MWENEZI TAWI LA NANE NANE MSONGOLA ACHUKUA FOMU YA UBUNGE KIVULE
Mchumi na Mkurugenzi Wa Kamarlon Microfinance, Mwezeshaji Wa Wafugaji wa Kuku na Mwenezi Wa Tawi la CCM Nane nane Kata ya Msongola Florian Karugaba amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge Jimbo la Kivule kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Karugaba amechukua fomu mapema leo Juni 29,2025 na kukabidhiwa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Ilala, Sylvester Yeredi.
Comments
Post a Comment