii inapata taarifa kwa usahihi. Haya yameelezwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Podium Ezekiel Kamwaga ambapo amesema kupitia mijadala hiyo wanahabari watapewa fursa ya kujifunza jinsi ya kuripoti taarifa mbalimbali za kimataifa na kujiongezea maarifa kwa mambo ambayo hawakufundishwa vyuoni. “Kupitia mijadala hiyo wanahabari watatuambia wao wanataka mafunzo gani pengine vyuoni hayakuwepo ila wameingia kazini wakakutana nayo, hivyo nitakuwa namleta mtu kufundisha kile ambacho wanataka kufundishwa, pia nitatoa elimu kuhusu matukio makubwa yanayotokea Duniani kama Tanzania tunakipi cha kujifunza mfano kwa sasa Mapinduzi yaliyotokea katika nchi ya Niger

TANZANIA KUJENGA USHIRIKIANO NA INDIA MAONYESHO YA CHAKULA

Image
Na fatma Ally, HPMedia  Tanzania kwa kushirikiana na India kupitia mkutano wa kimataifa wa chakula ambao unafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika wataweza kukabiliana na changamoto zilizopo na kuimarisha zaidi mahusiano yao na kuongeza uwekezaji kutoka India ambao utaongeza pato la taifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa TASO Event Suveer Rajpuexlint amesema kwani India ni soko kubwa kwa nchi za Afrika hivyo Afrika wanakaribishwa kuwekeza nchini humo. Aidha, kupitia mkutano huo utajenga ushirikiano kati ya India na nchi za Afrika kwenye maswali ya kiuchumi kibiashara na kijamii. "Mahusiano kati ya Afrika na India yanazidi kukua hususani sekta ya kilimo kwani changamoto za wakulima Afrika zinafanana na za India hivyo lengo lao ni kukuza wakulima wadogo na kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na India kwenye bidhaa za kilimo"amesema. Aidha, amesema Tanzania kwa mara ya kwanza kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa Chakula

DUMU 364 ZAKAMATWA KUNDUCHI, MITUMBWI MIWILI FERI

Image
Jeshi la Polisi Kikosi cha Wanamaji kinaendelea na Operesheni maalum iliyoanza Julai 19, 2023 na inayoendelea katika kudhibiti uhalifu ukanda wa Bahari ya Hindi. Aidha katika Operesheni hiyo Kikosi kazi cha Operesheni cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam wakitumia boti ya Polisi walikamata mitumbwi miwili isiyokuwa na jina wala usajili huko maeneo ya feri Wilaya ya Ilala, na Tafico Wilaya ya Kigamboni Jijini Dar es Salaam, iliyokuwa inatumika kuvua samaki kwa kutumia nyavu haramu aina ya kokoro. Katika hatua nyingine, operesheni hiyo Julai 25, 2023 majira ya saa nane usiku huko maeneo ya Kunduchi katika bahari ya hindi askari Polisi kwa kushirikiana na maofisa wa Mamlaka ya Mapato. Nchini (TRA) wakiwa doria walifanikiwa kuwakamata Abdalla Jecha @ omary (37) na Khatibu Kombo (23) wakiwa na Jahazi liitwalo SAFINIA lisilokuwa na namba za usajili likiwa limebeba mafuta ya kupikia aina ya ACTER dumu 364 na kila moja likiwa na lita 20 yakitokea Unguja kwenda Dar es Salaam kwa kupitia bandari bu

MAENDELEO BENKI YAADHIMISHA MIAKA 10 KWA MBIO ZA HISANI

Image
Na fatma Ally, HPMedia, Dar Katika kusherehekea kutimiza miaka 10 ya benki ya Maendeleo imeandaa matembezi ya hisani yenye lengo la kukusanya shill mill 200 ambazo zitakwenda kusaidia vituo viwili, ikiwemo kituo cha KCMC kilichopo kilimanjaro na Kituo cha kulea watoto wenye chamgamoto ya afya ya akili kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Akizungumza jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa matembezi hayo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo amesema ili kufikia upatikanaji wa fedha hizo ni lazima washiki wote katika matembezi hayo wafikirie upatikanaji wa fedha hizo ikiwemo kununua begi linalouzwa lenye vifaa mbalimbali . "Katika kuunga mkono zoezi hili nakuomba DAS ilala uchukue begi 10 ikiwa ni sehemu ya uchangiaji wetu Halmashauri ya ilala, niwaombe pia wadau wote tuchangie hizo fedha isiishie tu kutembea hadi viwanja vya farasi bali tuhitimishe kwa upatikanaji wa hizo mill 200"amesema DC Mpogolo. Ameongeza kuwa, wanatafuta fedha hizo lwa ajili ya watoto wenye usonji a

SELEMANI AGAI ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA KUTOA LUGHA ZA MATUSI

Image
Na Mwandishi wetu,  HPMedia Dar  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata na linamuhoji kwa kina Selemani Agai Gaya (18) mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kutoa lugha ya matusi mtandaoni dhidi ya Viongozi wakuu wa Serikali  Tanzania kwa kutumia mitandao wa kijamii wa Tiktok. Mtuhumiwa huyo amekamatwa Julai 29, mwaka huu na wenzake  wakitengeneza maudhui za mtandaoni (video) na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii zenye kuwatukana na kuwafedhehesha  viongozi wakuu wa Serikali katika akaunti zao za mtandao wa kijamii. Akizungumza  na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam mapema leo Agosti 1 Kamanda wa Kanda Maalumu  ya Dar es salaam SACP Muliro Jumanne amesema   Jeshi la Polisi linatoa onyo kali kwa mtu au watu wanaotoa lugha za matusi na fedheha kwa Viongozi wa Serikali kwa njia ya mtandao na njia nyingine yoyote. Amesema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Mamlaka nyingine za kisheria wamejipanga kuwafuatilia na kuwakamata, kuwahoji kwa kina kuhakikisha wanafikish

TIRA NA NBC ZAWAHAKIKISHIA WATANZANIA KAMPUNI ZA BIMA ZINA UKWASI WA KUTOSHA

Image
Na fatma Ally,  HPMedia, Dar  Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imewahakikishia watanzania kuwa kampuni wanazozisimiamia zina ukwasi wakutosha na zinaweza kulipa madai ya bima ambayo yameiva na yanatakiwa kulipwa. Kauli hiyo imeitolewa jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware wakati akifungua mafunzo ya akaunti ya dhamana kati ya TIRA na Benki ya NBC ambayo yalilenga kuwajengea uwezo wadau wa bima. Aidha amesema katika kuhakikisha kuwa kampuni za bima hapa nchini  zinatumia akaunti ya dhamana katika mabenki ili kuepusha changamoto ya kampuni hizo kutumia fedha bila ruhusa ya Kamishna wa Bima, leo wameanzisha mashirikiano na benki ya NBC.   "Hapo awali kulikuwa na changamoto ndogo ambapo kampuni za bima zilikuwa na kiwango cha fedha katika Benki ya Tanzania (BoT) lakini kiwango hicho huwekwa kwenye hati fungani na zinapoiva zinarudi katika akaunti ya kampuni ya bima hivyo tukawa tunapata changamoto ya baadhi ya kampun