Posts

Showing posts from September, 2023

USIKOSE KUFATILIA UTABIRI WA HALI YA HEWA, KUANZIA SAA 3 USIKU, LEO SEPT 15, 2023

Image
 

WATANZANIA WATAKIWA KUFANYA MAOMBI

Image
Na Mwandishi wetu, HPMedia, Dar Nabii wa Taifa Dkt. Kennedy Mwasumbi kupitia huduma ya Tanzania Itubu Ministry amesema kutokana na mambo yanayoendelea kwa sasa, Tanzania hali sio nzuri, hivyo kuna haja kama taifa kufanya maombi ya kutubu. Rai hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema amekua akipata maono kuhusu nchi ya Tanzania, hivyo anaomba kuonana Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwenda kumueleza kwa mustakabali wa nchi. "Nimejitokeza mbele yenu waandishinwa habari kuongea na watanzania kupitia vyombo vyenu, watanzania wanatakiwa wafanye maombi ya kutubu ili nchi iwe salama ipate utulivu, nchi yetu sio maskini lakini inahitajika kufunguliwa macho ili kuufikia utajiri uliopo,lazima tumtegemee Mungu"amesema Nabii Mwasumbi. Hata hivyo, amesema kumekuwa na mijadala mingi kupitia makundi tofauti kutumia sheria kutafsiri mambo kupitia hiyo mijadala kuna wenye hila wanaojificha nyuma ya matu

TAASISI YA MAMA ONGEA NA MWANAO YAIGUSA JAMII

Image
Na Mwandishi wetu,HPMedia, Dar Katika kuhamasisha elimu nchini Tanzania, Taasisi ya mama ongea na mwanao imelenga kufanya kampeni ya kugawa viatu kwa watoto mashuleni (wanafunzi) hususani vijijini nchi nzima lengo ni kuwaenua watoto hao kutokatisha ndoto zao za masomo.  Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Steven Mengele amesema lengo la kampeni hiyo kuinga mkono Serikali katika kuisaidia jamii ambapo zoezi hilo wanatarajia kuanza mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma. "Zoezi hili tutalifanya nchi nzima tumelenga vijijini na tutalifanya wenyewe na si kukabidhi kwa uongozi wa shule kwani lengo letu ni kuhakikisha viatu hivi vinamfikia mlengwa moja kwa moja"amesema Steve. Amesema kuwa, Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imeweka miundombinu mizuri katika sekta ya elimu hivyo wanawajibu kama taasisi inayounga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Dkt Samia kuhakikisha watoto wanaipenda shule. "Miundombinu im

KAMPUNI TANO ZA WAZAWA ZASHINDA ZABUNI UCHIMBAJI WA MAKAA YA MAWE

Image
Na Fatma Ally,HPMedi, Dar Katika kuhakikisha Serikali inatoa kipaumbele kwa wawekezaji wazawa imetiliana saini na kampuni tano za kitanzania ambazo zimeshinda zabuni ya uchimbaji wa makaa ya mawe eneo la Mchuchuma Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mchimbaji na Mwekezaji wa Madini kutoka kampuni ya Cleveland Minging and Cervice Compan, Ndaisaba George Luhoro amesema kwa sasa wanaenda kuandika historia na kuongeza ajira katika pato la taifa kwa makaa ya mawe waliyokuwa wanayasikia toka wazaliwe sasa wanaenda kuyachimba. "Kampuni yangu pamoja na makampuni mengine tulikuwa kwenye ushindani mkubwa ila kwa bahati nzuri kampuni tano ikiwemo na ya kwangu tumefanikiwa kupata mkataba huu hivyo tunaenda kuandika historia yale makaa ya mawe toka tuzaliwe tulikuwa tunayasikia sasa tunaenda kuya chimba na kuongeza ajira Kwa watanzania na kuchangia uchumi Kwa nchi yetu"amesema Mwekezaji Luhoro. Aidha, amesema kupitia uchimbaji huo watao

USIKOSE KUFUATILIA UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO, KUANZIA SAA 3 USIKU, SEPT 7,2023

Image
 

MAMIA YA VIJANA WAJITOKEZA TAMASHA SINGELI KIPAJI VINGUNGUTI

Image
  Mamia ya vijana wafurika uwanja wa msikate tamaa  kwenye uzinduzi wa Singeli kipaji kata ya Vingunguti Manispaa ya ilala jiji la Dar es salam ambapo vijana kutoka mikoa mbali mbali wamefika ikiwemo Mtwara na Morogoro. Akizungumza wakati wa kufunga mashindano hayo Meya wa jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto amesema lengo la mashindano hayo ni kutekeleza agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania la kuibua vipaji vya singeli katika halmashauri zote nchini. Amesema kuwa, mwitikio wa vijana kujitokeza kwenye tamasha hilo umekua mkubwa kwani wamejiyokeza kutoka mikoa mbalimbali sio Dar es Salaam peke yake. "Asanteni kwa kuja, mmeitikia wito mmekuja kwa wingi mmeujaza uwanja, kama serikali hatutowaangusha tutahakikisha tunaibua vipaji,leo muda umekua mchache kwa wingi wenu lakini tutairudia tena"amesema Meya Kumbilamoto. Aidha amewasihi vijana kutokata tamaa katika harakati za kujitafuta kwani wanaweza kuanguka hata mara kadhaa au kutokukubalika baadhi ya sehemu lakini