Posts

Showing posts from January, 2025

RC CHALAMILA: DAR- KUZINDUA BIASHARA SAA 24 FEBRUARI 22,2025

Image
Asema maandalizi ya kufunga taa na Camera za usalama yanendelea vizuri. Mara baada ya jiji la Dar es salaam kufanikiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Nishati wa wakuu wa Nchi za Afrika Mkuu wa Mkoa huo Mhe Albert Chalamila ametangaza rasmi kuanza kwa shughuli za biashara kwenye jiji hilo saa 24 ambapo uzinduzi rasmi utafanyika februari 22 mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo Januari 30,2025 katika ukumbi wa Hotel ya Johari Rotana,  RC Chalamila amesema jiji hilo ni muhimu kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi hivyo februari 22 mwaka Mkoa huo utazindua rasmi mpango shughuli za kibiashara kufanyika saa 24, kwa sasa wanaendelea kufunga taa za kutosha na maandalizi ya kufunga kamera yanaendelea vizuri kwa ajili ya usalama. Aidha akizungumzia Mkutano wa Nishati wa wakuu wa Nchi za Afrika RC Chalamila amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Mkoa huo kwa ushirikiano mkubwa walioutoa ikiwemo kuimarisha amani, utulivu na usafi hivvyo ameelekeza wilaya zote kuendelea...

FURAHIKA EDUCATION YAAHIDI KUINGA MKONO SERIKALI, YANADI MATUNDA YAKE

Image
KATIKA kuelekea kutimiza miaka 48 ya Chama cha Mapinduzi (CCM),tangu kuzaliwa kwake, Chuo cha Ufundi Furahika VETA  kilichopo Buguruni Malapa jijini Dar es Salaam kimeipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kusimamia vyema ilani ya Chama hicho kwa kupiga hatua katika kukuza Sekta ya Elimu nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa bodi ya Chuo hicho Ngwenje Mohamed amesema Sekta hiyo imekuwa Kwa kiwango Cha juu ikilinganishwa na miaka ya huko nyuma kwani sasa shule za kata Kila mahali vyuo vya kati na vikuu vimeongezeka hiyo yote ni jitihada za Chama cha CCM kupitia ilani yake kuhakikisha kila Mtanzania bila kubagua dini Chama ukabila watu wote wanapata elimu. "Kuelekea maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa chama cha CCM Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan tunaona mengi aliyoyafanya ameendeleza utoaji elimu bure vyuo vya Ufundi Veta navyo vikipewa kipaumbele ili kuibua ujuzi na tafitibalimbali hii inaonyesha  kuwa, m...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO KUANZIA SAA TATU USIKU, JAN 30, 2025

Image
 

HUU HAPA UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO, LEO JAN 26,2025

Image
 

WASIRA: UAMUZI WA MKUTANO MKUU UMEZINGATIA KATIBA YA CCM

Image
Awapa darasa wanaodai sababu ya CCM kupitisha wagombea Urais - Asema yupo tayari kuwapa somo waifahamu vyema katiba ya Chama   MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mainduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema uamuzi wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM, uliomchagua Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kugombea kiti cha Urais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, umezingatia takwa la kikatiba na mamlaka ya Mkutano Mkuu. Amesema baadhi ya watu wanaojiita wanaCCM wanaodai kwamba bado hawajaelewa sababu ya wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM kupitisha uamuzi huo, atawasaidia kuelewesha kwani uwezo wa binadamu kufahamu jambo hauwezi kulingana. Wasira aliyasema hayo jijini Dar es Salaam leo wakati viongozi, wanachama,  wapenzi wa CCM na wananchi kutoka maeneo mbalimbali walipojitokeza kumpokea. "Baada ya Mkutano Mkuu kutambua kazi kubwa zilizofanywa na serikali zote mbili, Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar, Mkutano Mkuu wa CCM ukasema kama hali ni hii kuna sababu ga...

UWOYA AJA KIVINGINE, AMPA HEKO RAIS DKT SAMIA "KILIMO KINALIPA"

Image
Mwenyekiti wa mradi wa Kilimo Jembe ni Mama Msanii wa bongo movie Iren Uwoya amesema  Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassani na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe katika kipindi cha miaka minne  kumekuwa na mageuzi makubwa sana kwenye sekta ya Kilimo chini ya . Kauli hiyo ameitoa leo Janiari 26, 2024 jijini Dar es Salaam katika hafla fupi ya  kutambulisha mradi huo wa Jembe ni Mama katika mkutano na waandishi wa habari amesema kuwa Serikali imeota ruzuku ya mbolea, pembejeo,mikopo, na kuwatafutia masoko wakulima ili wauze mazao ya Kwa bei nzuri bila ya kupata hasara hivyo hilo ni jambo la kipekee.  " Mradi huu wa Jembe ni Mama wataungana kufanya ziara nchi mzima Kwa wanawake wote wanafanyia Kilimo Kwa kuwatia moyo wasikate tamaa kwani Kilimo ni uti wa mgongo wa mtanzania na husaidia kusomesha watoto kulisha familia kujenga mkazi bora wanawake tutambee sisi ni nguzo muhimu Kwa familia Kilimo hakimtupi mtu " amesema Irene Uwoya. Irene U...

RC CHALAMILA AONGOZA WANANCHI KUFANYA USAFI

Image
  -Asema Tanzania inaingia kwenye historia nyingine ya kuwa mwenyeji wa Mkutano  mkubwa wa Marais wa Afrika -Atoa taarifa ya kufungwa kwa baadhi ya barabara siku chache ambazo ugeni utakuwa katika Mkoa huo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Januari 25, 2025 ameongoza mamia ya wananchi wa Wilaya ya Ilala kufanya usafi katika eneo la uwanja wa ndege wa Kimataifa Mwl JK Nyerere barabara ya Terminal One kuelekea mjini (City centre) ikiwa ni maandalizi ya mapokezi ya ugeni mkubwa wa Marais wa Afrika ambao wanatarajia kuwasili kuanzia leo. RC Chalamila amesema Tanzania inaingia kwenye historia ya kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa Marais wa nchi za Afrika kujadili masuala ya Nishati ambao utafanyika tarehe 27-28/01/2025 katika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam.  Mkutano huo unakuja na fursa nyingi za kiuchumi kwa Mkoa na Taifa kwa ujumla ambapo Mhe Mkuu wa Mkoa amewataka wakazi wa Mkoa huo kuzitumia vizuri fursa hizo. Aidha RC Chalamila amesisitiza umuhim...

SHIRIKA LA POSTA LAZINDUA MFUMO WA USAFIRISHAJI VIFURUSHI

Image
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry William Silaa (Mb), amesema kuwa kupitia mfumo wa usafirishaji wa vifurushi, mizigo, na abiria Serikali itaimarisha uchumi wa kidijitali, kukuza baishara mtandao na kuleta ajira nyingi kwa vijana hususan madereva wa pikipiki (bodaboda).   Waziri Silaa ameyasema hayo  wakati akizundua mfumo wa usafirishaji wa vifurushi, mizigo, na abiria ujulikanao kama “Swifpack” na kusisitiza kuwa, huduma hii itatoa fursa za kipato cha uhakika, na kuifanya kazi ya bodaboda kuwa sawa na kazi nyingine za usafirishaji wa vifurushi, mizigo, na abiria. "Leo tunashuhudia hatua nyingine muhimu kwa Shirika la Posta Tanzania kupitia huduma ya Swifpack ambayo itawezesha upatikanaji wa huduma za usafirishaji wa vifurushi, mizigo na abiria kwa kasi, ufanisi na gharama nafuu", amesema Waziri Silaa  Ameongeza kuwa Teknolojia inabadilisha jinsi tunavyofanya kazi na kuwasiliana, na huu ni mfano bora wa jinsi taasisi za umma zinavyoweza kutumia ub...

BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA MWANASHERIA MKUU LAKUTANA

Image
  Mwanasheria Mkuu wa Serikali asisitiza kuendelea kusogeza huduma karibu na Wananchi Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali limekutana na kufanya kikao kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali yatakayosaidia kurahisisha utendaji kazi na kutoa huduma bora zaidi za kisheria kwa wananchi.  Kikao hicho kimefanyika Januari 24, 2025 katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo Kibaha Mkoani, Pwani kwa kuwashirikisha wajumbe kutoka Divisheni, Vitengo na wajumbe wa TUGHE kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.  Akizungumza wakati wa kikao cha Baraza hilo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe, Hamza S. Johari, amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kufanya tathmini ya utendaji kazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na kujadili na kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Ofisi. “Tumekutana kwenye kikao hiki cha Baraza na kupitia kwa pamoja changamoto zetu hasa suala la mafunzo kwa ...

KAMATI YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA UANDAAJI WA MPANGO KAZI WA KITAIFA WAKUTANA DAR

Image
 Na Mwandishi wetu  Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi wa Uandaaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu na Biashara imefanya kikao maalum kuhakikisha kuwa rasimu ya mpango kazi huo inakidhi viwango vya kitaifa na kimataifa katika kulinda na kuheshimu haki za binadamu ndani ya mazingira ya biashara  Aidha, pamoja na mambo mengine timu hiyo ya wataalam imekabidhi rasimu ya awali ya mpango kazi huo kwa kamati lengo ikiwa ni kufanya mapitio na kuidhinishwa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mohamed Khamis Hamad amesema kuwa, mpango kazi huo utakuwa na mikakati ambayo inahusiana na masuala ya haki za binadamu katika shuguhuli za kibiashara, Serikali baada ya kuridhia itaikabidhi wizara ya katiba na sheria ya Tanzania bara na Zanzibar kwa ajili ya kuratibu mchakato mzima. Aidha, kikao hicho kimejumuisha wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali, sekta binafsi, asasi za kiraia, na wataalam...

TMA YATOA USHAURI HUU KUELEKEA MVUA ZA MSIMU WA MASIKA

Image
  Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) imewataka watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwa ni pamoja na wakulima, wafugaji, mamlaka za wanyama pori, mamlaka za maji na Afya kuendelea kufuata, kupata na kuzingatia ushauri wa wataalam katika sekta husika ili kuepusha athari zinazoweza kujitokeza katika mvua za msimu wa masika. Ushauri huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt Ladislaus Chang'a alipokua akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa mwelekeo wa mvua mvua za msimu wa Masika kuanzia Machi hadi Mei mwaka 2025 ambapo mvua hizo zinatarajiwa kuanzia wiki ya kwanza na pili katika maeneo ya Kanda ya Ziwa Victoria na Pwani ya kaskazini. Aidha, kwa wiki ya pili na ya tatu mwezi Machi mwaka huu katika maeneo ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki ambapo ongezeko la Mvua linatarajiwa mwezi April 2025. "Athari zinatarajiwa ni vipindi vya unyevu wa kuzidi kiasi pamoja na mafuriko vinaweza kujitokeza na kuathiri ukuaji w mazao hususani katika maeneo yanayotarajiwa ku...

KISHINDO CHA RAIS SAMIA SEKTA YA UTALII CHASIKIKA KILWA

Image
Mataifa mbalimbali yafurika Hifadhi ya Urithi wa Dunia Kilwa Kisiwani  Na Beatus Maganja, Kilwa. Kazi kubwa ya kutangaza vivutio vya utalii vya nchi yetu duniani iliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kudhihirika na kishindo chake kutikisa katika Hifadhi ya Urithi wa Utamaduni wa Dunia ya Magofu ya Kale ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara ambayo inaendelea kupokea makundi ya watalii wa nje kutoka Mataifa mbalimbali. Hifadhi hiyo iliyo chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA imefungua ukurasa mpya wa mwaka 2025 Kwa kupokea watalii wa kigeni kutoka Mataifa mbalimbali ambapo Januari 18, 2025 ilipokea wageni 98 na leo Januari 22, 2025 imepokea Kundi lingine la watalii wapatao 173 kutoka Mataifa ya  Uingereza,Finland, Sychelles, Marekani, Sweden, Australia na Ireland ambao Kwa kutumia meli kubwa aina ya Hebridean Sky walifika hifadhini humo Kwa lengo la kutalii. Hatua  iliyochukuliwa na Rai...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24, ZIJAZO KUANZIA SAA TATU USIKU

Image
 

BENKI KUU YANUNUA TANI 2.6 ZA DHAHABU INAYOCHIMBWA NCHINI – WAZIRI MAVUNDE

Image
BoT yanunua dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 570 Asisitiza dhamira ya Tanzania kuwa miongoni mwa mataifa 10 yenye hifadhi kubwa ya dhahabu Afrika Abainisha kuongezeka kwa mapato yatokanayo na madini ya dhahabu Dodoma Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amebainisha kuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imenunua tani 2.6 za dhahabu inayochimbwa na kusafishwa hapa nchini ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukabiliana na changamoto ya upungufu wa fedha za kigeni, kuboresha akiba ya fedha za kigeni, na kuimarisha thamani ya shilingi ya Tanzania. Amesema hayo leo Januari 22, 2024, jijini Dodoma, wakati akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, taarifa inayohusu utendaji wa viwanda vya kusafisha dhahabu nchini kwa kipindi cha Machi hadi Desemba 2024 pamoja na mwenendo wa ununuzi wa dhahabu unaotekelezwa na BoT. Mwenendo wa Ununuzi wa Dhahabu BoT Kwa mujibu wa Waziri Mavunde, tarehe 1 Oktoba 2024, Tume ya Madini ilitoa tangazo linalowataka wachimbaji n...

WAZIRI BASHUNGWA AWASILI MAKAO MAKUU YA POLISI, ZIARA YA KIKAZI.

Image
  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa leo tarehe 22 Januari 2025 amewasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma na kupokelewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP. Camillus Wambura pamoja na Makamishna wa Jeshi hilo Katika ziara hiyo ya kwanza ya Kikazi katika Jeshi la Polisi tangu alipoteuliwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Waziri Bashungwa amepokelewa kwa salamu ya  gwaride la heshima (Mounted Guard). Pamoja na Mambo mengine, Waziri Bashungwa atafanya kikao na kuzungumza na Maafisa, Wakaguzi, Askari wa vyeo mbalimbali na Watumishi wengine wa Jeshi la Polisi.

TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA KUTIKISA ZANZIBAR FEB 14 HADI 16

Image
Na Mwandishi wetu Wasanii kutoka Bara nzima la Afrika wanatarajia kujumuika kwa pamoja kuonesha vipaji vyao katika jukwaa la  Tamasha la Sauti za Busara linalotarajiwa kufanyika Februari 14 hadi 16 Ngome Kongwe Zanzibar huku liongozwa  na kauli mbiu ya "Voice For Peace". Akizugumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa tamasha hilo,Journey Ramadhan  amesema tamasha hilo litafanyika kwa siku tatu za amani, umoja, ubunifu pamoja na utofauti . "Tunawaalika wapenzi wa muziki na wafuasi wa amani kutoka pande zote za dunia kuungana katika tamasha hili kwa siku tatu hivyo tamasha la  Sauti za Busara 2025 linatarajiwa kuwa tukio lisilosahulika"amesema Ramadhan Akitaja majina ya wasanii hao ni pamoja  Thandiswa(Afrika Kusini), Blinky Bill(Kenya), Christian Bella&Malaika Bendi (Tanzania), Bokani Dyer (Afrika Kusini) Frida Amani (Tanzania) The Zawose Queens,Kasiva Mutual,(Kenya) Zanzibar Taarab Heritage Ensemble(Zanzibar), Leo Mkanyia & Swahili...

RAIS SAMIA APONGEZWA KUWEZESHA UJENZI OFISI KUU WMA

Image
✅Katibu Mkuu Viwanda na Biashara amshukuru Rais kutumia vyema fedha za Watanzania ✅Akagua ujenzi Jengo la WMA na kukiri kuridhishwa ✅Mtendaji Mkuu WMA asema litakamilika Februari 10 ✅Litakuwa na Maabara ya kisasa yenye kuhifadhi vipimo kiwango cha kimataifa  Na Veronica Simba – WMA Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah amempongeza na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kuwezesha ujenzi wa Jengo la Ofisi Kuu ya Wakala wa Vipimo (WMA) jijini Dodoma akisema ni matumizi mazuri ya fedha za Watanzania. Ameyasema hayo leo Januari 20, 2025 baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo hilo ambalo limegharimu shilingi bilioni 6.2 na liko katika hatua za mwisho kukamilika. Akizungumza na Waandishi wa Habari, Dkt. Abdallah amesema kuwa lengo la ujenzi wa jengo hilo ni kuhakikisha utoaji huduma katika sekta ya biashara hususan katika bidhaa zinazotoka viwandani unaboreshwa. Akifafanua, amesema kuwa maboresho ya kutoa huduma bora katika sekta ya biashara na katika u...