TMA YATOA USHAURI HUU KUELEKEA MVUA ZA MSIMU WA MASIKA


 Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) imewataka watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwa ni pamoja na wakulima, wafugaji, mamlaka za wanyama pori, mamlaka za maji na Afya kuendelea kufuata, kupata na kuzingatia ushauri wa wataalam katika sekta husika ili kuepusha athari zinazoweza kujitokeza katika mvua za msimu wa masika.


Ushauri huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt Ladislaus Chang'a alipokua akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa mwelekeo wa mvua mvua za msimu wa Masika kuanzia Machi hadi Mei mwaka 2025 ambapo mvua hizo zinatarajiwa kuanzia wiki ya kwanza na pili katika maeneo ya Kanda ya Ziwa Victoria na Pwani ya kaskazini.

Aidha, kwa wiki ya pili na ya tatu mwezi Machi mwaka huu katika maeneo ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki ambapo ongezeko la Mvua linatarajiwa mwezi April 2025.

"Athari zinatarajiwa ni vipindi vya unyevu wa kuzidi kiasi pamoja na mafuriko vinaweza kujitokeza na kuathiri ukuaji w mazao hususani katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani, kina Cha majibkatika mito na mabwawa kinatarajiwa kuongezeka hivyo hatari ya mafuriko hususani katika maeneo yanayoathiriwa na mafuriko"amesema

Hata hivyo, amesema  Mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya nyanda za juu Kaskazini Mashariki pamoja na Mashariki mwa Mikoa ya Mara na Simiyu, aidha mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa katika maeneo ya Pwani ya kaskazini kaskazini mwa Mkoa wa kigoma na ukanda wa Ziwa Victoria.

Amesema mvua za Masika zinatarajiwa kuanza Machi 2025 katika maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua, hasa Kanda ya Ziwa Victoria, Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki, Pwani ya Kaskazini, na kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma.

Amesema Mwelekeo wa mvua za Masika 2025 kwa Kanda ya Ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara) pamoja na kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma, Mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinatarajiwa, ambapo zitaanza Machi, wiki ya kwanza hadi ya pili, na kuisha Mei, wiki ya kwanza.

Aidha Pwani ya Kaskazini (kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro, Pwani, Dar es Salaam, Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba) Mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zitaanza Machi, wiki ya kwanza hadi ya pili, na kuisha Mei, wiki ya tatu hadi ya nne.

Pia Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro), kutakuwa na Mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani ambapo zitaanza Machi, wiki ya pili hadi ya tatu, na kuisha Mei, wiki ya kwanza.

Amesema athari zinazotarajiwa ni pamoja na unyevu na mafuriko, ambapo Mvua nyingi zinatarajiwa katika baadhi ya maeneo, na huenda zikapelekea mafuriko na kuathiri ukuaji wa mazao.

Amesisitiza kuwa taarifa hiyo inatolewa kwa ajili ya kusaidia wadau wa sekta mbalimbali, kama vile kilimo, mifugo, uvuvi, maliasili, afya, nishati, usafirishaji, na usimamizi wa maafa, kuchukua tahadhari stahiki na kupanga mikakati ya kukabiliana na athari za mvua.

Awali alisema Mwenendo wa mvua za Msimu (Novemba 2024 – Aprili 2025) zinatarajiwa kuwa za Wastani hadi Chini ya Wastani katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Songwe, Singida na Dodoma, huku mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani zikitarajiwa katika mikoa ya Njombe, Ruvuma, Mtwara, Lindi na mikoa mingine

Comments

Popular posts from this blog

TMA YATOA TAHADHARI KUHUSU UWEPO WA KIMBUNGA "HIDAYA"

HUU NDIO USHAURI WA TMA KWA SEKTA HIZI ...

NLD YAZINDUA KAMPENI "FYEKA CCM", YATOA WITO HUU KWA TAMISEMI