DCEA YAKAMATA KILO 399.28 ZA BANGI

 


 Na mwandishi wetu, HPMedia, Morogoro

Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na Dawa za (DCEA) imekamata jumla ya kilo 399.28 za dawa za kulevya aina ya bangi katika kitongoji cha sokoni, kijiji cha Chogoali kata ya Iyogwe, tarafa ya Gairo, Mkoani Morogoro.

Ukamataji huo umefanyika kufuatia Operesheni iliyofanywa na mamlaka mkoani humo hivi karibuni ambapo watu wawili wanashikiliwa kuhusika na usafirishaji wa kiasi hicho

Aidha watumiaji hao wamekutwa na bunduki mbili aina ya gobole zenye namba MG-188 na MG-148 pamoja na ngozi ya Mnyama anayedhaniwa kuwa kakakuona,

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na na Dawa za kulevya inaendelea kufanya Operesheni nchi nzima ili kuhakikisha inadhibiti usafirishaji wa Dawa za Kulevya na inawaomba wanachi kuwaunga mkono katika mapambano hayo.


Comments

Popular posts from this blog

TMA YATOA TAHADHARI KUHUSU UWEPO WA KIMBUNGA "HIDAYA"

HUU HAPA MWENENDO WA KIMBUNGA "HIDAYA" , UPEPO KUVUMA KWA KASI YA KILOMITA 130 KWA SAA

NHIF YAFANYA MABORESHO YA KITITA CHA HUDUMA ZA MATIBABU, YAENDELEA KUPOKEA MAONI