Posts

Showing posts from May, 2023

UWT KUNDUCHI YATOA ELIMU YA UKALITI NA MAADILI MEMA KWA WANAFUNZI 5000

Image
Na Mwandishi wetu HPMedia, Dar  Umoja wa Wanawake Kata Kunduchi (UWT) imewajengea uwezo wanafunzi zaidi ya 5000kutoka Shule ya Sekondari Kondo, Shule za Msingi Pius Msekwa na Shule ya Msingi Kunduchi lengo ikiwa ni kuwataka watambue cha kufanya hasa wanapotendewa ukatili wa kijinsia ama wanapokutana nao. Akizungumza na wanafunzi katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kunduchi Twilumba Jane Balama amesema watahakikisha wanawafikia wanafunzi wote katika shule zilizopo kwenye Kata ya Kunduchi ili kuisaidia Serikali kupambana na ukatili na hasa kutengeneza kizazi kilicho bora zaidi kwa maslahi mapana ya nchi ya Tanzania. Amesema kuwa, lengo kufanya ziara hiyo ni kutokana na vitendo vya ukatili wa kijinsia  kuongezeka siku hadi, hivyo wameona ni jambo jema kuanzia mashuleni ambako ndio kuna wahanga wakubwa. "Tumeona tuanzie mashuleni kwani watoto wengi ndio waathirika wa vitendo vya ukatili  kwa hiyo tumewafikia watoto wasiopungua 5000 na kuzungumza nao kuhusu maadili mema na nam

AMOS MAKALLA AHAMISHIWA MWANZA

Image
 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko ya wakuu wa mikoa ambapo aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amehamishiwa mkoa wa Mwanza

HII HAPA HISTORIA YA MEMBE NI BALAA

Image
  Bernard Kamilius Membe alizaliwa tarehe 9 Novemba, 1953, Rondo, Chiponda, katika Mkoa wa Lindi, akiwa ni mtoto wa pili kati wa watoto saba (7) waliozaliwa katika familia ya Mzee Kamillius Anthony Ntachile na Mama Cecilia John Membe. Bernard Membe ni Mmwera, na kama ilivyo desturi ya Wamwera, watoto hutumia jina la ukoo wa Mama. Hivyo watoto wote saba wa familia hii ya Mzee Kamillius wamekuwa wanatumia jina la upande wa mama yao, Cecilia, yaani Membe. Elimu 1962 – 1968: Elimu ya msingi katika shule ya msingi ya Chiponda, Lindi. 1969 – 1972: Elimu ya Sekondari, (O-level) Namupa Seminary, Lindi. 1973 – 1974: Kidato cha tano na sita (A-level) Itaga Seminary, Tabora. 1975 – 1980: Aliajiriwa serikalini, ofisi ya rais. 1981 – 1984: Alipata Shahada ya kwanza katika tasnia ya Sayansi katika maswala ya Siasa na mahusiano ya kimataifa (Bachelor Political Science and International Relations) 1985 – 1989: Aliendelea na ajira yake serikalini katika ofisi ya rais. 1990 – 1992: Alipata Stashada ya U

MEMBE AFARIKI DUNIA

Image
  Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Mhe.Bernard Kamilius Membe, amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali ya Kairuki mkoani Dar es Salaam. Taarifa za awali zinaeleza kuwa alipata changamoto ya kifua na kupelekwa alfajiri ya leo Hospitalini hapo na baadaye kufariki.