Posts

Showing posts from July, 2025

WANANCHI WAHIMIZWA KUTEMBELEA MAONESHO YA MUHARRAM EXPO 2025

Image
Na Mwandishi wetu Wananchi wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutembelea mabanda ya maonesho ya pili ya huduma za kifedhanq kijamii 'Muharram Expo 2025' yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam Kiongozi Mwandamizi wa Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Mohamed Issa, amesema  maonesho hayo ni ishara   ya kuingia mwaka mpya wa Kiislamu ambao ni Muharram sawa na mwezi wa kwanza wa kiislamu Hijiria. Amesema kuwa, katika maonesho hayo kutakua na mada mbalimbali ambazo zitatolewa kwa wananchi na wataweza kupata elimu kuhusu uwekezaji ambao hauna riba na watapata elimu namna ya kuweka akiba, kupata mikopo au uwezeshwaji usio na riba. Pia amesema wananchi watapewa elimu kuhusu huduma za Masoko ya mitaji na dhamana na uwekezaji wa pamoja (Collective Investment Schemes) isiyo na riba kama vile mifuko ya Uwekezaji Halal au Halal Fund, hati fungani zisizo na riba inayofahamika kama Sukuk. Aidha, katika Maonyesho h...

SERIKALI YAZINDUA MAFUNZO YA MTANDAO YA AFYA MOJA (ECHO)

Image
  Na Mwandishi wetu– Dar  SERIKALI imeanzisha mafunzo kwa njia ya mtandao ya Afya moja (ECHO) ili kuwajengea uwezo watoa huduma wa kada za afya ya binadamu, wanyama na mazingira kwa ngazi zote. Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Dk.Jim Yonazi wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo tarehe 15 Julai, 2025 katika Kituo cha kurushia Mafunzo kwa njia ya mtandao (ECHO HUB) kilichopo katika jengo la Idara ya Utafiti na Mafunzo Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam. Amesema Serikali inaendelea kukabiliana na majanga na dharula zenye athari kwa afya ya binadamu, wanyama na mazingira hivyo imeona umuhimu wa kuwezesha wataalamu wake kuelewa kwa kina dhana ya Afya Moja. “Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wizara za Kisekta na mradi wa USAID Usalama wa Afya Duniani unaotekelezwa na Shirika la CIHEB Tanzania, imeanzisha mafunzo ya mtandao ya Afya moja (ECHO) ili kujenga uwezo kwa watoa huduma wa kada za afya ya binadamu, wanyama na m...

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKABIDHI TUZO YA UMAHIRI KWA MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO WIZARA YA NISHATI

Image
Ni kufuatia Umahiri wa masuala ya Mawasiliano kwenye Maonesho ya Osaka Expo 2025 Ampongeza kwa kuwa Kiongozi wa mfano wakati wa Mkutano wa Biashara na Uwekezaji na Utalii Osaka Expo 2025 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa leo tarehe 13 Julai, 2025 amemkabidhi Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Nishati, Bi Neema Chalila Mbuja tuzo ya umahiri kufuatia mchango wake  alioutoa wakati wa Maonesho ya Dunia ya Biashara ya Osaka nchini Japan kwa upande wa Mawasiliano na kuitangaza nchi. Mhe Majaliwa amempongeza Bi. Mbuja wakati wa kilele cha  Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salaam maarufu kama Sabasaba 2025. Sambamba na hilo Mhe Majaliwa amempongeza Bi. Mbuja kwa kuwa muongozaji wa shughuli na kuwa mahiri wakati wa Kongamano la Kimataifa la Biashara, Uwekezaji na Utalii kwenye Maonesho ya Osaka Expo 2025. Kwa upande wake Bi. Mbuja amemshukuru Mhe. Majaliwa kwa kukabidhi tuzo hiyo iliyotolewa na Mamlaka ya...

TUMETIMIZA MATAKWA YA ILANI YA CCM YA KUFIKISHA WATALII MILIONI TANO-DKT CHANA

Image
Na Mwandishi wa NCAA, DSM Waziri wa Maliasili na Utalii  mhe. Balozi Dkt.Pindi Chana (mb) amewapongeza watendaji wa wizara hiyo kwa kutimiza malengo ya ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kufikisha idadi ya watalii milioni tano kama ilivyoainishwa kwenye ilanı ya chama hicho. Dkt.Chana ametoa pongezi hizo katika uzinduzi wa siku maalum ya Ngorongoro (Ngorongoro Day) ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya maonesho ya 49 ya biashara ya kimataifa Sabasaba. “Niwapongeze sana watendaji wenzangu wa Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na wadau wa sekta ya utalii kwani ilanı ya CCM ilitutaka tufikishe watalii milioni tano na sasa tunatembea kifua mbele kwani idadi hiyo imetimia. Waziri Chana pia ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) kwa kuvuka lengo la makusanyo kwa mwaka wa fedha 2024/25 kwa kukusanya shilingi bilioni 269.9 kutoka lengo la shilingi bilioni 230. Akitoa maelezo ya siku hiyo ya Ngorongoro Meneja wa huduma za utalii na Masoko Bi Mariam Kobelo amesema leng...

RAIS WA SHIRIKISHO LA FILAMU AMIRY AELEZEA MAFANIKIO YA MKUTANO WA UGANDA

Image
Rais wa shirikisho la filamu Tanzania Rajab Amiry amesema ameshiriki mkutano wa siku tatu nchini Uganda ambapo pamoja na mambo mengine wamesaini makubaliano ya Muungano (MAU) kwa nchi zaidi ya 8 Afrika lengo ni kukuza tasnia ya Filamu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es Salaam aliporudi katika mkutano huo uliofanyika nchini Uganda, amesema mkutano huo walijadili namna gani wanaweza kupata masoko makubwa hivyo wameweka utaratibu mzuri wa kusaini memorandam ambayo itasaidia filamu za Afrika kuweza kuwa katika sehemu nzuri. "Tunashukuru Serikali ya Uganda ambayo ilikuwa sehemu ya udhamani, UNESCO kwa ajili ya kufadhili, Tanzania kwa kutuamini kwa kuwepo bodi ya filamu kuwakilisha, Zanzibar nayo ilikuwepo katika mkutano huo" amesema Rajab Hata hivyo, amesema kushiriki katika mkutano huo kumezaa matunda ya kukutana na Marais wengine wa Shiriko Afrika ambapo imepelelekea kufungua milango mingine katika filamu haswa kwa waigizaji nchini hivyo wajiandae kupata matunda m...

MBIO ZA MSAKUZI PANDE GAME RESERVE ZAZINDULIWA RASMI

Image
Utalii wa michezo wahamasishwa Na. Joyce Ndunguru, Dar es Salaam. Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kushirikiana na Msakuzi Sports Promotion leo Julai 12,2025, imezindua rasmi msimu wa kwanza wa  mbio za riadha zinazojulikana kama "Msakuzi Pande Game Reserve Marathon" zilizofanyika katika Hifadhi ya Pande iliyopo jijini Dar es Salaam. Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa la Tanzania, Dkt. Noel Lwoga amesema lengo kuu la mbio hizi ni kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan za kutangaza na kuhamasisha utalii. "Sote ni mashahidi juhudi hizi zimeweza kuongeza idadi ya watalii wa nje na ndani, ukiangalia idadi ya watalii wa ndani wameongezeka kutoka takribani watalii laki tisa mwaka 2021 hadi watalii takriban Milioni tatu kwa mwaka 2024" amesema Dkt. Lwoga  Sambamba na hilo, Dkt. Lwoga amesema mbio hizi zimejikita pia katika kuhamasisha jami...

HUU HAPA MKAKATI WA WMA KUTOA ELIMU YA VIPIMO

Image
KATIKA kuhakikisha elimu ya vipimo inawakia wananchi wengi zaidi Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) imedhamiria kuanzisha club za mafunzo kuhusu Vipimo katika Shule za Msingi na Sekondari kuhusu Sekta ya vipimo ili watoto wawe na uwelewa mpana kuhusu vipimo. Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano na Uhusiano kutoka Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) Veronica Simba wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari walipomtembelea kwenye banda lao katika maonyesho ya 49 ya biashara ya kimataifa yanayoendelea Sabasaba. Amesema kuwa, kutokana na maoni na  maswali waliokuwa wanaulizwa na wananchi kuhusu Vipimo wameona ipo haja ya kuisambaza zaidi elimu hiyo ili imfikie kila mtu kwa upana zaidi. "Elimu hii inatakiwa imfikie kila mtu kwa upana zaidi na sasa tumekuja na mikakati ambayo tunatamani kwenda kuitekeleza ili sasa tufikie sehemu kubwa zaidi ya jamii"amesema Veronica . Amesema kuwa, kwa sasa wamekua wakitoa elimu kupitia vyombo vya habari na wanashukuru kwa ushir...

WMA YATOA WITO HUU KWA WANANCHI

Image
WANANCHI wametakiwa kuuliza na kujiridhisha wanapokwenda kupata huduma kama bidhaa wanazouziwa vimehakikiwa na Wakala wa Vipimo Tanzania ili kuhakikisha wanapata stahiki zao. Rai hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano na Uhusiano Wakala wa Vipimo Tanzania WMA Veronica Simba alipokua akizungumza na Mtandao wa Habari Plus katika maonyesho yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Sabasaba. Amesema kuwa, kupitia maonyesho hayo wamejifunza vitu vingi sana licha ya kuona mwitikio mkubwa wa wananchi lakini wamegundua wananchi hawana uthubutu wa kuuliza maswali ya uhakiki wa Vipimo wanapokwenda kupatiwa huduma. "Tumegundua kwamba wapo hata wale wanaofahamu kuhusu vipimo lakini bado wana uwoga hawana uthubutu  wa kuliza kama je kipimo kilichotumika kutoa huduma kimehakikiwa na Wakala wa Vipimo ?"amesema Veronica. Hata hivyo, amesema ni haki ya kila mwananchi, mlaji au mdau wa vipimo kujiridhisha na anahaki ya kumuliza mtoa huduma kama bidhaa anam...

WMA YAFIKIA MALENGO MAONYESHO SABASABA

Image
LENGO la kushiriki maonyesho ya Sabasaba limefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuliko hata matarajio yetu tumekuwa na mwitikio mkubwa watu wengi wamefika katika banda letu na kutaka kujua tunafanyaje kazi kuhusu Vipimo" Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano na Uhusiano kutoka Wakala wa Vipimo Tanzania WMA Veronica Simba wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es Salaam. Amesema kuwa katika kuhitimisha maonyesho hayo tangu yalipoanza June 28, 2025, wamepata matokeo mazuri na kwamba wanajipanga kwa mikakati mizuri zaidi ya kutoa elimu kwa jamii. "Sisi jukumu letu kubwa ni kuhakiki Vipimo kumlinda mlaji wa bidhaa na huduma mbalimbali kutoka sekta zote zinazohusiana na Vipimo ili kuhakikisha anapata stahiki yake kwa mujibu wa bidhaa aliyochukua"amesema Veronica. Ameongeza kuwa, wanafanya vipimo kwenye bidhaa zilizofungashwa hadi kwenye supamaket, mfano mtu akinunua bidhaa yoyote ambayo imeshapimwa kama kahawa, mafuta ya kula yeye anajuaje kama kipimo kil...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo,Julai 11,2025

Image
 

WAZIRI DKT NDUMBARO - OFISI YA OCPD NI MUHIMU KATIKA UTUNZI NA UREKEBU WA SHERIA

Image
Na Mwandishi wetu  WAZIRI wa Katiba na Sheria Dkt, Damas Ndubambaro amesema kuwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) ni Taasisi muhimu sana katika suala zima la utunzi na urekebu wa sheria. Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akitembelea banda la Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria OCPD lililopo katika maonyesho ya 49 ya biashara ya kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere (Sabasaba). Amesema kuwa, bila  Ofisi hiyo hakuna sheria ambayo inakwenda kufanyiwa marekebisho wala hakuna sheria ndogo, sheria zote zinafanyiwa marekebisho na zinatafsiriwa. Amesema kuwa ni Ofisi muhimu sana, kwani Ofisi hiyo ikifungwa hata mahakama itakua haiwezi kufanya kazi, kwani watatumia sheria ambazo sio sahihi . "Ni Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa sheria ndio ambayo inatuambia sheria sahihi ni hii ya mwaka huu na kwa toleo hili, lakini kwa sasa hivi wanafanya kazi nzuri za kutafsri sheria kutoka lugha ya kingereza kwenda kiswahili. Aidha, amesema mpaka kufikia June 30 Ofisi ...

RAIS WA SHIRIKISHO LA FILAM TANZANIA ASHIRIKI MKUTANO WA AFRIKA FILMMAKERS

Image
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Bw Rajabu Amiry akiwa na marais na viongozi mbalimbali wa mashirikisho na vyama vya “Filmmakers” ktk nchi nane za Africa. Baada ya vikao vya siku tatu Kampala Uganda tumesaini MOU kwa lengo kufungua mlango mwingine masoko ya Filamu (Sream East).