Posts

Showing posts from March, 2025

DCEA YAMNASA KINARA WA MIRUNGI, YATEKETEZA EKARI 285.5 SAME

Image
Na Mwandishi wetu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola, imefanya operesheni maalum wilayani Same, mkoani Kilimanjaro kuanzia tarehe 19 hadi 25 Machi 2025. Katika operesheni hiyo, ekari 285.5 za mashamba ya mirungi zimeteketezwa na watuhumiwa saba (7) wamekamatwa, akiwemo kinara wa biashara haramu ya mirungi nchini aliyekuwa akitafutwa kwa muda mrefu, Interindwa Zinywangwa Kirumbi, maarufu kwa jina la mama Dangote. Akizungumza baada ya operesheni hiyo, Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo, amesema kuwa, mama Dangote ni mzalishaji na msambazaji mkubwa wa dawa za kulevya aina ya mirungi nchini. Kwa zaidi ya miaka 30, amekuwa akiendesha mitandao ya biashara haramu ya mirungi na kusimamia masoko ya dawa hizo za kulevya katika maeneo mbalimbali nchini, licha ya kujua kuwa ni kinyume cha sheria. Aidha, kamishna Lyimo ameongeza kuwa, mwaka juzi Mamlaka ilifanya operesheni wilayani humo na kutoa elimu kwa wananchi ili waachan...

KAPINGA AZINDUA NAMBA YA BURE YA HUDUMA KWA WATEJA WA TANESCO

Image
Awapongeza TANESCO kutekeleza agizo la Mhe. Dkt. Biteko kuwataka kuanzisha namba ya huduma kwa wateja bure  Asema namba hii ya 180 ya bure kwa wateja kuimarisha huduma kwa wateja na kutatua changamoto zao Awaagiza Mameneja wa Mikoa na wilaya wa TANESCO kuwasimamia watoa huduma Awaasa watanzania kutumia namba hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga leo Machi 12, 2025 amezindua namba mpya ya huduma kwa wateja (mchongo 180) itakayotumiwa na wateja bure bila malipo ili kupata huduma mbalimbali kupitia kituo cha miito ya simu cha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kuanzishwa kwa namba hiyo inafuatia agizo lililotolewa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko la kuwataka TANESCO kuhakikisha wanakuwa na namba ya bure bila malipo kwa wateja ili kuboresha utoaji huduma kwa wateja na kupunguza malalamiko yasiyo ya lazima na kuongeza wigo wa wapokeaji wa simu kutoka namba ya awali hadi 150 kwa awamu. ‘’Naomba...

MRAMBA: BIASHARA YA KUUZIANA UMEME KUINUFAISHA TANZANIA

Image
  Afafanua kuuuza na kununua umeme ni jambo la kawaida kwa nchi Asisitiza kununua umeme kwa Mikoa ya Kaskazini kunamanufaa kwa Mikoa husika Asema kukamilika kwa Mradi wa TAZA kutainufaisha Tanzania na biashara ya umeme Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba ametoa Ufafanuzi zaidi kuhusu hatua ya Serikali kununua Umeme nchini Ethiopitia kupitia Nchini Kenya hadi Namanga Mkoani Arusha  utaimarisha Upatikanaji wa Umeme katika Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ambayo kimsingi kwa sasa inatumia umeme unaozalishwa katika Mikoa ya Kusini. Akizungumza na waandishi wa Habari leo tarehe 10, Machi 2025 Jijini Dar es Salaam Mha. Mramba amesema ununuzi wa Umeme kutoka nchi Jirani haimaanishi kuwa nchi iko katika changamoto ya upungufu wa umeme kwa kuwa mpaka sasa Tanzania inazalisha umeme wa kutosha ambao ni Takribani Megawati 3796. Amefafanua kuwa hatua hii ina faida kwa pande zote mbili kwa kuwa njia itakayotumiwa kununua umeme nchini Ethiopia ndio hiyo itakayotumiwa kuuza ...

TMA YATOA TAHADHARI UWEPO WA KIMBUNGA JUDE

Image
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya uwepo wa kimbunga "JUDE" katika Bahari ya Hindi eneo la Rasi ya Msumbiji. Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwa kimbunga hicho kitaingia nchi kavu katika eneo la Msumbiji mchana wa leo Machi 10 2025 na kupungua nguvu yake.  Hata hivyo, kimbunga “JUDE” kinatarajiwa kurejea tena baharini na kuimarisha nguvu yake katika kipindi cha kati ya tarehe 13 hadi 15 Machi 2025. Aidha, kutokana na mwelekeo na umbali wake kimbunga “JUDE” hakitarajiwi kuwa na athari za moja kwa moja hapa nchini. Hata hivyo, uwepo wa kimbunga hicho katika eneo la rasi ya Msumbiji unatarajiwa kuchagiza mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na kusababisha ongezeko la mvua katika maeneo mbalimbali.  Vilevile, uwepo wa kimbunga hicho unaenda sambamba na kuanza kwa msimu wa mvua za masika, 2025 katika maeneo yapatayo misimu miwili ya mvua kwa mwaka kama ilivyotabiriwa awali na taarifa kutolewa kwa hiyo Umma mnamo tarehe 31 Januari 2025. USHAURI: W...

TAWA NA MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE 2025 MOROGORO

Image
Katika kuadhimisha Kilele cha Siku ya Kimataifa ya wanawake Machi 08, 2025,  wanawake shupavu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA pia walikuwepo katika mji wa Ifakara, Wilaya ya Kilombero, Mkoa wa Morogoro kuungana na maelfu ya wanawake wengine kutoka mashirika, taasisi mbalimbali na wanawake wakazi wa Mkoa huo Kwa ujumla wake kuadhimisha siku hiyo yenye kauli mbiu "Wasichana na Wanawake 2025, Tuimarishe Usawa, Haki na Uwezeshaji". Wanawake wahifadhi wa TAWA wamekuwa mstari wa mbele katika kuadhimisha Siku hiyo adhimu katika mikoa mbalimbali nchini na kutumia fursa hiyo kuuonesha umma wa watanzania namna taasisi hiyo inavyotekeleza Kwa vitendo kauli mbiu ya mwaka 2025.

KILWA YAENDELEA KUFURIKA WATALII

Image
Meli ya "Le Bougainville yaleta wengine zaidi ya 130. Na Beatus Maganja Meli ya Kifahari ya kitalii ya "Le Bougainville,"  imewasili leo Machi 05, 2025 katika Hifadhi ya urithi wa utamaduni wa dunia Magofu ya Kale Kilwa Kisiwani na Songo Mnara Mkoani Lindi ikiwa na jumla ya watalii 133 kutoka Mataifa mbalimbali duniani Kwa ajili ya shughuli za utalii. Hii ikiwa ni safari  yake ya 7 tangu kuanza kwa msimu wa utalii wa Mwaka 2025 Watalii waliotembelea hifadhi hiyo  wametoka Mataifa ya  Denmark, Australia, Canada, Ufaransa, Marekani, Uingereza na Afrika Kusini huku wengine wakitokea Mataifa ya Uswisi, Romania, Ujerumani, Ubelgiji, New Zealand, na Ireland Meli hii ya kifahari inahudumia wageni kutoka pande zote za dunia, ikitoa fursa Kwa watalii kutembelea maeneo ya kihistoria na kiutamaduni ya Kilwa, ambayo ni urithi wa dunia wa UNESCO na kuwawezesha watalii  kushuhudia  tamaduni za kiasili zinazopatikana katika hifadhi hii ya kipekee iliyo chini ya usimamizi ...

DKT.MPANGO ATAKA AFRIKA KUBUNI NJIA BORA UENDELEZAJI RASILIMALI ZA NISHATI ILI KUKIDHI MAHITAJI

Image
Asema upatikanaji wa Nishati Afrika bado ni mdogo kulinganisha na Mabara mengine Asisitiza uendelezaji wa vyanzo vya Nishati uzingatie mustakabali wa vizazi vijavyo Afungua Kongamano na Maonesho ya Petroli kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25) Makamu wa Rais, Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango amesema kuwa matumizi ya nishati katika Bara la  Afrika hasa Kusini mwa Jangwa la Sahara  bado ni madogo ikilinganishwa na maeneo mengine kama Bara la Amerika, Asia na Ulaya hivyo kuna umuhimu wa kubuni njia bora za kuzitumia rasilimali zilizopo ikiwemo Mafuta na Gesi Asilia ili kuwawezesha wananchi kustawi kiuchumi na kijamii huku suala la utunzaji wa mazingira likizingatiwa. Amesema hayo tarehe 5 Machi, 2025 wakati akifungua rasmi Kongamano na Maonesho ya Petroli ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25) ambalo litafanyika kwa muda wa Siku Tatu jijini Dar es Salaam. “Katika kipindi ambacho maendeleo ya nishati endelevu yana mchango mkubwa katika mustakabali wa mazingir...

TAWA Yasherehekea Siku ya Wanyamapori Duniani kwa Kutoa Misaada na Elimu ya Uhifadhi

Image
MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA Kanda ya Magharibi leo Machi 3, 2025 imesherehekea Siku ya Wanyamapori Duniani kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii na uhifadhi, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za kulinda wanyamapori na mazingira. Katika maadhimisho hayo, Kanda hiyo ilitoa misaada ya vyakula kwa wanafunzi wenye uhitaji kutoka Shule ya Wanafunzi wenye changamoto ya uoni ya Furaha ikiwemo mchele, unga, mafuta, sukari na sabuni vyote vikiwa na thamani ya shillingi millioni moja.  Misaada hii imelenga kuwasaidia wanafunzi hao  na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum. Vilevile  TAWA ilitembelea Shule ya Sekondari Fundikila na kutoa miche 4000 ya miti ya matunda ya muda mfupi, ikihamasisha upandaji wa miti na kutoa elimu kuhusu uhifadhi wa mazingira. Shule ya Sekondari Kanyenye nayo ilipokea miche 2000 mingine, kama sehemu ya juhudi za kukuza mazingira bora na endelevu kwa jamii. Akikabidhi misaada hiyo na mi...

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Image
Wizara ya Nishati yajivunia jitihada katika kulinda haki, usawa na kuwawezesha wanawake Kapinga asema lengo ni kuboresha ustawi wa mwanamke na kuongeza thamani yake. Katika kuelekea maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Machi 8, 2025, yenye kaulimbiu "Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji” Wizara ya Nishati inajivunia jitihada zinazofanyika nchini katika kulinda haki usawa na kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia nishati ya umeme na nishati safi ya kupikia.  Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga alipokuwa akieleza ni nama gani Wizara ya Nishati inakwenda kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani. "Tumepeleka umeme kwenye zaidi ya Vitongoji elfu 33, lakini kupitia nishati safi ya kupikia kupitia programu mbalimbali tumepeleka mitungi takribani laki 4020, majiko banifu laki 2 pamoja na majiko ya umeme." Amesema  Kapinga  Ameeleza kuwa jitihada zote za Serikali katika  uwekezaji sekta ya nishati hususani nishati safi ya ...

CUF YATOA MSIMAMO WAKE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 202

Image
  Na Mwandishi Wetu, Dar  Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Prof Ibrahim Lipumba amesema kuwa kutokana na mapendekezo kadhaa yaliyotolewa na vyama vya siasa ni vyema uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ungefanyika baada ya marekebisho ya Sheria na Tume Huru ya Uchaguzi pamoja na upatikanaji wa Katiba Mpya. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema kuwa bila ya kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi ni ngumu sana haki kupatikana kwani waliokutana miaka minne imefika hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanyika, huku akitaka kuwepo na rasimu ya mabadiliko itakayojenga demokrasia . "Katika kuadhimisha miaka 30 ya mfumo wa vyama vingi wadau wa siasa tulikutana pale Dodoma mwaka 2021  kila chama kilinaso sera zao huku wakitoa mapendekezo kadhaa ikiwemo kupatikana kwa tume huru, katiba mpya, sheria ya vyama vya siasa ipitiwe upya pamoja na kuwepo kwa michakato shirikishi" Amesema kuwa, uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2019 na 2024  haukua huru wala haki, bali uliku...