RAIS SAMIA ANAAMINI KATIKA USHIRIKIANO NA VIONGOZI WA DINI - DKT. BITEKO
📌Atoa pole kwa Familia, KKKT kifo cha Askofu Sendoro 📌Kanisa Lashauriwa Kumuenzi Askofu Sendoro kwa Vitendo 📌 Waumini Waaswa Kuishi Maisha ya Kumpendeza Mungu Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali ipo tayari kushirikiana na viongozi wa dini ili kuwawezesha kutimiza majukumu yao ya kitume kwa maendeleo ya Watanzania. Dkt. Biteko amesema hayo leo Septemba 17, 2024 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya Mwanga, Kanisa Kuu lililopo Mkoani Kilimanjaro wakati akitoa salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya ibada ya mazishi ya aliyekuwa Askofu wa Dayosisi hiyo, Chediel Sendoro. Askofu Sendoro amefariki dunia kwa ajali ya gari iliyotokea Septemba 9, 2024 katika eneo la Kisangiro wilayani Mwanga. “ Rais yupo tayari kushirikiana na kanisa wakati wowote ili kanisa liweze kufanya kazi zote za kitume na sisi tuk