Posts

Showing posts from December, 2024

KAWAIDA ATOA UJUMBE MZITO KWA VIJANA KUUANZA MWAKA 2025

Image
Na Mohamed Ali Kawaida, _Mwenyekiti wa UVCCM Taifa_ Ndugu vijana wenzangu! Tukiwa tunaanza safari ya mwaka mpya wa 2025, nipende kutumia  fursa hii kuwatakia heri ya mwaka mpya, afya njema, na mafanikio tele. Mwaka mpya ni fursa mpya. Ni ukurasa mwingine wa kitabu cha maisha yetu, kitabu ambacho tunaendelea kukiandika sisi wenyewe kwa bidii na maarifa yetu. Tunapokabiliana na changamoto mbalimbali, ni muhimu tukumbuke kwamba ushindi wetu haupo katika kushindana na wengine, bali katika juhudi zetu binafsi huku tukiwatakia mema wenzetu. Pia umoja na mshikamano wetu kama vijana ndiyo silaha yetu kubwa ya mafanikio. Katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wangu kama Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), nimeona kwa macho yangu nguvu, uthubutu, na bidii za vijana wa Kitanzania katika kulijenga taifa letu. Japokuwa changamoto zipo, lakini fursa ni nyingi mbele yetu, fursa ambazo tukiweza kuzitumia vizuri  zitabadilisha maisha yetu na kuleta faida katika ta...

ZOEZI LA KULIPA FIDIA WANANCHI NGOMBO LINAKWENDA VIZURI : DC MALINYI

Image
 Waliohama kupokelewa vijiji jirani, waipongeza Serikali  Na Beatus Maganja, Malinyi. Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba amesema zoezi la kuwalipa fidia wananchi wa Kijiji cha Ngombo kilichopo ndani ya Pori la Akiba Kilombero Mkoani Morogoro linaendelea vizuri ambapo asilimia 93 ya wananchi wote tayari wamekwishalipwa fidia zao kwa ajili ya kupisha shughuli za uhifadhi katika Hifadhi hiyo na asilimia 7 ya wananchi waliosalia wanaendelea kushughulikiwa ili kukamilisha malipo yao. Akizungumzia zoezi hilo Desemba 31, 2024 wilayani humo Mhe. Sebastian amesema Serikali imetoa zaidi ya shilingi billioni 6.9 kulipa wananchi 1,056  ili waweze kuhama kwa hiari kutoka maeneo ya Hifadhi huku akitoa maelekezo kwa watendaji wa vijiji 32 wilayani Malinyi kuwapokea ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku. "Kwanza si kweli kwamba wananchi wa Ngombo hatujawaambia mahali pakwenda. Katika barua yangu ya tarehe 4 Disemba, 2024  niliyowaandikia watendaji wa vijiji...

ZAIDI YA WATALII 700 WAFURIKA TABORA ZOO KUJIONE MAAJABU YA BUSTANI HIYO

Image
Na Beatus Maganja  Jumla ya watalii 770 kutoka viunga vya Mkoa wa Tabora na mikoa ya karibu wametembelea Bustani ya wanyamapori hai almaarufu TABORA ZOO Desemba 25, 2024 kujionea maajabu yaliyopo ndani ya bustani hiyo ikiwemo Nyumbu rafiki wa binadamu mwenye sifa za kipekee za kuambatana na watalii akiwaongoza katika vivutio mbalimbali vilivyopo ndani ya bustani hiyo iliyo chini ya usimamizi wa TAWA Mkoani Tabora. TABORA ZOO ni bustani ya wanyamapori hai iliyosheni aina mbalimbali za wanyamapori kama vile tembo, fisi, pofu, Simba, Chui, Duma, Swala, Pundamilia, Ngiri na wengine wengi wakiwemo ndege nyuni wenye sauti za aina yake. Lakini kumekuwepo na mnyama nyumbu ambaye   amejizolea umaarufu mkubwa hivi karibuni kiasi cha kupewa Jina "TOUR GUIDE" ambaye licha ya kuongoza watalii amekuwa akipenda sana kucheza na binadamu  TAWA inaendelea kuwakaribisha watanzania wote kutembelea Bustani hiyo ya aina yake kujionea urithi wa nchi yao

HUU HAPA UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24, ZIJAZO

Image

GAVU AJIVUNIA UTEKELEZAJI WA ILANI JIMBO LA CHWAKA,AMPONGEZA RAIS MWINYI

Image
*Akabidhi vifaa mbalimbali vyenye thamani ya mamilioni ya fedha katika Jimbo la Chwaka MWAKILISHI wa Jimbo la Chwaka visiwani Zanzibar ambaye pia ni Katibu wa Halmashauri Kuu((NEC) Oganaizesheni Issa Gavu amesema Serikali ya Awamu ya Nane chini ya Rais Dk.Hussein Ali Mwinyi imefanya maendeleo makubwa kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu. Sambamba na hayo amesema wananchi wa Jimbo la Chwaka wameendelea kushuhudia changamoto mbalimbali zikipatiwa ufumbuzi pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya barabara,elimu,afya na maji huku akielezea wazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho kilichokuwa na uthubutu na utayari wa kuwatumikia wananchi. Gavu ameyasema hayo leo Desemba 14,2024 alipokuwa akielezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu katika Jimbo la Chwaka ambapo pia amekabidhi pikipiki 20 zenye thamani ya Sh.milioni 72 , Vifaa vya michezo vyenye thamani ya Sh.milioni 17. Pia amekabidhi  vitenge ,fulana na kofia vyenye thamani ya Sh.milioni  14 , michango kwa jamii milioni 22...

AZAM MEDIA YAWAPA WATEJA WAKE OFA HII, YAZINDUA TAMTHILIA 3 KWA MPIGO

Image
Na Mwandishi wetu, Dar  KAMPUNI ya Azam Media Ltd kupitia msimu huu wa sikukuu ya Christmas imezindua tamthilia tatu kwa mpigo ambazo zinakwenda kutoa elimu kwa watazamaji wake sambamba na kuwapatia  burudani isiyo kifani na kukonga nyoyo zao. Akizungumza Jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa tamthilia hizo Msimamizi Mkuu wa chaneli ya  Sinema Zetu, Sophia Mgaza amezitaja tamthilia hizo kuwa ni Kombolea, Tufani pamoja na Kiki ambazo zimeandaliwa kwa ubunifu mkubwa. "Tamthilia ya Tufani itaanza kuonyeshwa Desemba 9,2024 kuanzia Jumatatu hadi Alhamisi saa 1:30 usiku,Kombolela itaanza kuonyeshwa Disemba13,2024 siku ya ,ijumaa hadi jumapili saa 1:00 usiku,huku tamthilia ya Kiki itaanza kuonyeshwa Desemba 16 ,2024 jumatatu hadi Alhamisi saa 1:00 usiku,ambapo tamthilia zote hizi zitaonekana kupitia chaneli namba 106 Sinema zetu HD" amesema Mgaza Nakuongeza kuwa" Lengo la Azam Media Ltd kuendelea kutoa burudani ya hali ya juu kwa watazamaji Wetu huku tukisukuma Sanaa yetu ...

WAKILI MWABUKUSI AFUNGUKA KUTUPILIWA MBALI MAOMBI YA MDUDE.

Image
Na Mwandishi wetu, Dar  Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya mawakili wa upande wa utetezi kutaka mwanaharakati Mdude Nyagali afikishwe mahakamani kwa madai kuwa kiapo kinzani hakijathibitisha kujeruhiwa na kushikiliwa kinyume cha sheria kwa mwanaharakati huyo. Mawakili Boniface Mwabukusi na mwenzake Philip Mwakilima, walieleza hoja za mwanaharakati Mdude Nyagali Mpaluka kushikiliwa kinyume cha sheria na kwamba mpaka sasa bado yuko mikononi mwa Polisi hivyo pia walikuwa wakiiomba mahakama iamuru mwanaharakati huyo afikishwe mahakamani. Hata hivyo Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Mbeya aliyekuwa akisikiliza maombi hayo Musa Pomo ametupilia mbali maombi hayo akisema upande wa waleta maombi (Wakili Mwabukusi na Mwakilima) hawajathibitisha kuwa Mdude Nyagali alipigwa wala kujeruhiwa jambo ambalo linaelezwa na mawakili wa utetezi kuwa halikuhitajika na upande wowote mbele ya Mahakama na kama kungehitajika uthibitisho wa vielelezo wangewasilisha iki...

KAWAIDA ATOA UJUMBE HUU SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Image
Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani 2024, Chagua Njia, Tokomeza UKIMWI Ujumbe wangu, Mohammed Ali Kawaida, _Mwenyekiti UVCCM Taifa Leo, tarehe 1 Desemba 2024, Tanzania inaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani. Maadhimisho haya yanayoratibiwa kitaifa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), mwaka huu yanafanyika mkoani Ruvuma yakibeba kauli mbiu yenye nguvu na matumaini: “Chagua Njia, Tokomeza UKIMWI.” Kauli mbiu hii haizungumzii tu mbinu za kujikinga, bali inatufundisha kuchagua njia ya maisha yenye afya, mshikamano, na uwajibikaji ili kufanikisha lengo la dunia la sifuri tatu: sifuri maambukizi mapya ya VVU, sifuri unyanyapaa na ubaguzi, na sifuri vifo vinavyotokana na UKIMWI. Mimi Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, ninatoa wito kwa vijana wenzangu wa  Kitanzania kushikamana na kutumia nafasi yetu ya kipekee katika mapambano haya. Ni wakati wetu kuchukua hatua, si tu kwa faida yet...