NCHI 43 ZASHIRIKI MKUTANO WA RASIMALI WATU AFRIKA TANZANIA


Na Mwandishi wetu,Dar

NCHI 43 za bara la Afrika  zashiriki mkutano wa Rasilimali Watu Afrika ambao unafanyika Tanzania kuanzia Julai 25 na 26 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha  Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.                                 

Idadi hiyo ya nchi shiriki imetolewa na Benki ya Dunia (WB) ambao wameshirikiana na Serikali ya Tanzania kuandaa mkutano huo muhimu katika eneo la rasilimali watu.         

Kwa mujibu wa taarifa ambayo imesambazwa kwa waandishi wa habari imeonesha kuwa katika nchi hizo 43 zipo ambazo zimewakilishwa na Marais wenyewe, makamu wa rais, mawaziri wakuu, makamu waziri wakuu, mawaziri na watendaji wengine hii ni kuonyesha ushirikano ulipo baina ya nchi hizo . 

Mkutano huo ulioanza Julai 25 ulifunguliwa na Makamu wa Rais Dk Philip Mpango ka ngazi ya mawaziri na watendaji wa nchi shiriki    Kabla ya mkutano huo kuanza Julai 24 walikutana watendaji wa ngazi mbalimbali wa nchi shiriki na kujadiliana mambo mbalimbali ikiwemo namna ya kusaidia suala la ajira kwa vijana,raslimali za Afrika zitakavyoinua Uchumi,Suala la taasisi la kifedha .         

Taarifa iliyotolewa leo imeonesha nchi zilizowakilishwa na marais ni Kenya, Afrika ya Kati, Madagascar, Malawi, Sao Tome na Principe, Msumbiji na Sierra Leone.

 Aidha taarifa hiyo imesema nchi zilizowakilishwa na Makamu wa Rais ni Benin, Sudan Kusini, Zazmbia na Uganda.

Kwa upande wa nchi zilizowakilishwa na mawaziri wakuu ni Burundi, Ethiopia, Somalia, Eswatin na Cape Verde.                       

Pia wapo wawakilishi kutoka Nigeria, Algeria, DRCL Congo, Tunisia na kwingineko.

Comments

Popular posts from this blog

TMA YATOA TAHADHARI KUHUSU UWEPO WA KIMBUNGA "HIDAYA"

HUU HAPA MWENENDO WA KIMBUNGA "HIDAYA" , UPEPO KUVUMA KWA KASI YA KILOMITA 130 KWA SAA

NHIF YAFANYA MABORESHO YA KITITA CHA HUDUMA ZA MATIBABU, YAENDELEA KUPOKEA MAONI